Home » »

Membe Akanusha kuwa na Undugu wa Damu na Kikwete


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe amekanusha uvumi ambao umekuwa ukienezwa kuwa yeye na  Rais Jakaya Kikwete ni ndugu wa damu.
 
Membe amesema kuwa japo wanafanana kwa sura lakini hawana uhusiano wowote wa kibaiolojia.

Mhe. Membe alikanusha uvumi huo  jana Mjini Dodoma wakati akichukua fomu za kuwania urais kwa tiketi ya CCM, ambapo pamoja na mambo mengine alisema ataimarisha viwanda vidogo na vya kati.

Kada mwingine wa CCM aliyechukua fomu za kuwania urais hii jana ni Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina ambaye amesema vipaumbele vyake vitakuwa ni kuboresha ukusanyaji wa kodi pamoja na usimamizi thabiti wa mapato ya kodi ili taifa liondokane na utegemezi
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog