Makala Maalumu: kumbukumbu ya safari ya kundi la Christ ambassadors kutoka Rwanda kuja Tanzania na kuwapoteza wenzao watatu katika ajali ya Gari.

Kundi la Ambasadors of christ choir Rwanda kabla ya ajali
Ambassadors of Christ Choir ni kwaya ambayo kwa sasa inafanya Vizuri sana na nyimbo zake zimekuwa Gumzo hapa nchini. Kundi hili lenye maskani yake nchini Rwanda katika jiji la Kigali hivi sasa limetimiza miezi takribani miwili tangu baadhi ya wanakikundi hicho kufariki dunia tarehe 9/05/2011  walipokuja nchini kwa mualiko wa kwaya ya Acasia Mwenge SDA ya jijini Da es salaam.

Baada ya kupata Mualiko huo, tarehe 5/05/2011 Kundi hilo lilianza safari ya kuja jijini Dar es salaam kwa ajili ya Uzinduzi wa DVD ya kwaya ya Acasia ambao ulipangwa kufanyika katika ukumbi wa PTA ulio katika viwanja vya Sabasaba jijini Dr es salaam.

Ambassadors of Christ walifanikiwa kufika Dar es salaam tarehe 6/05/2011. Kundi hili liliweza kushiriki ibada ya sabato siku ya jumamsi ya tarehe 7/5/2011 na lilialikwa katika Interview katika kituo cha Redio cha Morning Star Adventist Radio of Tanzania kilichoko jijini Dar-es salaam  kwenye kipindi kiitwacho “LULU ZA INJILI”  ambacho hungozwa na Bro Emmanuel Maduhu.

Wakiwa Redioni hapo, kundi hili lilivutia wasikilizaji wengi hasa kwa uwezo wao wa kuimba Live. Tarehe 8/05/2011 ndio siku iliyokuwa ikisubiriwa kwani ilikuwa siku Maalumu kwa kwaya ya Acasia Mwenge SDA Kufanya uzinduzi wa dvd yao ya Pili iitwayo “MNAZARAYO” katika ukumbi wa PTA.

Kundi hilo likiimba wakati wa uzinduzi wa dvd ya acasia choir katika ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam
Watu kutoka kona tofauti tofauti za jijini Dar walifurika kutaka kuwaona vijana hawa Live wakiwa jukwaani wakimtukuza Mungu. Muda uliwadia na ndipo vikundi mbalimbali vya injili vilitangulia kuimba wakiwemo Voice of Victory wakifuatiwa na Triumph Generation pamoja na Harvesters vyote vya jijini Dar es salaam.

Muda uliwadia ambapo ukumbi mzima ulizizima kwa furaha na vifijo pindi Ambassadors of Christ walipotajwa kuwa ndio wanafuata kupanda jukwaani. Taratibu huku ala ya nyimbo yao maarufu iitwayo Twapaona vijana hawa walipanda jukwani na ukumbi mzima ulizidi kupiga kelele za furaha.

Miongoni mwa nyimbo ambazo Ambassadors of Christ walizimba Live siku hiyo ni pamoja na Kazi Tufanye, Yesu Ndiye Njia, Twapaona, Kuna Siku, Huyo ni Yesu, pamoja na nyimbo yao maarufu iitwayo Kwetu Pazuri. Watu wote waliofika ukumbini hapo walibarikiwa na kazi za kundi hili kwa utukufu wa Mungu.

Kuhusu Ajali

Baada ya kumaliza huduma tarehe 8/05/2011, kundi zima la Ambassadors of Christ lilianza safari ya kurudi Kigali asubuhi ya tarehe 9/05/2011 kwa njia ya basi. Walipofika Wilaya ya Kahama mkoani shinyanga mnamo saa tatu usiku walikutana na Lorry likiwa limepaki barabarani likiwa halina reflector yeyote. Dreva wa gari la kundi hilo hakuweza kulina lorry hilo na pindi alipoliona na  kutaka kuliovatake  ndipo lorry lingine lilikuwa likija kwa kasi hivyo wakakutana uso kwa uso na ajali ikatokea.

Hali ya Gari la kundi hilo baada ya ajali
Baada ya ajali hiyo iliyotokea  kilometa kadhaa kabla ya kufika Rwanda, wanakwaya watatu wa kundi hil Filbert Manzi, Gatare Ephraim pamoja na mtanzania Amos Fares  ambaye nayee ni muimbaji wakundi hilo aliyekuwa mbele akielekeza njia walifariki papo hapo.

Muda mfupi baada ya ajali hiyo kutokea serikali ya Rwanda ilituma Helkopta ya Jeshi la ulinzi la nchi hiyo [RDF] pamoja na Ambulance mbili kwa ajili ya kusafirishia wagonjwa kutoka Kahama kwenda Hospitali ya Mkoa wa shinyanga. Baada ya kufika Hospitali ya shinyanga wahanga hao waliweza kupata huduma ya kwanza na hatimaye walikimbizwa nchini Rwanda katika Hospitali iitwayo King Faisal kwa matibanu zaidi.

Helkopta ya Jeshi la ulinzi la Rwanda iliyofika kwenye eneo la ajali
Kwa msaada wa Mungu majeruhi wane wa ajali hiyo walipata nafuu na hatimaye kurutuhusiwa kutoka Hospitali. Taratibu za mazishi zilifanywa ambapo Marehemu Filbert Manzi aliyekuwa mmoja wa vingozi wa kwaya hiy na pia mtangazaji wa kitu kimoja cha Redio nchini Rwanda, pamoja na Gatare Efraimu ambaye alikuwa ni muanzilishi na kiongozi wa kwaya hiyo wa walizikiwa nchini Rwanda, wakati Mtanzania Amos Fares yeye alizikiwa nyumbani kwao  mkoani Kigoma.

Zifuatazo ni baadhi ya matukio ya kundi hilo wakati wakiimba jijini Dar na baada ya ajali hiyo.

Majeruhi
Pichani ni kijana Marc Ndizaye kabla na baada ya ajali ila yeye aliruhusiwa baada ya matibabu

Baadhi ya Majeruhi kabla na baada ya ajali
Waliotangulia
Hawa ndio watumishi waliopoteza maisha kufuatia ajali hiyo

Hili ndio kava la Album yao ambapo kushoto mstari wa juu vijana hao watatu Ephraim, Filbert, na Mtanzania Amos hawako nasi tena


Miili ya marehemu Ephraimu na Filbert ikiwa nchini Rwanda

Miili yao ikiwa kanisani

Ephraim ambaye alikuwa kiongozi na muanzilishi wa kwaya hiyo

Philbert Manzi katika siku za utumishi wake chini ya jua


Safari ya Mwisho ya Philbert Manzi

Hatimaye muda huu uliwadia na kuacha simanzi zito

 Mungu anabaki kuwa Mungu kwa lolote afanyalo juu yetu kwa ajili ya Utukufu wake

Hii ni kazi yao iitwayo NI VEMA ambayo inafanya Vizuri sana hapa nchini

HABARI PICHA: KILICHOTOKEA KANISA KATOLIKI PAROKIA YA MTAKATIFU JOSEPH, ARUSHA


Wananchi wakikimbia kuelekea barabarani kutoka Kanisa katoliki, Parokia ya Mtakatifu Joseph iliyokuwa izinduliwe jana na balozi wa kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa Benedict, Askfou Francisco Montecillo Padilla.
Sehemu ya mbele ya kanisa katoliki Parokia ya  Mtakatifu Joseph, Olasiti, Arusha.
Huzuni ikiwa imetanda kwa masista kanisani hapo.

Askari Polisi wakichukua sampuli eneo la tukio.
Wapelelezi wakiendelea na kazi yao eneo la tukio.

vikosi vya kila aina, ndani ya uniofrm na bila uniform.
Ufute wa polisi ukizungushiwa kuzuia watu kuingia eneo la tukio.
Taswira ya ndani ya kanisa hilo jipya,

RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU AWATAKA WAKRISTO NCHINI KUONGEZA KASI YA SALA

Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa

=====================================
Na Gustav Chahe, Iringa              
RAIS wa Baraza la Maakofu Tanzania (TEC) Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa amewataka waamini wakristo kutokuwa na moyo wa kuhamaki kutokana na kitendo kilipuliwa Kanisa Katoliki huko Arusha.
Amezungumza hayo katika mahojiano maalum mtandao  huu wa www.matukiodaima.com mahojiano  yaliyofanyika ofisini kwake Iringa juu ya vitendo vinanyoendelea kutokea nchini vikiwemo vya kuchomwa makanisa na kuuawa wachungaji wa kiroho huku vikihusishwa na imani za kidini.
Amesema kama ilivyoutamaduni wa Kikristo, yanapotukia matukio ya kusikitisha kama hayo silaha iliyo kubwa ni sala kumuomba Mungu atoe jibu kwa wanaohusika na mateso kama hayo.
“Kasi ya sala iendelee, ili Mungu wetu wa Amani ajenge fikira za upendo na haki katika mioyo yetu” alisema.
Amesema waamini wasikate tamaa na kuacha kusali kwa kuwa Mungu ndiye mwenye jibu na atatoa majibu kadiri atakavyo kwa wale wote wanaowatesa wenzao kwa sababu zao binafsi.
Hata hivyo alisema licha ya kuwa kila mtu amepokea kwa mshituko na maumivu makubwa, roho za watu zinazoteswa na wengine Mungu atazifariji na kuziponya lakini mtesaji atapata majibu yake.
Alisema waliopoteza maisha katika mlipuko huo Mungu atawarehemu na kuwafariji majeruhi wote.
“Waliopoteza maisha wapokee Rehema ya Mungu na waliojeruhiwa wafarijiwe na uwezo wa Mungu” alisema.
Hali kadhalika amesema upendo na haki ni zawadi kutoka kwa Mungu na hivyo, anayedhurumu wengine zawadi hiyo atapata pigo kubwa.
Aidha amesema wakati uliopo sasa ni wakutafakari na kumkabidhi Mungu yale yote yanayowasumbua wanadamu na kuongeza nguvu ya sala ili majibu ya Mungu yapatikane kwao.
“Tulieni na kufanya tafakari kasha mwambie Mungu hayo yote ayafanyie kazi kwa uweza wake. Sisi binadamu tunategemea nguvu kutoka kwake” alisema.

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog