MANJI AJIZUIA KUTOA MACHOZI MAHAKAMANI

TAPELI WA MTANDAONI AKAMATWA NA JESHI LA POLISI MKOANI IRINGA

TUNDU LISSU AMVAA WAZIRI WA MAGUFURI KUHUSU NDEGE

WATOTO WATATU WA LUCKY VICENT WALIOWASILI LEO WAWALIZA WATANZANIA WALIOENDA KUWAPOKEA UWANJA WA NDEGE WA KIA

Wazazi, watoto na watu mbali mbali wameshindwa kujizuia na kumwaga chozi walipokuwa wakiwapokea watoto Sadia Ismail, Doreen Eribariki na Wilson Tarimo, ambao wamerejea rasmi nchini wakitokea nchini Marekani walikokuwa wakipatiwa matibabu.
Watoto hao ambao ni manusura wa ajali iliyoua takriban wanafunzi 32 wa shule ya msingi Lucky Vicent, wamepokelewa na viongozi mbali mbali wa serikali wakiwemo Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Bi. Anna Mghwira, Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu, wazazi na wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent, waliwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Watu mbali mbali walihudhuria uwanjani hapo wakiwa na mashada ya maua kuwalaki huku kukiwa na burudani mbali mbali kutoka kwa sanii Mercy Masika wa Kenya, Angel Bernad wa Tanzania na Kwaya ya Shangwe kutoka jijini Arusha.

Shirika la Samaritan Purse la Marekani lilijitolea kusaidia watoto hao kuanzia usafiri na gharama za matibabu kwa muda wote ambao walikuwa nchini humo wakitibiwa, katika Hospitali ya Sioux City tangu mwezi Mei 15, kufuatia majeraha makubwa kwenye ajali kubwa waliyoipata tarehe 6 Mei 2017, wakitokea hospitali ya Mt. Meru Arusha.

Polisi Afrika Kusini wapiga kambi mipakani kumzuia mke wa Rais Mugabe





Maafisa wa polisi wa Afrika Kusini wametoa tahadhari dhidi ya Mkewe rais Mugabe katika mipaka ya taifa hilo , waziri wa polisi nchini humo amesema.
Ametuhumiwa kwa kumpiga na kumjeruhi mwanamke wa miaka 20 katika kichwa chake katika chumba cha hoteli karibu na mji wa Johannesburg .
Polisi wanatariaji kwamba Bi Mugabe mwenye umri wa miaka 52 alipaswa kujiwasilisha mbele yao siku ya JUmanne lakini akakataa kufanya hivyo.
Bi Grace mugabe kwa sasa hajulikani yu wapi lakini inaaminikwamba bado yupo Afrika Kusini.
Gabnriela Engels
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe pia amewasili nchini Afrika Kusini kwa kikao cha viongozi wa mataifa ya Afrika Kusini SADC unaotarajiwa kuanza siku ya Ijumaa.
Bi Mugabe hajatoa tamko lolote kuhusu madai hayo.
Waziri wa polisi Fikile Mbalula alisema: Sisi polisi wa Afrika Kusini tayari tumeweka notisi katika mipaka yetu yote ili kumzuia bi Mugabe kuondoka nchini siku ya Jumatano, wakili wa Afrika Kusini Gerrie Nel aliyefanikiwa kumshtaki mwanariadha mlemavu Oscar PIstorius anamuunga mkono mwanamke anayemtuhumu bi Mugabe kwa kumpiga, Gabriela Engels.
Bwana Nel sasa anashirikiana na kundi la Afriforum ambalo linapigania haki za Afrikaners nchini Afrika Kusini.
Kundi hilo limesema kuwa iwapo polisi watashindwa kuchukua hatua katika kesi hiyo basi litamshtaki bi Mugabe.

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog