MAMLAKA YA MAJI MKOA WA IRINGA IRUWASA YAMNASA MWIZI WA MAJI ALIJIINGIZIA KINYEMELA.

Afisa mahusiano wa iruwasa bi restuta akihakikisha bomba la ndani likitoa maji ndani ya nyumba iliyokuwa ikitumia maji kwa zaidi ya miezi mitatu.



wa kwanza kulia ni mtuhumiwa wa wizi wa maji akitoa maelezo kwa mamlaka ya maji mkoani iringa baada ya kugundulika akitumia maji bila kulipia.




Jitihada za kupambana na maji zinazofanywa na mamlaka ya maji iruwasa zimeaanza kuzaa matunda baada ya leo kufanikiwa kumkamata mwizi mmoja katika mtaa wa kihodombi manispaa ya iringa.
akizungumza na mtndao huu afisa uhusiano wa idara ya maji bi restuta amesema taarifa za wizi huo zimetolewa na wanainchi wasamaria baada ya kugundua kuwa mwanainchi alijiingizia maji kinyemela.
Akizungumza mara baada ya kukamatwa mwanainchi huyo aliyefahamika kwa jina la lugenge amesema usumbufu wa watu wa ardhi ndio uliopelekea yeye kufanya kitendo hicho.
Afisa mahusiano huyo ameongeza kuwa madhara yatokanayo na watu kujiingizia maji kuwa ni pamoja na watumiaji sahihi wa maji kulipa bili kubwa ,pia ameongeza kuwa bado wataendelea na msako ili kuwabaini wote walioingiza maji bila idhini yao.

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog