MAMIA WAMIMINIKA KATIKA KONGAMANO LA MAOMBI NA MAOMBEZI KWA KATUNZI

Mamia ya wakazi wa jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake wanamiminika katika kongamano kubwa la maombi na maombezi lililoandaliwa na kanisa la E.A.G.T City Centre chini ya mchungaji wake kiongozi Florian Katunzi katika ukumbi wa PTA uliopo viwanja vya mwalimu JK Nyerere zamani Sabasaba.

Kongamano hilo la siku nane lililoanza siku ya jumapili nakutarajiwa kumalizika jumapili hii linatarajia kupambwa na waimbaji mbalimbali wa gospel nchini wakiongozwa na Bahati Bukuku, Masanja Mkandamizaji, Flora Mbasha, Martha Mwaipaja, Solomon Mukubwa, Madam Ruti, Bonny Mwaitege na waimbaji wengine lukuki zikiwemo kwaya za kanisa hilo.

Ambapo toka jumapili tayari uwepo wa Mungu umeanza kujidhihirisha ukumbini hapo kwa watu mbalimbali kupokea uponyaji na kufunguliwa kutoka katika vifungo mbalimbali vya ibilisi ambapo kwa watu wasiofika katika ukumbi huo wanapata yanayojiri kwakusikiliza Wapo Radio FM inayorusha matangazo ya moja kwa moja kutoka ukumbini hapo.

  CHEKI BAADHI YA PICHA KUTOKA KATIKA KONGAMANO HILO TOKA LILIPOANZA.
Mchungaji Florian Katunzi akiwaongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar katika maombi.
Solomon Mukubwa kutoka Kenya akiita uwepo wa Mungu katika kongamano hilo.

Martha Mwaipaja wa John Saidi akimtukuza Mungu.
Solomon Mukubwa akimpiga picha Martha Mwaipaja wakati akiimba.
Picha ya Juu ni Waimbaji Madam Ruth pamoja na Martha Mwaipaja wakiwa na Solomoni Mukubwa kwa Pamoja wakimsikiliza Mtumishi wa Mungu wa Mungu Mchungaji Frolian Katunzi wakati akitamka Neno la Baraka kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam.
Mchungaji mtarajiwa a.k.a Masanja Mkandamizaji akipiga gombo la uimbaji katika kongamano hilo.
Sio utangazaji tu hata uimbaji ni balaa, anaitwa Silas Mbise ambaye pia ni mtangazaji wa Wapo Radio Fm akimtukuza Mungu katika kongamano hilo,
Flora Mbasha na mumewe mpenzi Emanuel Mbasha wakimsifu Mungu kwa pamoja.
Eveline Msoome nayeye hakuwa mbali katika kumsifu Mungu.
Kijana mwenye mavocal Samuel Limbu akimsifu Mungu katika kongamano hilo.
Mchungaji Yohana Mwegoha akimsifu Mungu. picha kwa hisani ya Yonathanlanda.blogspot.com

MAMA AMCHOMA MTOTO MOTO NA KUMLISHA KINYESI CHA MAMA MDOGO WAKE

 mtoto anety akionesha jeraha alilounguzwa na mama yake

 mama ambaye jina lake halikufahamika akiwa amembeba mtoto tayari kwa kumpeleka hospitalini
MTOTO aliyejulikana kwa jina moja la Aneth (pichani) anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka miwili, mkazi wa eneo la Majengo Kaskazini jijini Mbeya ameunguzwa vibaya mwili wake na kulazimishwa kula kinyesi na Mama yake Mdogo aliyejitambulisha kwa jina la Revina.

Tukio hilo la kikatili liligundulika jana eneo hilo majira ya saa tano asubuhi ambapo mwandishi wa habari hizi alifika eneo la tukio na kuukuta umati wa watu na mtuhumiwa akimuogesha mtoto huyo.

Mtoto huyo alipoulizwa kuwa ilikuwaje, aliongea kwa woga akisema kuwa alikuwa amefungwa mkono na kumwagiwa maji na kupigwa.

Mtuhumiwa huyo alipohojiwa alikataa kusema chochote na kuishia kutaja jina lake moja la Revina, kisha wananchi wakaamua kumchukua mtoto huyo na mtuhumiwa na kuwapeleka kituo cha Polisi cha Kati.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa baada ya kutomuona mtoto huyo mwenye historia ya kuteswa na mama yake huyo mdogo anayeelezwa kuwa mama yake mzazi, Bahati Mkandara alifariki, wakaamua kumuuliza binti huyo ambapo aliwajibu kuwa mtoto huyo alikuwa kucheza na walipompiga ndipo akaamua kukimbilia chumbani na walipoingia wakamkuta mtoto amesimama akiwa uchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti  wa Mtaa wa Majengo Kaskazini, Shack Mwakanyamale alisema kuwa binti huyo amezoea kumtesa mtoto huyo huku mtoto wake akiwa na afya njema ambapo aliwatuliza wananchi wenye hasira kali na kuongoza msafara wa kumpeleka katika kituo cha polisi mtuhumiwa huyo

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog