HAKIKA KUMTEGEMEA MUNGU INALIPA


 HEBU MWANGALIE MWIGIZAJI MFILIPINO AMBAYE NI MTU ANAYE MJUA MUNGU KWELIKWELI

Mwigizaji huyu ni kati ya waigizaji wanaompenda Mungu ambapo mpaka sasa bado yupo katika ndoa yake na mkewe mpenzi Glydel Mercado ambaye pia ni mwigizaji, kabla ya ndoa uhusiano wao ulidumu miaka 6 kisha alimvalisha pete ya uchumba mkewe baadaye ndani ya miezi 2 aliweza kufunga naye ndoa. Wasimamizi wao ni marafiki wao wakubwa mwanamama Lorna Tolentino (Red Butterfly) pamoja na marehemu mumewe Rudy Hernandez. Mwigizaji huyu ametoka katika familia ya wasanii baba yake mzazi Eddie Gutierrez na mama yake pamoja na ndugu zake waigizaji kama yeye.











Msanii Lorna Tolention(Red Butterfly) wa kwanza baada ya bibi harusi, pamoja na marehemu mumewe baada ya Eduardo bwana Rudy Hernandez walikuwa ndio wasimamizi wa harusi hiyo.



                                

PADRI AFARIKI BAHARINI WAKATI AKIOGELEA



Mkuu wa Shirika la Kitawa la Consolata la Kanisa Katoliki nchini, Padri Salutaris Massawe (pichani) amefariki Dunia baada ya kuzidiwa na maji ya Bahari wakati akiogelea katika ufukwe wa Pwani ya Bagamoyo Oktoba 25.


Padre huyo ambaye alikuwa yupo Bagamoyo kwa shughuli za shirika lake, alizidiwa na maji hayo ambayo yalimchukua majira ya alasili ya siku hiyo wakati alipokuwa akiogelea pamoja na wageni wa shirika hilo walioitembelea Bagamoyo. 


Mwili wa Marehemu Padri Salutaris Massawe ulipatikana jana asubuhi katika fukwe hiyo ya Bagamoyo.
Akizungumzia tukio hilo mbele ya Ripota Wetu, Katibu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Joseph Masenge alikiri kutokea kwa kifo cha Padri huyo, ambapo padri huyo alifariki baada ya kuchukuliwa na maji alipokuwa akiogelea juzi saa tisa alasiri (kwa saa za Afrika Mashariki) na mwili wake kuonekana jana asubuhi ufukweni.


Padri huyo alikuwa akiogelea baharini karibu na Msalaba Mkuu wa Bagamoyo
Hadi jana mchana Padri Masenge alisema walikuwa katika maandalizi ya kuusafirisha mwili wa Padri Salutaris Massawe kuja Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuuhifadhi wakati mipango ya mazishi ikiandaliwa.


Naye, Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam,Eusebius Nzigirwa alisema kifo cha padri huyo kimeacha pengo kubwa kwani wamepoteza mtu mchapakazi na aliyefanya kazi kwa mipango.
Alisema anamfahamu Padri Massawe kwani aliwahi kufanya kazi katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam kabla ya kuchaguliwa kuwa Mkuu wa shirika hilo ambapo aliwajibika vizuri katika kusimamia majukumu yake.


Alisema kwa taarifa alizozipata awali, Padri huyo alikwenda Bagamoyo na wageni wa shirika ambao walitaka kupata historia ya jinsi Ukristo ulivyoingia nchini pamoja na historia nzima ya Ukristo.

ASKOFU MKUU WA TANZANIA ASSEMBLIS AZINDUA MAABARA YA KISASA KATIKA SHULE YA SEMINARY EBENEZER MKOANI IRINGA

Wito umetolelewa kwa wanafunzi wanao hitimu kidato cha nne hapa nchini kuweza kuendeleza nidhamu zao hata baada ya kuhitimu kwani hiyo ndo njia pekee itakayowawezesha wanafunzi kufaulu na kukamilisha malengo yao ya hapo baadae.

Wito huo umetolewa na Askofu mkuu wa kanisa la Tanzania assemblia of god   Dr Barnabas Mtokambali katika mahafali ya tatu ya kidato cha nne ya shule ya seminary ebenezer iliyopo nduli jirani na uwanja wa ndege manispaa ya iringa.

Ambapo mbali na maafari hayo Askofu Mtokambali aliweza kuzindua rasmi maabara ya kisasa itakayo wasaidia wanafunzi wote wanaosoma masomo ya sayansi Mtokambali alisema iwapo wanafunzi watafuata nidhamu waliyofundishwa na kuionyesha  katika jamii zao hakika hakutakuwa na mwanafunzi wa kufeli hata mmoja kwa anaamini kuwa nidhamu ndio chanzo kikuu cha mafanikio.

Hata hivo alimpongeza mwalimu mkuu wa shule hiyo bw.makweta na kuaahidi kusaidiana katikachanga moto mbalimbali zinazohusu shule hiyo kama tatizo la maji ambapo askofu mkuu aliahidi million mbili katika kufanikisha na kutatua jambo hilo, na zaidi ya millioni sita zilichangiashwa katika kutatua sual;a la maji .

Kwa upande wake  mkuu wa shule ya ebenezer alimpongeza askofu mkuu pamja na uongozi wa jimbo  la iringa uliongozwa na Askofu Jonas Mkane pamoja na makamu wake Edward Tom Matipa kwa uwepo wao katika kufanikisha zoezi zima la mahaafari pamoja na uzinduzi wa maabara ya kisasa kwa wanafunzi wa shule hiyo.




Askofu mkuu wa tanzania assemblis of god wakati akiwasili katika shule ya ebenezer




Askofu mkuu wakati akizindua rasmi maabara ya kisasa


Asikofu  wa jimbo la iringa jonas mkane akifungua kwa maombi sherehe


makamu askofu wa jimbo la iringa rev edward tom matipa




baadhi ya majengo ya shule ya ebenezer seminary

wahitimu wakicheza kwaito kwa pamoja



KANISA LA BETHEL PENTECOSTE BUZA NALO LAPATA KISANGA CHA MOTO

Wakati jeshi la polisi na lile la wananchi (JWTZ) waliweza kutuliza hali ya uvunjifu wa amani ikiwa pamoja na maandamano yaliyokuwa yamepengwa kufanywa na waumini wa dini ya kiislamu kuelekea ikulu ili kushinikiza kuachiwa huru kwa sheikh Ponda Issa Ponda na waumini wengine wa dini hiyo waliokamatwa kwa tuhuma za kuchochea vurugu za kidini nchini.

Huko Buza njia panda ya kuelekea Kitunda jijini Dar es salaam, watu wasiofahamika wamelichoma moto upande mmoja kanisa la Bethel Pentecoste linaloongozwa na mchungaji Emanuel Kapama majira ya usiku wakati waumini wakiwa tayari majumbani mwao.

Kwa mujibu wa mchungaji Kapama amesema jana walikuwa na ibada kuanzia majira ya saa 1 usiku hadi saa 2 kisha kutawanyika lakini waliporejea asubuhi wakashangaa kukuta kanisa lao limechomwa moto upande mmoja na kukuta chupa ya mafuta ya taa ambayo imechukuliwa na jeshi la polisi kwa  ushahidi ikiwa ndani ya kanisa hilo huku watu hao wakiwa wameshamwaga mafuta ya taa kanisa zima ambalo limezungushiwa kwa mabati pamoja na mifuko migumu aina ya viroba.

Ambapo kwa mujibu wa mchungaji huyo amesema jeshi la polisi tayari limefika na kuangalia kilichotokea na kuchukua vitu ambavyo vitatumika kwa ushahidi ikiwemo chupa hiyo ya mafuta ya taa.
Moja ya kanisa lililochomwa moto huko mkoani Kigoma wiki hii. picha by Fungo Omary.

MAKANISA 2 YOMBO NUSURA KUCHOMWA MOTO, MAASKOFU LUTHERAN WATOA SALAMU JUU YA VITENDO HIVYO

Watu wasiofahamika usiku wa kuamkia leo wamevamia kanisa la kilutheri Yombo jijini Dar es salaam kwa lengo la kufanya uharibifu kanisani hapo majira ya saa 9 kasoro za usiku lakini walinzi wa kanisa hao walifanikiwa kuzuia zoezi lao hilo.

Kwa mujibu wa mmoja wa watu waliofika kutoa msaada baada ya walinzi hao kugonga kengele iliyowaamsha wakazi wa eneo hilo ambaye pia husaidia kazi ya ulinzi kanisani hapo bwana Hosea Mbwambo amesema vijana wapatao saba waliingia kanisani humo kwa kuruka ukuta kwa nia ya kwenda madhabahuni lakini mlinzi aliyekuwepo aliwaambia mnataka nini ndipo walipomfuata nakusema kwamba tunakutaka wewe nakuanza kumpiga kabla mlinzi mwingine aliyekuwepo gorofani kushuka ili kusaidia ndipo vijana hao wakagundua kwamba kuna walinzi wengi hivyo kuamua kutimua mbio lakini wakiwa wamemuachia jeraha mlinzi Nkya ambaye alipelekwa hospitali ya Buguruni kisha Amana kwa matibabu zaidi hali yake inaendelea vizuri pia ulinzi ukiwa umeimarishwa kanisani hapo.


Pia habari ambazo GK imezipata kutoka kwa chanzo kingine cha habari ikiwemo Wapo Radio Fm inasema kwamba watu wasiofahamika waliwasha moto katika kanisa la Faraja International Gospel lililoko huko huko Kiwalani ingawa watu waliweza kuudhibiti baadaye. Wakati huo huo maaskofu wapatao 20 wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT) wakiongozwa na mkuu wa kanisa hilo Dkt. Alex Gehaz Malasusa, wamekutana hii leo katika kanisa lililofanyiwa uharibifu la Mbagala na kutoa tamko zito juu ya vitendo vilivyofanywa na waumini wa dini ya kiislamu dhidi ya makanisa ya eneo hilo.








Baadhi ya picha za tukio la leo huko Mbagala kama zilivyotolewa na Samsasali.blogspot.com

JE? MWIMBAJI WA ''MY GOD IS GOOD'' PASTOR UCHE AMEJITOA JOYOUS CELEBRATION?

Pastor Uche akiimba Solid Rock ndani ya Joyous 15 part 2.
Baada ya kuwemo ndani ya kundi la Joyous Celebration kwa takribani miaka 5, mwimbaji aliyejipatia umaarufu sana duniani ikiwa pamoja na kulitangaza vyema kundi hilo Pastor Agu Uchechukwu au unaweza kumuita Pastor Uche a.k.a Double double yawezekana album ya 16 ndio ilikuwa ya mwisho kwa mwimbaji huyo akiwa na kundi hilo.

Hali hii yakujiuliza maswali kama haya ni hivi karibuni JC imetangaza tarehe ya kurekodi album yao mpya ya 17 ambayo itafanyika mwezi December, mwimbaji Pastor Uche siku chache kabla kupitia katika moja ya kurasa zake za Facebook aliaga kwamba anaelekea nchini Marekani na kuongeza kuwa kurudi kwake nchini Afrika ya kusini hadi mwezi wa tatu mwakani 2013 jambo ambalo linatafsiri kama mwimbaji huyo hayumo tena kundini humo.

Tangu JC ianze tour ya kutangaza album yao ya 16, pastor Uche hakuweza kuhudhuria takribani maonyesho yote kutokana na mialiko anayoipata huko nchini Marekani. Ambapo kwasasa anapanga kurekodi DVD yake ya pili Live huko Houston nchini Marekani, kama ni kweli atakuwa ameachana na kundi hilo inamaanisha atakuwa amebakia kijana mzimbabwe Mkhululi anayeimba nyimbo zinazo kwenda sambamba na Uche au kundi hilo litakuwa mbioni kutafuta mtu wa kuchukua nafasi yake.

Moja ya ratiba zake alizoweka katika ukurasa wake wa FB inaonyesha kabisa kwamba hatarekodi album mpya na JC mwaka huu kwani siku ambayo kundi hilo linarekodi yeye atakuwa na show sehemu nyingine

WANANCHI RUKWA WATEKETEZA SHAMBA LINALOMILIKIWA NA KANISA LA EFATHA

Shamba la Malonje linalomilikiwa na Kanisa la Efatha limepata hasara kubwa baada ya wananchi wa kijiji cha Sikaungu wilayani Sumbawanga vijijini mkoani Rukwa, kujichukulia sheria mkononi na kuvamia moja ya kambi ya mashamba hayo ijulikanayo kama sikaungu na kuyateketeza kabisa matrekta mawili makubwa mawili aina ya New Holland na kubomoa baadhi ya nyumba zilizopo katika kambi hiyo.

Mchungaji kiongozi Michael Meela wa kanisa la Efatha mkoani Rukwa akiongelea kuhusu suala hilo amesema hasara iliyopatikana kutokana na tukio hilo ni zaidi ya shilingi milioni 228 na tukio hilo lilitokea baada ya mbunge wa jimbo la Kwela Mh. Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo na kuwahamasisha wanachi watumiee nguvu ya umma kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.

MWIMBAJI ANAYEIBUKIA KATIKA UIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KIJANA DANNY SANGA AFANYA MAKUBWA IRINGA KATIKA UKUMBI WA IDYDC



                                  Hapa mwimbaji danny akionesha utundu aliopewa na mungu
 hakika ukumbimni palikuwa hapatoshi kila mmoja alitamani kuruka hadi juu




 baadhi ya umati wa watu waliohudhuria katika huduma ya overcomers power center

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog