HEBU LEO TAFAKARI   TOFAUTI YA KIONGOZI NA MTAWALA

Mchungaji Peter Mitimingi, mkurugenzi wa The Voice of Hope Ministries (VHM)

KIONGOZI

1. Ni mtu wa Watu
• Kiongozi kipaumbele chake ni watu
• Anakuna kichwa afanye nini ili watu wake waweze kuishi kwa amani na furaha.
• Kupenda kuwasikiliza watu wanasema nini, wanalia juu ya nini, wanacheka juu ya nini nk.

2. Hugusa Moyo wa Mtu
• Mkono wa kiongozi hugusa moyo wa wafuasi.
• Ushawishi wake kiongozi huwa sio wa akilini au kichwani bali hupenya hadi ndani ya moyo wa mtu.
• Anauhakika wa kuwa na watu nyuma yake kumfuata popote atakapo kwenda

3. Huuliza Kuna nini Moyoni
• Hutaka kujua nini kimeujaza moyo wako
• Mbona huna furaha moyoni kumetokea nini? Nifanye nini kukusaidia furaha ya moyo wako iweze kurudi.
• Mbona unafuraha sana leo nini kimetokea mpaka umekuwa mwenye furaha hivyo moyoni? Unahitaji kuendeleza hiyo furaha yako.

4. Hufundisha Watu
Kiongozi hufundisha wato na sio kufundisha somo
Kiongozi hutamani hata Yule mbumbumbu asiyeelewa darasani au kanisani ameelewa na kupokea kitu.
Huchukua juhudi za makusudi kufuatilia zaidi.
Kipimo chake cha uwelewa wa wanafunzi ni Yule mtu wa mwisho kuelewa darasani.

5. Ana upeo wa Kuona Mbali
• Huangalia faida itakayopatikana kule mbele sio lazima sasa.
• Anawekeza sasa kwaajili ya sasa na badae
• Anawekeza vikubwa anavuna vikubwa pia.
• Anafanya leo kwajili ya kesho

6. Ni Mbunifu na Muanzishaji (Originate)
• Anamawazo mapya
• Anabuni na kuwapa wengine
• Anaweza kubuni na kupitisha barabara katikati yam situ mnene mahali usingefikiri kamwe barabara ingepita
• Ni mvumilivu kusubiria matunda kwa wakati wake.
7. Hujiuliza Nini na Kwanini (What and Why)
• Ninafanya nini na kwanini ninafanya hiki.
• Huwa na sababu ya kutosha kumuwezesha kufanya anachokifanya kwa nguvu zaidi.

MTAWALA
1. Ni Mtu wa Vitu
• Kitu cha muhimi kwake ni vitu sio watu.
• Kama ni mmiliki wa basi, likipinduka chakwanza kuuliza gari imesalimika haijaumia?
• Akiambiwa mzee gari imepona ila watu wote wamevunjika vunjika na kufa atasema afadhali.
• Akiambiwa gari imesagiga sagika hakuna hata cha kuokota ila watu wote wamesalimika ataangua kilio kweli maana gari imekwisha.

2. Hugusa Vitu vya mtu
• Tofauti na kiongozi mtawala hagusi moyo anagusa vitu
• Mitambo au vitu nivyamuhimu sana kuliko watu.
• Chombo kikiungua ni hasara kubwa sana lakini mtu akivunjika mguu ni kawaida ajali kazini.

3. Huuliza Kunanini mfukoni
• Tofauti na kiongozi ambaye huuliza kunanini moyoni, interest ya mtawala nikujua kuna nini mfukoni.
• Hugusa pochi na sio moyo
• Hugusa kichwani na sio Moyoni
4. Hufundisha Somo
• Hufundisha somo watu na sio kufundhisha watu somo
• Hufundiaha kumaliza mtaala na sio kufundisha kuwaelimisha.
• Hufundisha kwa kuwapa wanafunzi taarifa, na sio badiliko la maisha.
• Teaching for information not transformation.
5. Ana upeo wa Kuona ya Sasa
• Hushughulika sana na ya sasa.
• Macho yake ni dhaifu hayana nguvu ya kuona ya mbele.
• Anataka kupanda leo na kuvuna leo.
• Hana mpango wa kuwekeza kwaajili ya baadae.

6. Huiga na kukarabati Kilichokuwepo (Immitate)
• Hana uwezo wa kubuni vitu vipya.
• Yeye huendeleza walivyobuni wengine
• Kama ni barabara hana uwezo wa kubuni barabara mpya ataziba tu viraka vya barabara aliyokabidhiwa.
• Kama ni kanisa akipewa hata kama likijaa hawezi kuja na mpango mpya wa kujenga linguine la kisasa bali atakuwa anabadilisha tu milango na kupiga rangi upya nk.

7. Hujiuliza Kivipi na Lini (How and When)
• Nitafanyaje hiki nilichopewa kiendelee kuonekana kizuri?
• Lini nitaweza kutekeleza hii kabla sijanyan’ganywa madaraka haya?

NB: VIONGOZI WENGI TUNAO WAITA “VIONGOZI” KIUKWELI SIO VIONGOZI NI WATAWALA

WAPENDA MIUJIZA, HIKI NDICHO KINACHOWAPATA

Mtume Lesego Daniel.
Leo bado tupo nchini Afrika ya kusini, kuhusiana na huduma ya mtume Lesego Daniel iitwayo Rabboni Centre ministries ambayo inaendelea kujizolea waumini kila kukicha licha ya aina ya ufunuo unaotumiwa na muasisi wa huduma hiyo mtume Lesego kuleta ualakini kama kweli umetoka kwa Mungu, hasa kitendo cha kuwataka waumini wake kula manyasi na majani ya miti lakini pia mda mwingine kuwafanyia maombi akiwa amewakanyaga.

GK imeamua kuandika tena hii leo kuhusiana na huduma hii, mara baada ya kuona video fupi iliyorekodiwa na mchungaji Thami Dlalisa wakati akiangalia kipindi kwenye runinga kilichokuwa kikionyesha huduma ya mtumishi Lesego akiwa amemrukia kwa juu kwa kumkanyaga kwa nguvu mwanadada aliyekuwa amelala chini kwa ajili ya maombi kitendo ambacho pia kilisikika sauti ya waumini wake ikionyesha mstuko namna dada huyo atakavyohimili uzito wa mchungaji huyo.

Katika maelezo yake mchungaji Dlalisa ambaye alirekodi video fupi ambayo ipo chini, amewataka marafiki zake wa facebook kuangalia video aliyorekodi yenye dakika 12 na kuwataka maoni yao wanafikiriaje watakachokiona, mchungaji anamrukia muumini wake wakati wengine wamesimama kama mazombi huku wengine wamekaa kama wanatazama igizo. Ambapo watu walioweka maoni yao walionekana kuponda sana huduma hiyo huku wengine pia wakisema hata waumini nao pia wanachangia kwa kupenda kufuata miujiza.

ISRAEL HOUGHTON KUIMBA NCHINI UGANDA MWEZI UJAO, HAKUNA KIINGILIO

Watoto Children Choir namba 66 wakiimba kanisani kwao kabla ya kuelekea nchini Australia kwa ziara wiki mbili zilizopita.
Nyota wa muziki wa injili duniani Israel Houghton kutoka nchini Marekani anatarajiwa kuwa mwimbaji mwalikwa katika sherehe za kutimiza miaka 30 ya huduma ya kanisa la Watoto Uganda pamoja na miaka 20 ya huduma ya wanawake na watoto kupitia Watoto child care ministries zote zikiwa chini ya kanisa la Watoto ambalo umaarufu wake umetokana na kwaya ya Watoto children chini ya waanzilishi wa huduma hiyo Gary na Marilyn Skinner  zitakazofanyika mwezi wa sita nchini
humo.

Israel na kundi lake la New breed wanatarajiwa kuimba siku ya alhamis tarehe 5 katika kanisa la Watoto west tukio ambalo halitakuwa na kiingilio lililopewa jina la 'Watoto Big Party'. Hii itakuwa si mara ya kwanza kwa mwimbaji huyo kuimba jukwaa moja na Watoto children choir ambao amekuwa akikutana nao sehemu mbalimbali. Mwimbaji huyo atakuwa nchini Uganda wiki moja baada ya kumaliza tamasha lake kubwa la uimbaji litakalofanyika jijini London nchini Uingereza tarehe 27 mwezi wa tano akiwa na kundi lake kamili.

Haya kwa wale wapenzi wa mwanamuziki huyo, ni kujipanga nauli ya kwenda na kurudi na sehemu ya kufikia bila kusahau chakula, onyesho halitakuwa na kiingilio.

PSPF YAIPIGA JEKI SERIKALI YATOA MSAADA WA MADAWATI 100 KWA SHULE ZA MSINGI

Afisa Mfawidhi  Mfuko wa Pensheni kwa watumishi (PSPF)Mkoa wa Iringa, Baraka Jumanne akizungumza na waalimu wa Shule za Msingi tatu Mufindi Kaskazini(hawapo pichani)  kabla ya kukabidhi madawati 100 yaliyotolewa na mfuko huo.
Afisa Mfawidhi PSPF Iringa,Bakari Jumanne akimkabidhi Mkuu wa Wilaya Mufindi Evarista Kalalu Madawati miamoja kwa ajili ya Shule za Msingi Mjimwema, Mamba na Nyamalala yenye thamani ya sh. milioni 5 katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Mufindi.
 Baadhi ya madawati yakiwa ndani ya lori kabla ya kukabidhiwa kwa shule za msingi 3 za Mufindi Kaskazini.(picha zote na Denis Mlowe)

SHULE tatu za msingi za jimbo la Mufindi Kaskazini katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa zimenufaika kwa msaada wa madawati 100 yaliyotolewa na mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) yenye thamani ya shilingi milioni 5.
Akikabidhi msaada huo kwa mkuu wa wilaya ya Mufindi Monica Kalalu juzi katika ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo, Afisa Mfawidhi wa PSPF mkoa wa Iringa Baraka Jumanne alisema lengo la msaada huo ni sehemu ya mpango wao katika kusaidia sekta ya elimu nchini na kukuza elimu ya shule za msingi katika wilaya hiyo.
 "PSPF ni shirika la mfuko wa pensheni hivyo faida lazima iifikie jamii hasa katika suala la elimu ya msingi hivyo tumeamua kuwapatia madawati haya baada ya maombi ya Mbunge wenu  Mahamudu Mgimwa kutuomba kumsaidia katika suala la madawati hivyo tuna kila sababu ya kuwasaidia watoto wetu ili wawe katika mazingira mazuri ya kupata elimu, ndiyo maana tumechukua jukumu hili," alisema Jumanne
Alisema kuwa tatizo la ukosefu wa madawati ni kubwa, hivyo kila mtu anapaswa kusaidia ili wanafunzi wapate elimu sahihi na yenye ubora na kuepukana na kukaa chini kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Aidha Jumanne alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kujiunga mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma wa PSPF kwa huduma bora na mafao bora yakiwemo mafao ya uzeeni,ulemavu,mirathi,mafao ya rambirambi za mazishi, malipo ya wategemezi na malipo ya penshini ya kila mwezi.
Alizitaja shule zilizonufaika na msaada huo kuwa ni shule ya msingi Mjimwema ilipata madawati (40), Mamba shule ya msingi (40) na shule ya msingi Kinyanambo (20) na kuongeza kuwa awamu ya kwanza walitoa madawati 250 kwa shule mbalimbali msingi katika jimbo la Mufindi Kaskani na kuzinufaisha shule zaidi ya 6.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mufindi Monica Kalalu alilishukuru shirika la PSPF kwa msaada huo na kutoa wito kwa wanafunzi na walimu kuyatunza madawati na kuwataka wadau wengine wajitokeze kuisaidia sekta ya elimu hususani elimu ya msingi kwa kuwa kwa upande wa sekondari tatizo la madawati limekwisha.

Wateja wa Airtel kununua Tiketi za Ndege za Precicsion Air kupitia huduma ya Airtel Money

Meneja Uendeshaji wa pitiaAirtel Money Asupya  Naligingwa (kushoto) akiongea wakati wa uzinduzii wa ushirikiano kati ya Airtel na Precision Airt utakaowawezesha wateja wa Airtel kulipia tiketi za ndege kupitita huduma ya Airtel Money. akishuhudia ni Afisa uhusiano wa Airtel bi Jane Matinde na na Afisa masoko wa Precision Air Hillary Mremi
 
Meneja Uendeshaji wa pitiaAirtel Money Asupya  Naligingwa (kushoto)  na Afisa masoko wa Precision Air Hillary Mremi (kulia) kwa pamoja wakizindua ushirikiano kati ya Airtel na Precision Air utakaowawezesha wateja wa Airtel kulipia tiketi za ndege kupitita huduma ya Airtel Money. akishuhudia ni Afisa uhusiano wa Airtel bi Jane Matinde
 
Wateja wa Airtel kununua Tiketi za Ndege za Precicsion Air kupitia huduma ya Airtel Money
·         Wateja wa Airtel wawezeshwa kulipia tiketi zao za ndege kwa njia rahisi na haraka zaidi
 Dar es Salaam Jumatano , Mai 7, 2014, kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeanzisha ushirikiano na Precision Airtel utakaowawezesha wateja wake nchi nzima kununua tiketi za ndege kupitia huduma ya Airtel Money
Ushirikiano huu utawapatia wateja wa Precision Air urahisi katika kupanga safari zao na kuwawezesha kununua ticket zao wakati wowote bila usumbufu kupitia huduma ya Airtel Money.

Akionge wakati wa uzinduzi Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde alisema ushirikiano huu utawapatia wateja wetu wa Airtel  njia mbadala, rahisi naya uhakika ya kulipia safari zao za ndani na za nje  huku ikiwapatia watanzania na wateja wetu uzoefu tofauti wa kufanya malipo ya tiketi zao za ndege kupitia simu zao za kiganjani. 

 Kwa   kupitia huduma hii mpya  sasa wateja wetu wataweza kufanya malipo ya tiketi zao za ndege mahali popote kwa usalama  na haraka zaidi  kupitia huduma ya Airtel Money. ”

“Tutaendelea kuthibitisha dhamira yetu ya kutoa bidhaa na huduma za kibunifu huku tukiwahakikishia wateja wetu huduma bora kupitia huduma ya Airtel Money na nyinginezo wakati wote”. Aliongeza Matinde
Akiongelea  kuhusu ushirikiano huo Afisa Masoko wa Precision Air Bwana Hillary Mremi alisema “  

ushirikiano huu umekuwa kwa wakati muafaka wakati Precision  Air imejipanga kuboresha  huduma zetu na kuwapatia wateja wetu uzoefu tofauti katika huduma za ndege  huku tukihakikisha wateja wanafurahia huduma zetu zinazoenda zaidi ya matarajio yao.

Wateja wetu sasa wanaweza kufanya malipo ya tiketi zao za ndege  kwa kupitia huduma ya Airtel Money . kupitia simu zao za mkononi wateja wetu wanaweza kupiga call center au kutembelea tovuti yetu kufanya booking ya safari zao na kulipia kupitia Airtel Money na kisha kupokea tiketi yako kupitia simu yako ya mkononi” aliongeza Mremi

Akiongea kuhusu namna ya kupata huduma hiyo Meneja uendeshaji wa Airtel Money  Asupya  Naligingwa alisema” huduma hii ni rahisi kutumia , mteja anachotakiwa kufanya ni kupiga simu na kufanya booking ya safari au kufanya booking kupitia tovuti ya Precision Air ambapo mteja atapewa namba ambayo itatumika kama reference wakati wa malipo.

Kununua tiketi kupitia Airtel Money wateja wanatakiwa kufanya yafuatayo
Piga  *150*60#
Chagua namba  5  (Lipia Bili)
Chagua namba 8 (NYINGINEZO)
Andika jina la biashara
PW
Ingiza Kiasi  cha pesa
Kumbukumbu rejea
(namba ya booking)
Ingiza neno la siri kulipa PW, Tsh xxxxx, kumbukumbu rejea namba xxxxxx
Baada ya kufanya  hayo utapokea ujumbe wenye uthibitisho wa malipo na tiketi yake ya ndege “aliongeza Nalingingwa
Huduma ya Airtel Money ni huduma inayowawezesha wateja wa Airtel Nchi nzima kufanya malipo na miamala ya pesa kupitia pesa simu ya mkononi . kwa kupitia huduma ya Airtel money wateja wanaweza kulipia ankra  kama vile DAWASCO, LUKU, USA visa, DSTV, kulipia mikopo , kununua muda wa maongezi, kununua vifurushi vya yatosha na kutuma na kupokea pesa kutoka kwa marafiki na familia na huduma nyingine nyingi.
Mwisho

                   HOT NEWSSSSSSSSSSS
MSIKILIZE  MUNGU YA EMMANUEL MGOGO VIDEO KUINGIA MTAANI SASA [SAYUNI BAND]
 mwimbaji wa nyimbo za injili wa nyanda za juu kusini mwa tanzania emmanuel mgogo ambaye amewahi kutamba na albamu ya iko wapi njia ile sasa amekamilisha albamu yake mpya inayokwenda kwa jina msikilize mungu ikiwa na nyimbo kama vile  msikilize mungu,  itakuwaje inatarajia kuingia mtaani kuanzia kesho tare 8 mwezi may 2014 akizungumza na mmiliki wa mtandao huu emanuel mgogo amesema anatarajia kazi hiyo kusambaa kwa kasi nchi nzima
hata hivyo alipoulizwa juu ya kuzindua albamu hiyo amesema anatarajia kuzindua katika mikoa ya nyanda za juu kusini pamoja na mkoa wa dare.salam.


                    emanueli mgogo akiwa katika moja ya huduma akimsimu mungu

PICHA KAMILI ZA TAMASHA LA PASAKA KUTOKA MWANZA, MALOPE AMALIZA

Malkia wa nyimbo za injili barani Afrika, Rebecca Malope.
Kwa wale ambao hawakufanikiwa kufika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye hitimisho la Pasaka, basi fursa ipo kupitia hapa kuona namna matukio yote yalivyokuwa, ambapo muimbaji mkongwe wa nyimbo za injili kutoka Afrika Kusini - tena malkia wa nyimbo za injili barani Afrika, Rebecca Malope alifanikiwa kugusa mioyo ya watu, si tu kwa uimbaji, bali hata kupitia kwa kuwatia moyo kwamba Mungu anasikia pale umuombapo.

Sehemu ya watu waliokuwa wakiingia uwanjani hapo.
Sehemu ya wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake.
Son of Tanzania, Ephraim Sekeleti kutoka Zambia
Katika tamasha hilo ambalo lilihudumiiuwa na waimbaji mbalimbali kutoka maeneo tofauti barani Afrika, lilikuwa na ugeni rasmi wa Mbunge wa jimbo la Sengerema, William Ngeleja, ambapo alisisitiza watu kuliombea taifa katika mchakato huu mgumu ambao unapitia wa kupata katiba. Na pia wakati hupohuo risala iliyosomwa kwa mgeni huyo rasmi na mojawapo wa waratibu wa tamasha hilo, Bwana John Melele, Mhe. Ngeleja ametakiwa kuwakumbusha wabunge wenzake kuwa pasipo Mungu hakuna kitakachowezekana, na hivyo wamtangulize.
BWANA asifiweeee, asema mgeni rasmi, mbunge wa jimbo la Sengerema, Mheshimiwa William Ngeleja.
Tukio la uzinduzi wa album ya muimbaji Grace pia lilifanyika ambapo mgeni rasmi alikiri wazi kuwa amani ya Tanzania pia inachangiwa na waimbaji wa nyimbo za injili, na hivyo wanatakiwa kusonga mbele bila kukata tamaa.

Wachungaji wakiwa wameiwekea mikono album ya mwanadada Grace Mwikabwe
Rebecca Malope na timu yake wakiingia ndani ya uwanja tayari kwa kuhudumu.
Akipokulewa na baadhi ya waimbaji wenzake.
Timu ikiwa 'standby'

Sasa tayari kwa kazi

BOMU LALIPUKA NDANI YA KANISA LA KILUTHERI MWANZA NA KUJERUHI

Mhudumu wa nyumba ya kupumzikia wageni wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria, jijijini Bernadetha Alfred (25) akiwa amelazwa katika Hospitali ya Bugando baada ya kulipukiwa na Bomu hilo jijini Mwanza.
Mhudumu wa nyumba ya kupumzikia wageni wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria, jijijini hapa, amejeruhiwa vibaya baada ya kulipukiwa na bomu lililokuwa limewekwa kwenye korido la nyumba hiyo.

Tukio hilo lilitokea siku moja baada ya tamasha la kimataifa la pasaka kufanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba (Jumatatu), kati ya saa 1:45 na saa 2:20 usiku, katika eneo la Makongoro
wilayani Ilemela wakati mhudumu huyo Bernadetha Alfred (25) alipofungua kifurushi cha mzigo alichodhani kimesahaulika kwenye eneo hilo, kabla ya kumlipukia.

Kwa mujibu wa Katibu wa Dayosisi hiyo, Mollel Rogart, kifurushi hicho kilichokuwa kwenye mfuko mweusi wa nailoni, kilikuwa juu ya kreti (tupu) za soda, karibu na eneo la kulia chakula lililopo katika nyumba hiyo.

“Ule mfuko ulikaa pale siku tatu ndiyo usiku huo mhudumu wetu akakichukua kukiangalia akidhani ni mzigo wa mtu umesahaulika.” Alieleza Katibu huyo na kudai kuwa kifurushi hicho kilimlipukia mara tu alipokifungua na kujeruhi vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili.

“Bernadetha kajeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo miguuni na usoni na siwezi kusema kwamba chanzo cha mlipuko huo ni mambo ya kidini japo ulinzi wetu haukuwa mkali kiasi cha kudhibiti watu walioingia na vitu.” Alisema

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Valentino Mlowola akithibitisha tukio hilo, alisema kwamba uchunguzi wa awali uliofanywa na kikosi maalum kutoka Dar es salaam umebaini kuwa bomu hilo limetengenezwa kienyeji.



“Bado tunaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili tubaini ni nani kafanya ili kama ni mtu au kikundi kimehusika tuchukue hatua haraka. Natoa wito kwa wananchi kutochukua vitu ambavyo hawa uhakika navyo, wanapoona vitu vya aina hiyo, watoe taarifa kwetu.” Alisema Kamanda Mulowola.

Mlowola alieleza kuwa, Bernadetha aliyejeruhiwa vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili, alikimbizwa katika Hospitali ya rufaa ya Bugando ambako anaendelea na matibabu.

Kamanda huyo alieleza kwamba, mabomu (yakiwemo ya kienyeji) yako katika mifumo mbalimbali hivyo wananchi hususan wahudumu wa sehemu za mikusanyiko wawe na tahadhari na vitu vinavyoonekana kusahaulika na wasisite kuwajulisha polisi vinapoonekana hivyo.

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog