Home » »

PSPF YAIPIGA JEKI SERIKALI YATOA MSAADA WA MADAWATI 100 KWA SHULE ZA MSINGI

Afisa Mfawidhi  Mfuko wa Pensheni kwa watumishi (PSPF)Mkoa wa Iringa, Baraka Jumanne akizungumza na waalimu wa Shule za Msingi tatu Mufindi Kaskazini(hawapo pichani)  kabla ya kukabidhi madawati 100 yaliyotolewa na mfuko huo.
Afisa Mfawidhi PSPF Iringa,Bakari Jumanne akimkabidhi Mkuu wa Wilaya Mufindi Evarista Kalalu Madawati miamoja kwa ajili ya Shule za Msingi Mjimwema, Mamba na Nyamalala yenye thamani ya sh. milioni 5 katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Mufindi.
 Baadhi ya madawati yakiwa ndani ya lori kabla ya kukabidhiwa kwa shule za msingi 3 za Mufindi Kaskazini.(picha zote na Denis Mlowe)

SHULE tatu za msingi za jimbo la Mufindi Kaskazini katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa zimenufaika kwa msaada wa madawati 100 yaliyotolewa na mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) yenye thamani ya shilingi milioni 5.
Akikabidhi msaada huo kwa mkuu wa wilaya ya Mufindi Monica Kalalu juzi katika ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo, Afisa Mfawidhi wa PSPF mkoa wa Iringa Baraka Jumanne alisema lengo la msaada huo ni sehemu ya mpango wao katika kusaidia sekta ya elimu nchini na kukuza elimu ya shule za msingi katika wilaya hiyo.
 "PSPF ni shirika la mfuko wa pensheni hivyo faida lazima iifikie jamii hasa katika suala la elimu ya msingi hivyo tumeamua kuwapatia madawati haya baada ya maombi ya Mbunge wenu  Mahamudu Mgimwa kutuomba kumsaidia katika suala la madawati hivyo tuna kila sababu ya kuwasaidia watoto wetu ili wawe katika mazingira mazuri ya kupata elimu, ndiyo maana tumechukua jukumu hili," alisema Jumanne
Alisema kuwa tatizo la ukosefu wa madawati ni kubwa, hivyo kila mtu anapaswa kusaidia ili wanafunzi wapate elimu sahihi na yenye ubora na kuepukana na kukaa chini kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Aidha Jumanne alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kujiunga mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma wa PSPF kwa huduma bora na mafao bora yakiwemo mafao ya uzeeni,ulemavu,mirathi,mafao ya rambirambi za mazishi, malipo ya wategemezi na malipo ya penshini ya kila mwezi.
Alizitaja shule zilizonufaika na msaada huo kuwa ni shule ya msingi Mjimwema ilipata madawati (40), Mamba shule ya msingi (40) na shule ya msingi Kinyanambo (20) na kuongeza kuwa awamu ya kwanza walitoa madawati 250 kwa shule mbalimbali msingi katika jimbo la Mufindi Kaskani na kuzinufaisha shule zaidi ya 6.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mufindi Monica Kalalu alilishukuru shirika la PSPF kwa msaada huo na kutoa wito kwa wanafunzi na walimu kuyatunza madawati na kuwataka wadau wengine wajitokeze kuisaidia sekta ya elimu hususani elimu ya msingi kwa kuwa kwa upande wa sekondari tatizo la madawati limekwisha.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog