APRIL 29 2015 MAGAZETI ya TANZANIA leo yameandika hizi kubwa >> Udaku,

.
DSC01924
DSC01925
DSC01926
DSC01927
DSC01929
DSC01930
DSC01931
DSC01932
DSC01933
DSC01934
DSC01935
DSC01936
DSC01937
DSC01938
DSC01939
DSC01940
DSC01941
DSC01942
DSC01943
DSC01944
DSC01945
DSC01946
DSC01947
DSC01948
DSC01949
DSC01950
DSC01951
DSC01952
DSC01953
DSC01954
DSC01955
DSC01956

MKE ACHINJWA KISA KWENDA SALUNI NA KUPENDEZESHWA, MAJIRANI WADAI ASINGEKUFA MKE ANGEKUFA MUME.. SIMULIZI YAO INASIKITISHA.

Enzi za uhai wake, Mary Lucas (20) anaedaiwa kuchinjwa na mumewe.


Tukio hilo lililoacha simulizi ya kushangaza miongoni mwa wanandoa na wanaotarajia kuingia, lilijiri Aprili 18, mwaka huu nyumbani kwa mwanaume huyo, Mtaa wa Mapinduzi ‘A’ Kata ya Duga jijini hapa.

WANACHOKIJUA POLISI WA TANGA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Zuberi Mwombeki alitangaza kwa waandishi wa habari kwamba, mauaji hayo yalitokea saa nne na nusu asubuhi ya Aprili 18 mwaka huu.

Alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kati ya wawili hao ambapo marehemu alimuomba mumewe pesa kiasi cha shilingi elfu kumi aende saluni kutengeneza nywele lakini mwanaume akasema hana.

“Mwanaume hakumpa pesa marehemu lakini baadaye alimkuta amesuka na ndipo ugomvi ulipoanzia hapo hadi kutokea mauaji hayo,” alieleza kamanda huyo.

UWAZI LAANZA NA MAJIRANI

Mengi yamesemwa kufuatia mauaji hayo, lakini kama kawaida ya Gazeti la Uwazi ni kufuatilia kwa kina ili kujua chanzo cha kila habari inayotakiwa kuandikwa gazetini.

Ili kujua nini kilitokea kabla na baada ya mauaji hayo, Uwazi lilizungumza na baadhi ya majirani wa nyumbani kwa mtuhumiwa huyo ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi chini ya ulinzi mkali.

“Jamani sisi wenyewe tumeshtuka sana kwa kifo cha Mary, mimi nimeongea naye akiwa anakwenda saluni na hata aliporudi. Kama angejua ndiyo siku yake ya kufa naamini asingekwenda. Inauma sana!

“Mary alitoka saluni akiwa amependeza maana alitengenezwa nywele vizuri sana. Mimi mwenyewe nilimsifia. Kufika nyumbani kwake, mzozo ukaanza.

“Mumewe alitaka kujua alikotoa shilingi elfu kumi ya kuendea saluni maana yeye hakumpa. Mzozo ulikwenda hadi mwanaume akachukua panga na kumchinja. Naamini ni wivu,” alisema jirani mmoja.

KUMBE WALIKUWA NA HISTORIA YA UGOMVI

Jirani mwingine, Shaban Juma yeye alisema: “Hawa watu wameishi katika hali ya kutoelewana na walikuwa wakigombana kila wakati, lakini hatukujua kama litatokea hili kwani mara zote katika kugombana kwao, mwanaume ndiye aliyekuwa akipigwa jambo ambalo liliwafanya watu wa karibu yake kumshauri kuvunja uhusiano wao kulikoni aibu ya kupigwa na mke.”

Jennifer Charles yeye pia ni jirani, alisema: “Siku ya tukio Mary alimwomba mumewe hela ya kwenda kutengeneza nywele saluni lakini mume hakuwa na pesa siku hiyo lakini baada ya kuondoka nyumbani, marehemu naye alikwenda saluni.

“Baadaye mume aliporudi nyumbani hakumkuta Mary lakini mara alirudi akiwa ametengenezwa nywele jambo lililomfanya bwana kuhisi kuwa fedha hizo amehongwa na mwanaume mwingine tofauti na yeye na hivyo kuzuka ugomvi huo.”

MUME ALITOKA NJE AKITAMBA KUUA

Baada ya Jennifer kumaliza kusimulia hayo, Juma Ally, naye ni jirani, akaendeleza: “Hatukujua kilichoendelea katika mzozo wao, lakini baadaye ukimya ulitawala. Muda mfupi mbele mume alitoka nje na kutuambia kwamba ameshaua huko ndani kwani amechoka kupigwa na sasa amejibu mapigo.

“Kwanza tulijua anatutania lakini tulivyoona kimya kimezidi tukaamua kuingia ndipo

tulipomkuta marehemu akiwa chini, akitoka damu nyingi. Tuliogopa kwa kweli. Mary mrembo tunayemjua sisi, amelala chini na damu chapachapa.

“Alikuwa ana majeraha makubwa sehemu ya shingo na kichwani yaliyotokana na kupigwa na panga. Ilionekana panga lilikuwa kali sana na panga lenyewe lilikuwa pembeni yake. Ndipo tulipoamua kumkimbiza Hospitali ya Mkoa, Bombo ambapo alipoteza maisha wakati madaktari wakihangaika kuokoa uhai wake.”

ASINGEKUFA MKE

Naye, Fatuma Ramadhani alisema kutokana na ugomvi wa mara kwa mara kati ya wawili hao na mwanaume kupigwa kila wakati, majirani waliamini siku moja mume huyo ndiye angekuja kupata madhara hata kufa kutokana na alivyokuwa akipigwa.

MTUHUMIWA KUPANDA MAHAKAMANI WAKATI WOWOTE

Kamanda Mwombeki alisema upelelezi unaendelea ili kuweza kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo.

Marehemu Mary alizikwa katika eneo la Mwakizaro jijini Tanga, siku ya pili baada ya tukio hilo la kuhuzunisha.

RAIS KIKWETE AZINDUA MELI MBILI ZA KIVITA ZA KIKOSI CHA WANAMAJI CHA JWTZ JIJINI DAR ES SALAAM LEO‏.

Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua rasmi meli mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015.


Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mara baada ya kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015



Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya kumbukumbu na makamanda wa meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015


Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Chifu Edward Wanzagi wa kabila la Wazanaki (kati) pamoja na Mbunge wa Afrika Mashariki Mhe Makongoro Nyerere baada ya kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015.

Watanzania 26 Waliokuwa Afrika Kusini Warejea Nyumbani.......20 Wengine Kuhakikiwa na Kurejeshwa


Kundi la Watanzania 25 limerejea nyumbani kutoka Afrika Kusini jana tarehe 26 Aprili, 2015 kufuatia mashambulizi ya wazawa dhidi ya wageni. Kundi hilo la kwanza kurejea nyumbani liliwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere saa 11 alfajiri na Ndege ya Fast Jet.

Watanzania hao walikuwa wanaishi katika kambi za dharura za Isipingo na Phoenix zilizopo jijini Durban. Walisindikizwa kurudi nyumbani na Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Bw. Elibahati Lowassa. Zoezi la kuwarejesha wananchi hao lilisimamiwa na kuratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini.

Wakati huo huo, Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini umepata taarifa kuwa kuna Watanzania wengine wapatao 20 wanaishi kwenye Kambi ya Hillbrough jijini Johannesburg.
 
Ubalozi umetuma Afisa kwenda katika kambi hiyo ili kufanya uhakiki wa taarifa hizo kwa madhumuni ya kuwarejesha nyumbani Tanzania haraka iwezekanavyo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
25 Aprili 2015

Zaidi ya Watu 900 Wadaiwa Kupoteza Maisha kwa Tetemeko la Ardhi Nchini Nepal

TETEMEKO la ardhi limetokea nchini Nepal jana  na na kupoteza maisha ya watu  ya 900 na kuangusha Mnara wa Karne ya 19 Mjini, Kathmandu pamoja na kusababisha maporomoko ya theluji kutoka katika milima. 

Taarifa zinadai kuna uharibifu katika maeneo ya nje ya kitovu cha tetemeko hilo lenye ukubwa wa kipimo cha richter cha 7.9 maili 50 kutoka Pokhara mji wa pili kwa ukubwa nchini Nepal. 

Tetetemeko hilo la ardhi ni kubwa kabisa kuwahi kuikumba nchi hiyo katika kipindi cha miaka 81 na pia limesababisha athari katika majimbo ya nchi jirani kaskazini mwa India na Bangladesh. 

Kunauwezekano vifo hivyo vinaweza kuongezeka katika Bonde la Kathmandu ambalo lina watu milioni 2.5.

Naibu balozi wa Nepal mjini New Delhi Prasad Pandey amesema inahofiwa kuwa mamia ya watu wamekufa na kuna ripoti ya kuwepo kwa uharibifu mkubwa kila sehemu kubwa na kwamba sio tu katika baadhi ya maeneo ya Nepal bali ni nchi nzima imeathirika. 

Nepal ilikumbwa na tetemeko kubwa la ardhi kuwahi kurekodiwa nchini humo hapo mwaka 1934 likiwa na kipimo cha 8.0 ambapo watu 8,500 walipoteza maisha yao.
Baadhi ya Waokoaji wakiwa wamsaidia mmoja wa waathirika wa Tetemoko hilo aliekuwa amefukiwa kwenye kifusi ya moja ya majembo yaliyoporokoma kutokana na tetemeoko hilo.
Sehemu ya athari za tetemeko hilo.
Jitihada za kuokoa waliofunikwa na kifusi zikiendelea.
Wananchi wa Nepal wakishirikiana kwa pamoja kuvuta kamba. 

Ramani inayoonyesha sehemu iliyokumbwa na tetemeko hilo.
 

Muuguzi amchapa mjamzito viboko......Ni wakati wa uchungu wa kujifungua, Mtoto afia tumboni.


Muuguzi mmoja wa zahanati ya Muungano, Chamwino, mkoani Dodoma, amekumbwa na kashfa nzito baada ya kudaiwa kumchapa viboko mama mjamzito, wakati akiwa katika hali ya uchungu wa kujifungua na kusababisha mtoto aliyetaka kujifungua kufariki akiwa tumboni.

Aidha, mama huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, hali yake inaelezwa kuwa mbaya.

Mwanamke huyo, Mariamu Maroda, anadaiwa kulazwa kwenye chumba hicho kwa zaidi ya wiki moja, ambapo pamoja na kufanyiwa upasuaji, hakufanikiwa kupata mtoto wake akiwa hai.

Akisimulia mkasa huo, mama mdogo wa Maroda, Joyce Charles, alisema Aprili 3, mwaka huu Saa 12:00 jioni, walimpeleka zahanati ya Muungano akiwa na dalili za kujifungua na kupokelewa na muuguzi aliyemfahamu kwa jina la Lucy. 
 
“Nilishuhudia Lucy akimchapa Maroda viboko kwenye mapaja na mgongoni, akisema ana uwezo wa kujifungua lakini anadeka tu, nilishindwa kuingilia nikihofia asimdhuru zaidi mwanangu, ila nilihuzunika sana,” alisema.

Alisema muuguzi huyo alitumia fimbo tatu kumchapa mgonjwa wake, ambazo alikuwa akizitumia kila moja inapovunjika. Alisema fimbo hizo zilipomalizika, alianza kumfinya kwenye mapaja kwa kutumia rula.

“Kesho yake saa 12:00 alfajiri, huku hali ya mgonjwa ikiwa mbaya, walitupatia gari likatupeleka hospitali ya Mvumi Misheni, ambako walisema hali aliyokuwa nayo mgonjwa wasingeiweza na kutuelekeza tumpeleke hospitali ya rufaa, lakini walimpa mgonjwa chupa mbili za damu,” alisema.

Alisema Maroda alifikishiwa chumba cha upasuaji na kisha alilazwa wodi namba 17, lakini miguu na tumbo vilianza kuvimba na alipochunguzwa ikabainika ana usaha tumboni, hivyo aliamriwa arudishwe kwenye chumba cha upasuaji.
 
 “Yaani ukimuona, mwilini ana alama za fimbo na kufinywa. Sasa walipomfanyia upasuaji kwa awamu ya pili, alipelekwa ICU mpaka hivi tunavyozungumza ni zaidi ya wiki moja,” alieleza Charles.

Viongozi wa Hospitali ya Rufaa, wenye mamlaka ya kuzungumzia suala hilo walionekana ‘kurushiana mpira’ walipotakiwa kuelezea suala hilo. Hata hivyo, Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anatoria Mkindo, alikiri kuwepo kwa mgonjwa huyo.

Awali Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Zainab Chaula, alisema hakuwa na taarifa za kina kuhusu Maroda.
 
Mkindo alisema walikuwa wameagiza Ofisi ya Mganga wa Wilaya wa Chamwino, kuwapelekea taarifa kuhusu suala hilo.

Alisema pia wametaka Ofisi ya Mganga Mkuu wa mkoa, ifahamishwe hatua zilizochukuliwa dhidi ya mtumishi aliyedaiwa kumchapa viboko mjamzito huyo.

“Mimi sio msemaji, anayetakiwa kuwapa taarifa kamili ni RMO (Chaula) kwanini awalete kwangu, nilichowaeleza ni ambacho nafahamu lakini siyo msemaji, nashauri muende ofisini kwa matroni wa hospitali mtapata taarifa kamili,” alisema.

Afisa Muuguzi wa ICU, Christina Mlumba, alisema, Maroda alipelekwa ICU baada ya kufanyiwa upasuaji na kwamba hali yake inaendelea vizuri.

Mdogo wa Maroda, Silika Mkwawi alivieleza vyombo vya habari kuwa ingawa hakuingia kwenye chumba cha kujifungulia katika zahanati ya muungano, dada yake alipotolewa nje, muuguzi alimueleza kuwa alimchapa fimbo mbili tu, kwa sababu ya kudeka kwake.
KUTANA MWANAMKE PEKEE AMBAYE ANAENDESHA CHOMBO CHA KUTENGENEZEA BARABARA YA LAMI YA DODOMA IRINGA HAPA.

                        hili ndo preva linaloendeshwa na mwanadada huyu 





                            hapa akiafanyiwa mahojiano na mmiliki wa blog hii

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog