Home » »

Lowassa Avunja Rekodi Mkoani Shinyanga.......Wananchi Waumizana Wakigombea Kumuona, Avuna Wadhamini 7,114


Mh. Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wana CCM waliomdhamini mkoani Shinyanga, kutoka kwa katibu wa CCM wilaya ya Shin yanga mjini Charles Sangula, Juni 11, 2015.
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, akipungia mkono wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Shinyanga, alipokuwa akiondoka ofisi za chama hicho wilaya ya Shinyanga mjini mara baada ya kupata wana CCM wa kumdhamini .
 
Mh. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, jana  amevunja rekodi ya kupata wadhamini 7,114, idadi  ambayo  ni kubwa kuliko  mgombea  mwingine  yeyete  ndani  ya  CCM hadi sasa. 

Furaha ya kumuona Mh. Lowassa, ilitawala ukumbi mzima
Wana CCM waliofika kumdhamini Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, wakishangilia wakati akiingia ukumbi wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015.
Wananchi wa mkoa wa Shinyanga, wakisukumana ili wapate kumuona Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, alipokuwa akiwasili kwenye ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015, ili kuomba wanachama wenzake wa chama hicho wamdhamini.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog