Home » »

Maelfu ya wananchi kumsindikiza Lowassa kuchukua fomu ya Urais


Waziri Mkuu Wa zamani Edward Lowassa  anatarajia kwenda makao makuu ya chama cha Mapinduzi maarufu kama White House mkoani Dodoma  june 3 akisindikizwa na maelfu ya wananchi.

Kwa  mujibu wa  Mnyetishaji  wetu  aliyezungumza  na mtandao  huu,  amearifu  kuwa wakazi wa Manispaa ya Dodoma watakwenda  kumpokea  Mbunge wa   Monduli   Edward   katika   wilaya  ya Manyoni   akitokea  mkoani  Arusha  kwenda mkoani Dodoma kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa tiketi ya chama  cha Mapinduzi (CCM).

Aidha, wagombea wote  wanaotaka kuwania urais kupitia chama cha Mapinduzi wanatakiwa kuchukua  fomu  ifikapo tarehe  3/6/2015  na  kurudisha  2/7/2015. Kutafuta  wadhamini  mikoani ni 3/6/2015 hadi 2/7/2015.

Kamati  ya usalama na maadili itakutana 8/7/2015 ikifuatiwa na kamati ya Halmashauri kuu ya Taifa 9/7/2015. Uteuzi  wa  wagombea  urais  utafanyika  Zanzibar tarehe  10/7/2015  ukifuatiwa na mkutano mkuu Taifa wa  tarehe 11-12/7/2015.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog