Home » »

Itazame familia hii iliyotembelewa na Mbunge wa Vitimaalum Ritta Kabati wote wakiwa walemavu.



 WANANCHI NA VIONGOZI WAMPONGEZA MBUNGE WA VITIMAALUM KWA JUHUDI ZAKE KATIKA KUPIGANIA MAENDELEO IRINGA.
Mbunge wa Vitimaalum mkoani Iringa Ritta Kabati alipotembelea familia ya watu watano wote wakiwa walemavu na wanaishi mazingira magumu Wilayani kilolo ambapo aahidi kuwajengea Nyumba ya Kisasa.
 

Zikiwa zimebaki siku kadhaa kumalizika kwa kipindi cha Uongozi wa wabunge hapa nchini hususani wabunge wa Viti maalumu ambao wanatarajia kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo wananchi na viongozi mkoani Iringa wampongeza Mbunge wa Viti maalumu Ritta Kabati.

Wakizungumza na Morning star redio kwa nyakati tofauti wananchi hao wamempongeza Mh.Kabati kwa mchango wake kwa jamii ya mkoa wa Iringa na kuonyesha moyo wa upendo na kuthamini ubora wa maisha ya wanairinga wote bila kujali itikadi ya dini,siasa wa rangi ambapo amekuwa akipigania maendeleo ya watu wa rika zote.

Wananchi hao wamemtaja Mbunge Kabati kuwa ndiye kiongozi wa kuigwa na viongozi wengine kwa kuwa amekuwa amefanikiwa kusemea vema mkoa wa Iringa na kutoa kero za wananchi bungeni bila woga na kuifanya serikali kutekeleza kwa kuzingatia mchango wake.

Wakizitaja baadhi ya kazi alizozifanya Mh.Kabati  kuwa na pamoja na kulipigania suala la haki sawa baina ya mwanamke na mwanaume,suala la kuwapa elimu watoto wa kike ukizingatia katika ofisi ya mbunge huyo imekuwa ikisaidi watoto wasiojiweza waliohitimu kidato cha nne kwa kuwatafutia vyuo mbalimbali jambo ambalo limewafanya zaidi ya watoto elfu 15 kuendelea na masomo.

Aidha wamesema amekuwa akipigania suala la miundombinu pamoja na afya ambapo kupitia jitihada zake zimesaidia kuboresha wodi za wazazi katika Hospital ya wilaya ya Iringa sambamba na hilo amejenga kituo cha polisi kwa ghalama ya Sh mil 45 kilichopo Semtema manispaa ya Iringa.

Kwa upande wa viongozi akiwemo Meya wa Halmashauri ya Iringa Amani Mwamwindi,Katibu wa CCM mkoa Hasani mtenga na mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake mkoani Iringa Wamempongeza kwa jitihada za kuwezesha eneo la kihesa kilolo kuwa eneo la uendelezaji kwa makazi badala ya kuwa eneo la hifadhi.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog