BAADA YA PADRI KUNASWA LAIVU KICHAKANI NA MREMBO, WAUMINI WATAKA MAPADRI WARUHUSIWE KUONA KWANI WAAIBISHA KANISA
Mpasuko! Kufuatia
kuibuka wimbi la kashfa za ngono zinazowagusa waseja wa daraja la upadri
duniani, baadhi ya waumini wa madhehebu mbalimbali yakiwemo Katoliki na
Anglikana, wameibuka na kudai kuwepo kwa marekebisho ya sheria ya
makanisa hayo yanayoruhusu watumishi hao kuoa kwani kwa sasa
wanayaaibisha, jambo ambalo linaharibu imani juu ya Ukristo.
NINI KIMETOKEA?
Hayo yanakuja kufuatia
tukio la hivi karibuni la kunaswa kwa Padri Anatoly Salawa ambaye ana
cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu
wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference, Tec)
aliyekutwa na mrembo vichakani.
Father Salawa alinaswa na mrembo huyo vichakani ndani ya gari maeneo ya Kurasini jijini Dar.
Mbali na tukio hilo, pia
yapo matukio mengine ya mafumanizi likiwemo lile la Father Urbanus
Ngowi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi aliyefumaniwa ‘laivu’ na mke wa
mtu aliyetajwa kwa jina la mama P.
Katika tukio hilo la
mwaka 2013 lililoripotiwa na gazeti ndugu la hili, Ijumaa Wikienda,
Father Ngowi alikutwa na mwanamke huyo ambaye alikuwa muumini wake,
chumbani kwake maeneo ya Marangu Wilaya ya Moshi Vijijini.
Padri Anatoly Salawa aliyenaswa na binti kichakani.
WAUMINI WAFUNGUKA
Wakizungumza kwa nyakati
tofauti na gazeti hili, mwanzoni mwa wiki hii, waumini hao walitolea
mifano ya baadhi ya viongozi wa madhehebu hayo kunaswa katika skendo za
uhusiano wa kimapenziu hivyo kuona ni bora wakaruhusiwa kuoa ili
kuliondolea aibu kanisa.
“Ni bora kama ni sheria
irekebishwe ili hawa mapadri waruhusiwe kuoa kwani sasa hii ni aibu kwa
kanisa, kuliko kuendelea kuchafua taswira ya misingi ya dini ambayo
imekuwepo tangu enzi na enzi.
“Mbona mapadri wengine
wa Ulaya Mashariki wa madhehebu ya Katoliki (Ukranian Greek Catholic
Church na Coptic Catholic Church) wanaoa? Kwa nini na wa kwetu wasioe?”
alihoji mmoja wa waumini hao katika mahojiano na mwandishi wetu ndani ya
ofisi za gazeti hili, Bamaga-Mwenge jijini Dar.
BARUA YA WAZI KWA PAPA
Mbali na waumini wa hapa
nchini, mapema mwaka jana, wanawake wapatao 26 waishio nchini Italia,
walimwandikia barua ya wazi Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Katoliki Duniani,
Papa Francis wakimueleza mateso wanayopata kwa kuwa na uhusiano wa siri
wa kimapenzi na baadhi ya mapadri wa kanisa hilo.
Mkuu wa Kanisa la Katoliki Duniani, Papa Francis.
PAPA ANENA
Akifafanua sakata hilo
katika mahojiano maalum na Jarida la Republica la jijini Vatikani, Papa
Francis alikiri kuwepo kwa taarifa za mapadri kuwa na uhusiano wa
kimapenzi, kauli ambayo ilipingwa vikali na msemaji wa kanisa hilo,
Federico Lombardi kwa madai kuwa mwandishi wa jarida hilo alimnukuu papa
vibaya.
Mbali na hayo, padri
mmoja aishiye Italia kutoka Kanisa la Kigiriki la Byzantine lililo chini
ya Mamlaka ya Vatican, Jani Pecoraro alisema ifike wakati sasa nyakati
zitambuliwe kwani kuoa kwa mapadri hakuondoi weledi wa huduma zao.
“Tunapaswa kusoma
nyakati na hakuna shaka kwamba jamii ya sasa imekuwa ikiibua hoja kuwa
mapadri waliooa wanaweza kuwa na kiwango sawa cha utumishi na wengine,”
alikaririwa padri huyo.
PAPA AWA MAKINI
Hata hivyo, Papa Francis
amekuwa makini na jambo hilo huku akieleza kuwa zuio la mapadri kuoa
liliasisiwa karne 10, ikiwa ni karne tisa nyuma kabla ya kifo cha Yesu
Kristo huku kukiibuka sintofahamu juu ya uamuzi wa papa juu ya mapadri
wanaokiuka misingi hiyo.
PIGO KWA KANISA
Mbali na waamini
wanaotaka mapadri kuruhusiwa kuoa, wapo wanaoliona jambo hilo kuwa ni
pigo jipya kwa kanisa kwani wanatamani mapadri kuendelea kuwa waseja.
Father Urbanus Ngowi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi.
Kuhusiana na sakata
hilo, gazeti hili lilikwenda Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la
Dar es Salaam na kukutana na Katibu wa Mwadhama Polycarp Kadinali
Pengo, Denis Aminias na kuzungumza naye ambapo alisema:
“Sisi kama kanisa tutaendelea kusimamia katika misingi ileile ya mapadri kutooa.”
0 comments:
Post a Comment