WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM KUKUTANA IJUMAA HII

Wakazi wa jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake ijumaa hii wanatarajiwa kujumuika pamoja katika mkesha mkubwa wa maombi na maombezi unaotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa BCIC Mbezi beach uliochini ya Wapo Mission International na kiongozi wake askofu Sylvester Gamanywa.

Mkesha huo ambao unatarajiwa kuwa na vipindi mbalimbali vya kusifu na kuabudu pamoja na neno la Mungu pamoja na maombi umekuwa ukivutia maelfu ya wakazi wa jiji hilo kutokana na kile ambacho Mungu amekuwa akitenda kupitia watu wake.Ambapo maombi maalumu yatafanyika kwa watu wote hususani wanafunzi ambao wamekuwa na matokeo mabaya katika mitihani yao pamoja na kufeli katika mambo mbalimbali, watu wanaoteswa na vifungo mbalimbali vya shetani, yakiwemo majini na mambo mengi yafananayo na hayo.

Kati ya waimbaji watakaokuwepo ijumaa hii kwenye mkesha huo ni pamoja Emanuel Mgogo kutoka Mbeya, Masanja Mkandamizaji, Kikundi cha kusifu na kuabudu cha Mbezi beach BCIC na waimbaji wengineo, mkesha huo utaanza majira ya saa 3 usiku na kuendelea huku kituo cha Wapo Radio Fm kikirusha live mkesha huo.
Rais wa Wapo Mission International, askofu Sylvester Gamanywa akiwa katika moja ya ibada kituo cha Mbezi beach kutakofanyika mkesha huo.

mwimbaji wa mahiri wa nyimbo za injili NESTER SANGA KUZINDUA ALBAM YAKE MPYA IITWAYO TWENDENI.

Mwimbaji Mahiri wa nyimbo za injili Tanzania kutoka Dar el Salaam Nester Sanga ameweka wazi malengo ya uzinduzi wa albam yake mpya jijini Mwanza iitwayo Twendeni ambayo ina takribani nyimbo tisa na imetoka mwezi huu wa nane.

Akiongea na mwandishi wa habari hizi bi. Sanga amesema kuwa amefikia uamuzi huu baada ya kupata simu nyingi kutoka Mwanza watu wakimuomba aje afanye tamasha la uzinduzi wa albam yake mpya iitwayo Twendeni.


Akizungumzia ubora wa albam hii ya Twendeni bi. Sanga amesema ni moja kati ya albam ambayo imetokea kupendwa wa watu wa dini na rika zote na kutibithisha kuwa itafanya vizuri kuliko albam yake ya kwanza iliyojulikana ka Jiandaeni.


Uzinduzi wa albam ya Twendeni yake Nester Sanga unatarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi wa kumi katika uwanja wa furahisha Mwanza.

Hii ni albam ya pili yake Mtumishi Nester Sanga ambayo ameitoa baada ya kufanya vizuri na albamu yake ya kwanza iliyojulikana kama Jiandaeni.


Nester Sanga ameanza kuimba siku nyingi baada ya kugundua kuwa ana wito na kipaji hivyo anahitaji sapoti ya watanzania ili waeze kufikia malengo ambayo Mungu ameyaweka mbele yake. Watanzania Tumuunge mkono.


Nester Sanga akiongea na mtandao huu kuelezea kusudi la uzinduzi wa albam yake mpya.


MAMBO YAZIDI KUNYOOKA KWA WAIMBAJI WA GOSPEL NCHINI

Mwimbaji nyota wa muziki wa gospel nchini ambaye mashabiki wameamua kumpachika jina la malkia wa muziki wa gospel nchini bibie Rose Muhando kwasasa yuko busy nchini Afrika ya kusini akirekodi video ya album yake mpya ambayo hata hivyo jina bado halijatajwa ingawa GK inahisi album hiyo itaitwa Haleluya Hossana.

Akiwa chini ya kampuni maarufu ya muziki duniani ya Sony Music kwa barani Afrika ikiwa imejikita nchini Afrika ya kusini, tayari mwimbaji huyo alishakamilisha album ya sauti wiki mbili zilizopita na kwasasa tayari ameanza kurekodi nyimbo zilizobaki katika video yake hiyo ambayo inategemewa kuleta kitu cha tofauti kuanzia usikivu wa kanda bya sauti mpaka video kutokana na ubora wa kampuni hiyo ya Sony.

Rose Muhando katika pozi la picha.
Wakati huohuo mwimbaji mwingine wa muziki wa gospel nchini Upendo Nkone ambaye ameachia album yake ya nne hivi majuzi, jumamosi hii anatarajiwa kuwa mmoja kati ya waimbaji watakaomsifu Mungu katika tamasha kubwa la kimataifa  liitwalo ''International Gospel Music Festival'' litakalofanyika huko Columbus Ohio nchini Marekani likiwa limeandaliwa na Pastor Donis na mkewe Nnunu Nkone.

Hii itakuwa mara ya pili kwa Upendo kuingia nchini Marekani kwa ajili ya huduma ya kumtangaza Kristo ikitanguliwa na safari ya kwanza aliyokuwa ameambatana na waimbaji wenzake Upendo Kilahiro pamoja na Christina Shusho mwishoni mwa mwaka jana, ambapo tayari mwimbaji huyo ameshawasili nchini Marekani na kulakiwa na wenyeji wake.
Upendo Nkone akipokewa uwanjani mara baada ya kuwasili nchini Marekani.

VIONGOZI WA DINI CHANZO CHA MIGOGORO--JAJI MKUU MSTAAFU

Jaji mkuu mstaafu wa Tanzania akizungumza.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustino Ramadhani, amewataka viongozi wa dini kuacha kuwa chanzo cha migogoro makanisani na badala yake kurudi zaidi kwa Bwana Yesu ili kuweza kutimiliza kusudi walilopewa katika utumishi wao.

Rai hiyo aliitoa juzi siku ya Jumapili katika sherehe za uzinduzi wa miaka hamsini ya Umoja wa Kujisomea Biblia (Scripture Union) zilizofanyika katika ofisi za makao makuu ya shirika hilo maeneo ya Muhimbili wakati alipohudhulia kama mgeni rasmi wa tukio hilo.
Alisema tatizo kubwa lilipo makanisani kwa hivi sasa linasababishwa na viongozi wenyewe ambao badala ya kumtumikia Mungu wamegeuka na kuangalia vyeo hivyo basi ni vyema kurudi kwa Bwana ili waweze kumtumikia.

Migogoro mingi iliyopo makanisani hivi sasa matatizo makubwa yako kwenye uongozi wala sio wanaoongozwa cha muhimu tu ni kwamba viongozi warudi zaidi kwa Bwana wanayemtumikia” alisema Jaji Augustino Ramadhani.

Sherehe hizo zilihudhuliwa na watu mbalimbali wakiwemo Jaji Angera Kileo, Askofu Philemon Tibanenason, Mweka Hazina wa Chuo Kikuu cha Mlimani, Donata Mugassa pamoja na viongozi wa shirika hilo, Mwenyekiti Dk. Edda Mwandi aliyekuwa mwenyeji wa sherehe hizo pamoja na Katibu Rev. Emaus Bandikile.

MJI MPYA WA WILAYA YA KILOLO HUENDA SASA UKAWA MOJA KATI YA MIJI BORA MKOA WA IRINGA KUTOKANA NA MAJENGO YANAYOENDEREA KUJENGWA

HII NI MOJA KATI YA GUEST NA LORGE MAALUFU UKIFIKA KATIKA WILAYA MPYA YA KILOLO KATIKA MKOA WA IRINGAA



AFISA MTENDAJI WA KIJIJI CHA LUGANGA WILAYA YA KILOLO BWANA THABIT JUMA KALOLO AKIFAFANUA JUU YA UELEWA WA WANAICHI KUHUSU KATIBA MPYA

HII NDO KATIBA YENYEWE

mtangaji wa overcomers na mmiliki wa mtandao huu akifanya mahiojiano na baadhi ya wanaichi

MIRIAM LUKINDO, CHRISTINA SHUSHO KUPAMBA UZINDUZI WA ALBUM YA KWAYA

Miriam Lukindo wa Mauki akimsifu Mungu.
Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Miriam Lukindo Mauki ‘Binti Afrika’ Jumamosi hii anatarajiwa kuiteka Matembele ya Pili, Ukonga jijini Dar es Salaam atakaposhiriki uzinduzi wa albamu mbili za kwaya ya Sauti za Sifa iliyo chini ya Huduma ya The Word of Reconciliation Ministries (WRM).

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwalimu wa kwaya hiyo, Elibariki Isango, alisema, Miriam amekubali kuungana nao na siku hiyo atapanda jukwaa moja na Christina Shusho kuimba, wakati wa uzinduzi wa albamu zao hizo ambazo ni ‘Enendeni kwa Roho’ na ‘Pokea Sifa’.
Miriam amekubali kuja kutuunga mkono katika shughuli yetu ya kuzindua albamu zetu mbili na ataungana na Shusho kuimba nyimbo zao mbalimbali, hivyo naomba wakazi wote wa Dar es Salaam na vitongoji vyake, kufika kwa wingi kwenye uzinduzi huo,” alisema Isango.
Christina Shusho.
                        
Mwalimu Isango alisema kuwa, lengo la uzinduzi wa albamu hizo ni kukusanya fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa jengo la huduma hiyo, ambalo kwa sasa lipo katika hatua za mwisho, hivyo kila atakayefika katika uzinduzi huo na kununua CD zao, atakuwa ametoa sadaka yake ya kukamilisha hekalu la Bwana.

Waimbaji wengine watakaoimba kwenye uzinduzi huo ni Ami Mwakitalu, Madame Luti & Chris, Faraja Moleli, Queen Talaba, Wilson John, Magreth na wengine wengi, ambako shughuli itaanza majira ya saa 6:00 mchana na kumalizika saa 12 jioni.

Mwalimu Isango aliongeza kuwa, hakutakuwa na kiingilio katika uzinduzi huo, hivyo wadau wa muziki wa injili, hasa wanaoishi maeneo ya Kitunda, Ukonga na Gongo la Mboto kufika kwa wingi, kwani hiyo ni mara ya kwanza kwa waimbaji kama Shusho na Miriam kuimba eneo hilo.

KAMBI NA TAMASHA LA WAIMBAJI WA MKOA WA KIGOMA LAFANA

Wiki iliyoisha kuanzia tarehe 15 hadi 19 kumefanyika kambi pamoja na tamasha kubwa la waimbaji wote wa mkoa wa Kigoma(Leka Dutigite), tukio hilo ambalo limefanyika kwa mara ya kwanza na kwa mafanikio makubwa liliandaliwa na kwaya ya KYGC ya kanisa la Free Pentecostal Church Tanzania (FPCT).
Ambapo kambi imefanyika katika viwanja vya kanisa la FPCT Mwanga na kuhitimishwa kwa tamasha kubwa katika uwanja wa Lake Tanganyika likisindikizwa na waimbaji waliopo mkoani hapo na wale waishio nje ya mkoa huo kama Victor Aron, Upendo Nkone, Amon na mkewe Upendo Kilahiro, Mery Nkwabi na kwaya ya Dar es salaam Gospel Choir(DGC) kutoka FPCT Kurasini.

Kwa upande wa walimu waliohudhuria na kufundisha katika semina hiyo ni pamoja na George Mwita, Sossy Mabele, Joseph Malumbu pamoja na mwenyeji wao Wilson Gwimo, huku wahudhuriaji walilipa ada ya ushiriki katika kambi na tamasha hilo.
                                       ANGALIA BAADHI YA PICHA ZA TUKIO HILO.
Asubuhi watumishi wakipata kifungua kinywa kabla ya kutumika.
DGC wakimsifu Mungu kanisani Mwanga.
Amon Kilahiro wa kwanza kuume akiwa na watumishi wenzake.
Kwaya wenyeji waandaaji wa kambi na tamasha hilo KYGC wakimsifu Mungu.
Mmoja wa masolo matata wa DGC aitwaye Rose wa kwanza kuume akiwa na wenzake wakifuatilia kilichokuwa kikijiri madhabahuni.
Upendo Kilahiro akiwaongoza wenzake na Zindonga ziwelale.
DGC wakimsifu Mungu uwanja wa Lake Tanganyika katika tamasha.
Furaha ndani ya Yesu, DGC wakimsifu Mungu katika uwanja wa kanisa FPCT Mwanga.
Kiongozi wa kwaya ya DGC akipokea cheti cha ushiriki wa kwaya katika kambi na tamasha hilo.
DGC wakipanda gari kurudi kambini kujiandaa na safari ya kurejea jijini DSM.
DGC wakitoka uwanja wa Lake Tanganyika. Picha kwa hisani ya Eliud Mathias.

ROSE MUHANDO AKAMILISHA ALBUM MPYA CHINI YA SONY MUSIC AFRIKA YA KUSINI

Malkia wa muziki wa gospel nchini bibie Rose Muhando hatimaye amemaliza kurekodi album yake mpya ya sauti pamoja na kurekodi nyimbo mbili kwenye video huko nchini Afrika ya kusini chini ya kampuni ya Sony Music Entertainment ya Afrika ya kusini.

Kwa mujibu wa taarifa alizotoa mwimbaji huyo hii leo amesema amekamilisha nyimbo tatu zilizokuwa zimebakia katika kukamilisha album hiyo ya sauti ambayo hata hivyo hajaitaja jina. Mwimbaji huyo ambaye aliingia mkataba na kampuni hiyo ya kimataifa mapema mwaka jana, tayari amepata mafanikio makubwa kwenye medani ya muziki wa injili nchini tokea atoe album yake ya kwanza ya ''Mteule uwe Macho'' hadi yasasa ya ''Utamu wa Yesu''.

Hapana shaka kwamba album mpya itakuwa na kiwango kikubwa zaidi cha usikivu si kwenye sauti tu pia muziki wake utakuwa umerekodiwa kwenye viwango vikubwa kitu ambacho kitalifanya jina la Kristo lizidi kutangazwa si Tanzania tu bali maeneo mbalimbali duniani. Kila la kheri Rose Muhando.

Rose Muhando

WAPENZI WA MUZIKI WA GOSPEL JIJINI NAIROBI KUKUTANISHWA NA PAUL MWAI

Paul Mwai mwandaaji wa tamasha hilo.                   
Wapenzi wa muziki wa gospel jijini Nairobi nchini Kenya wanatarajiwa kukutanishwa pamoja siku ya tarehe 2 mwezi ujao katika uwanja wa mpira wa Thika kwenye tamasha kubwa la muziki wa injili lililoandaliwa na mwimbaji aliyejipatia umaarufu siku za karibuni Paul Mwai ambaye ameamua kulipa jina  tamasha hilo kama  Groove awards skiza tune of the year celebration.

Mwimbaji huyo ambaye amefahamika zaidi nchini kwa album yake ya Racing Up amewaalika waimbaji mbalimbali kutoka nchini humo akiwemo Emmy Kosgei, Mbuvi, Pastor Ruth Wamuyu, Ben Githae, Loise Kim, Carol Wanjiru, Charles Kingori, James Warachi, Muigai Wanjoroge na waimbaji wengine wengi huku waendesha tamasha hilo ama MC bwana Mwai amewataja kuwa ni Muthee Kiengei akisaidiwa Olo Matope wa Coro Fm.

Tanzania imekuwa ikisifika katika nyanja ya muziki kwa ujumla nchi za Afrika ya mashariki ikifuatia Kenya lakini pia katika uchunguzi uliofanywa na GK kwakusikiliza maoni ya watu mbalimbali inaonekana kwamba licha ya Tanzania kuwa juu, lakini waimbaji wa nchini Kenya wameonekana kufanya kazi zao katika viwango vya juu katika recording audio pamoja na video hali ambayo ni tofauti na waimbaji waliowengi nchini ambao linapokuja suala la ubunifu katika kazi zao haswa video mara nyingi muongozo(script) unakuwa mbaya.
Paul Mwai katika moja ya huduma zake za kumwinua Mungu.              
Emmy Kosgei kuongeza nguvu katika tamasha hilo.   

MFALME WA R&B AFRIKA YA KUSINI AOKOKA, APOTEZA DILI YA KUFANYA KAZI NA MMAREKANI

IOL Loyiso mic
Loyiso Bala mfalme wa R&B Afrika ya kusini aliyeamua kuokoka.
Mashabiki wa mwanamuziki Loyiso Bala wa Afrika ya kusini ambaye amekuwa akitamba na aina yake ya muziki R&B kwa muda mrefu, hivi karibuni walipigwa na butwaa wengine kucheka na kushindwa kuamini walichokuwa wakikisikia kutoka kwa mwimbaji huyo pale alipoamua kuwasilimia kwa salamu ya ''Nawasalimu kwa jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo'' ikiwa katika uzinduzi wa album yake ya CD na DVD aliyoipa jina la ''Love Complete''.

Mwimbaji huyo aliyepewa jina la mfalme wa R&B nchini kwao, ameamua kuachana na uimbaji wa muziki wa nje ya kanisa na kuamua kumwimbia Mungu akitoa sababu nyingi ikiwemo aliyosema kwamba katika maisha yake amepata mafanikio makubwa sana ya muziki ikiwa pamoja na tuzo tano za SAMA na tuzo nyingine mbalimbali.

Ameimba mbele ya Will Smith, Oprah, zaidi ya mara nane kwenye kinyang'anyiro cha Miss SA, na mengineyo lakini katika hayo yote bado alikuwa akihisi kuna kitu hakikosawa ndani ya moyo wake na kitu chenyewe ni suala la kiroho jambo ambalo lilimfanya kwenda shule ya biblia ya Rhema Bible school ambako alikwenda kusomea kozi iitwayo ''Heart of Worship'' ambayo amesema ilimbadilisha haswa na kuona kabisa hakuna mwimbaji mwingine wa kumuimbia zaidi ya Mungu.

Loyiso ambaye ana miaka 30 sasa amesema hashangazwi na watu walivyoshangaa salamu hiyo licha ya kwamba walijua anazindua album ya gospel, amesema walijua ameimba album hiyo kwa ajili ya biashara lakini hawakujua ukweli kwamba sasa maisha yake yamebadilika kabisa na kuamua kumwimbia Mungu. Wakati hayo yakitokea mwimbaji huyo amepoteza nafasi ya kurekodiwa na mtayarishaji wa muziki nchini Marekani kama alivyokuwa akiomba maishani mwake itokee hivyo lakini imekuja kutokea wakati imani yake imebadilika na ujumbe wa nyimbo zake kumwelekea Mungu hali iliyofanya mtayarishaji huyo kuamua kuachana na mwimbaji huyo jambo ambalo hata hivyo mwimbaji huyo ajutii.

Mwimbaji huyu pia huwa anaimba na kundi la ndugu zake liitwalo Bala Brothers.
Haya ni baadhi ya maneno aliyonukuliwa akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na kile kilichotokea maishani mwake

''The funny thing is at the time that I made this decision, I had to let go an opportunity to record with a US producer. For years I had been trying to get a US deal and when this particular guy came through it was a big deal for me. 

He produced Jason Derulo, and all he needed was R400 000. But when I was in Scotland, with the Bala Brothers, I decided I wanted to make a gospel album. As I decided that, literally the following day, my manager called to say there was a guy in Kenya who was willing to pay for my trip to the US to record and I turned it down.

 I knew that my heart was not in it anymore,
I found greater purpose in doing Love Complete than go out there to be another stat,” he said.

KWA TAARIFA YAKO--WADOGO ZAKE UCHE WOTE WAFUATA NYAYO ZA WAZAZI ''WACHUNGAJI''

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu
Pastor Uche akiwa na mdogo wake anayemfuatia Pastor Samuel Bruno.
Ninadra sana kukuta familia ya watoto zaidi ya mmoja kufuata nyayo za wazazi wao wote kwa pamoja ama kama baba ni docta basi watoto wote wanakuwa madokta, basi KWA TAARIFA YAKO ni kwamba mwimbaji aliyejitambulisha vyema na wimbo wake wa ''My God is good'' kupitia kundi la Joyous Celebration pastor Agu Uchechukwu a.k.a Double double ambaye ni mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia yao ya watoto watano wa mchungaji Bruno.

Uche ambaye alibarikiwa mwaka 2010 kuwa mchungaji kupitia Alleluia Ministry ya Afrika ya kusini, mdogo wake anayemfuatia Samuel Bruno ni mchungaji ambaye amefungua huduma yake jijini London nchini Uingereza ikifahamika kwa jina la Hopeway Ministries International, huku wadogo zake kama Miracle Bruno, Chisomi Bruno wenyewe wako nyumbani Nigeria na wazazi wao wakitumika katika makanisa mbalimbali wakifahamika kama wainjilisti hata Uche alithibitisha hilo wakati alipofanyiwa mahojiano na Wapo Radio Fm siku zilizopita
.
                  


MY GOD IS GOOD EVERYTHING DOUBLE DOUBLE
Wimbo huu ndio uliompa Uche tiketi ya kujiunga na Joyous mwaka 2009 baada ya mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Maduhva aliyekuwepo katika kanisa la Rhema North aliposikia mwimbaji huyo akiimba wimbo huo nakuupenda nakuamua kumtafuta mmoja wa viongozi wa kundi la Joyous bwana Lindelani Mkhize(choir master) ambaye aliamua kumwalika Uche kwenye mazoezi yao na kuanza kuufanyia mazoezi wimbo huo hatimaye kurekodiwa na Uche milango kuanza kufunguka nasasa anashiriki na waimbaji wengine wa kimataifa wa injili jukwaa moja.

Pamoja na hayo mwimbaji huyu lengo lake lilikuwa awe mwanasheria hakuwahi kuwaza kuja kuwa mwimbaji ingawa alipokuwa mtoto alikuwa akiimba kwaya ya watoto, amesema wazazi wake hawajawahi kumlazimisha kumwamini Mungu ama kuwa mwimbaji bali walikuwa wakimuombea mpaka Mungu alipomuonyesha wito wake katika maisha ambako anasema kwakweli ana kila sababu ya kumshukuru Mungu mambo yanakwenda vizuri.
Wazazi wa pastor Uche.

Uche akiwa na wadogo zake waishio Nigeria alipowatembelea mapema mwezi May mwaka huu.

HEBU MFAHAMU EPHRAM SEKELETI KUTOKA ZAMBIA MWIMBAJI MAALUFU WA NYIMBO ZA INJILI

HISTORIA YA MWANAMUZIKI WA INJILI EPHRAIM SEKELETI MUTALANGE


Ephraim Sekeleti
Ephraim Sekeleti Mutalange ni muimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini Zambia, alizaliwa Mwaka 1983 katika mji wa Kalulushi nchini Zambia. Alimaliza elimu yake ya sekondari katika shule ya Kalulushi mwaka 2001.

Ephraim ni mtoto wa pili toka mwisho kati ya watoto sita, aliingia kwenye muziki wa injili tangu akiwa kinda huku alifundishwa kupiga kinanda na mmishonari alipokuwa bado mdogo. Mama yake anasema  “ Ephraim alikuwa ni mtoto aliyekuwa wa kelele nyingi”. Yeye pamoja na dada zake waliimba kanisani wakitumia kinanda na huko alipata uzoefu katika uimbaji na upigaji wa kinanda. Baadaye alijiendeleza katika uimbaji kwenye kikundi kilichojulikana kwa jina la  “Virtue for Christ” na aliimba katika kikundi hicho kwa muda wa miaka miwili.
Ephraim akiimba katika ibada ya kanisa la redeemed christian nchini Australia
 Mwaka 2002 akiwa na kiu ya kurekodi album yake, Aliamua kujitoa muhanga kwenda Afrika ya Kusini kwa kutumia kiasi kidogo tu cha pesa alichokuwa nacho, nia ilikua ni kurekodi album yake ya kwanza. Pamoja na jitihada hizo, baada ya kufika nchini Afrika ya Kusini alijikuta anaweza kurekodi nyimbo mbili tu kati ya album nzima. Hivyo akaamua kujiingiza katika Theater ya Pretoria na ndipo akapata fursa ya kuimba mbele ya Rais wa Afrika ya Kusini. Nafasi nyingi ziliendelea kujitokeza zilizomsababishia kutaka kuacha kuendelea na muziki wa injili ili aimbe miziki ya kidunia, lakini akawa muaminifu kuendelea na uimbaji wa injili. Mlango ulifunguka kumruhusu kurekodi album ya kwanza iitwayo Temba Baby“(Mtoto wa Miujiza)”.

Baada ya kurekodi, na kuuza nakala za kutosha za album hiyo ya Temba boy, kwa mafanikio ya hiyo kazi Ephraim aliamua kurudi nyumbani kuwekeza ile fedha. aliona awekeze zaidi kwenye ya album yake ya pili iliyopata mafanikio makubwa iliyoitwa Limo Ndanaka. Hi album imefanya vizuri kwenye chati mbalibali za muziki wa injili. Ephraim akiwa nje ya Zambia ameimba katika nchi mbali mbali zikiwemo Namibia, Afrika ya Kusini, Tanzania, Zimbawe na Australia.

Ephraim akiwa na mkewe Faith Mutalange
   
Alisema anafurahi akiona watu wasiokuwa na tumaina la Kristo wakianza kuwa na matumain, Licha ya kufanya muziki wake nchini Zambia amewahi kuja nchini Tanzania na kurekodi album yake nzima kwa Lugha ya Kiswahili. Moja kati ya Nyimbo zake zinazotamba hapa nchini ni pamoja na
Binti wa Ephraim

                                             1. Uniongoze                                 
                                             2. Baraka Zako
                                             3. Huu Mwaka 
 
 Ephraim hajui Kiswahili fasaha na nyimbo zake hizo alifundishwa kuziimba kwa lugha ya Kiswahili na Mchungaji ambaye pia ni muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Tanzania Ency Mwalukasa. Ephraim amesema ataendelea kuhubiri kwa njia ya uimbaji kwa sababu imempa changamoto zilizomuinua. Licha ya uimbaji Ephraim amefunga ndoa na Faith Chelishe na wamejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike

                                                                                                                                                        


Ephraim na Faith

HIVI NDIVYO LOVE TANZANIA FESTIVAL ILIVYOKUWA KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI


Maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es salaam hapo jana waliweza kufurika katika viwanja vya Jangwani jijini   hapa ili kupata baraka zao katika sherehe za Ipende Tanzania (Love Tanzania Festival) inayoongozwa na muhubiri Andrew Palau akishirikiana na waimbaji kutoka ndani na nje ya nchi wakiongozwa na Don Moen na mwanadada Nicole C. Mullen ambao wameweza kuwabariki wengi kwa huduma yao.

Katika siku ya kwanza hapo jana watu walipigwa butwaa kuona mchezo wa kuruka na pikipiki, uimbaji na muziki kwa ujumla hasa wakati walipoimba waimbaji Nicole na Don Moen vyombo viliweza kusikika vyema kabisa, sherehe hizo zinatarajiwa kuhitimika hii leo katika viwanja hivyo vya Jangwani kuanzia majira ya saa saba mchana hadi saa 2 usiku.




Vijana walioongozana na Askofu Andrew Palau wakitoa burudani na mafundisho ya dini kwa njia muziki.
Umati wa watu ukiwa kwenye foleni ya kupata huduma ya chakula uwanja hapo.
Michezo ya pikipiki.


Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wakishuhudia mchezo wa Baiskeli.
Mmoja wa wafanyakazi wa Kampuni ya Green Waste Pro Ltd akihakikisha swala usafi linazingitiwa uwanjani hapo kama inavyoonekana.




Mchezo wa kuruka na baiskeli ambao pia uliwaacha watu midomo wazi, picha kwa hisani ya Issamichuzi blog.
Masanja Mkandamizaji jukwaani akimsifu Mungu wake.
Askofu Andrew Palau akitoa ujumbe wa neno la Mungu.
Don Moen akiwa jukwaani kumtukuza Mungu.
Don Moen akiendelea kumsifu Mungu katika sherehe hizo.
Mwanadada Nicole C. Mullen akiwa jukwaani, aliweza kuwabariki watu alipoimba wimbo my redeemer lives kwa kiswahili. picha kwa hisani ya mulengathehero blog pamoja na Rick Japhet.

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog