MAMBO YAZIDI KUNYOOKA KWA WAIMBAJI WA GOSPEL NCHINI
Akiwa chini ya kampuni maarufu ya muziki duniani ya Sony Music kwa barani Afrika ikiwa imejikita nchini Afrika ya kusini, tayari mwimbaji huyo alishakamilisha album ya sauti wiki mbili zilizopita na kwasasa tayari ameanza kurekodi nyimbo zilizobaki katika video yake hiyo ambayo inategemewa kuleta kitu cha tofauti kuanzia usikivu wa kanda bya sauti mpaka video kutokana na ubora wa kampuni hiyo ya Sony.
Rose Muhando katika pozi la picha. |
Hii itakuwa mara ya pili kwa Upendo kuingia nchini Marekani kwa ajili ya huduma ya kumtangaza Kristo ikitanguliwa na safari ya kwanza aliyokuwa ameambatana na waimbaji wenzake Upendo Kilahiro pamoja na Christina Shusho mwishoni mwa mwaka jana, ambapo tayari mwimbaji huyo ameshawasili nchini Marekani na kulakiwa na wenyeji wake.
Upendo Nkone akipokewa uwanjani mara baada ya kuwasili nchini Marekani. |
0 comments:
Post a Comment