KUELEKEA UCHAGUZI MKUU TAG, MAJAMBAZI WAVAMIA MAKAO MAKUU, WAHARIBU VITU NA KUIBA LAPTOP 3
Kanisa la TAG likiwa linajiandaa na uchaguzi wa nyadhifa mbalimbali
unaotarajia kufanyika Dodoma, watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi
wamevamia ofisi za kanisa la TAG
makao makuu na kuiba, usiku wa kuamkia Jumanne.
Taarifa zilizoifikia blog hii watu hao walivamia juzi usiku na kuwafunga kwa kamba walinzi waliokuwa zamu na hatimaye kuvunja ofisi mbali mbali za makao makuu ikiwemo ya askofu mkuu na kuharibu samani.
Taarifa zilizoifikia blog hii watu hao walivamia juzi usiku na kuwafunga kwa kamba walinzi waliokuwa zamu na hatimaye kuvunja ofisi mbali mbali za makao makuu ikiwemo ya askofu mkuu na kuharibu samani.
Askofu Mkuu wa TAG, Barnabas Mtokambali |
Watu hao waliweza kufanikiwa kuiba laptop 3 katika ofisi hizo na
hatimaye kuhamia ofisi za kanisa la TAG Ubungo ambako walifanya
uharibifu na kufanikiwa kuiba sefu ya pesa, inayokadiriwa kuwa na kiasi
cha shilingi milioni 6 za ujenzi wa kanisa, mafungu ya kumi na sadaka
ambazo kiasi chake bado hakijafahamika.
Habari zaidi zinasema baadae sefu hiyo ilitelekezwa maeneo ya Kigogo na ikiwa limevunjwa na kuchukuliwa pesa yote.
Pamoja na wizi huo lakini leo ndiyo baadhi ya wajumbe wanaendelea kwenda katika mkutano mkuu wa kanisa la TAG unaofanyika Dodoma ambako kufanyika uchaguzi wa nyadhifa mbalimbali.
Habari zaidi zinasema baadae sefu hiyo ilitelekezwa maeneo ya Kigogo na ikiwa limevunjwa na kuchukuliwa pesa yote.
Pamoja na wizi huo lakini leo ndiyo baadhi ya wajumbe wanaendelea kwenda katika mkutano mkuu wa kanisa la TAG unaofanyika Dodoma ambako kufanyika uchaguzi wa nyadhifa mbalimbali.
0 comments:
Post a Comment