Home » » RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU AWATAKA WAKRISTO NCHINI KUONGEZA KASI YA SALA

RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU AWATAKA WAKRISTO NCHINI KUONGEZA KASI YA SALA

Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa

=====================================
Na Gustav Chahe, Iringa              
RAIS wa Baraza la Maakofu Tanzania (TEC) Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa amewataka waamini wakristo kutokuwa na moyo wa kuhamaki kutokana na kitendo kilipuliwa Kanisa Katoliki huko Arusha.
Amezungumza hayo katika mahojiano maalum mtandao  huu wa www.matukiodaima.com mahojiano  yaliyofanyika ofisini kwake Iringa juu ya vitendo vinanyoendelea kutokea nchini vikiwemo vya kuchomwa makanisa na kuuawa wachungaji wa kiroho huku vikihusishwa na imani za kidini.
Amesema kama ilivyoutamaduni wa Kikristo, yanapotukia matukio ya kusikitisha kama hayo silaha iliyo kubwa ni sala kumuomba Mungu atoe jibu kwa wanaohusika na mateso kama hayo.
“Kasi ya sala iendelee, ili Mungu wetu wa Amani ajenge fikira za upendo na haki katika mioyo yetu” alisema.
Amesema waamini wasikate tamaa na kuacha kusali kwa kuwa Mungu ndiye mwenye jibu na atatoa majibu kadiri atakavyo kwa wale wote wanaowatesa wenzao kwa sababu zao binafsi.
Hata hivyo alisema licha ya kuwa kila mtu amepokea kwa mshituko na maumivu makubwa, roho za watu zinazoteswa na wengine Mungu atazifariji na kuziponya lakini mtesaji atapata majibu yake.
Alisema waliopoteza maisha katika mlipuko huo Mungu atawarehemu na kuwafariji majeruhi wote.
“Waliopoteza maisha wapokee Rehema ya Mungu na waliojeruhiwa wafarijiwe na uwezo wa Mungu” alisema.
Hali kadhalika amesema upendo na haki ni zawadi kutoka kwa Mungu na hivyo, anayedhurumu wengine zawadi hiyo atapata pigo kubwa.
Aidha amesema wakati uliopo sasa ni wakutafakari na kumkabidhi Mungu yale yote yanayowasumbua wanadamu na kuongeza nguvu ya sala ili majibu ya Mungu yapatikane kwao.
“Tulieni na kufanya tafakari kasha mwambie Mungu hayo yote ayafanyie kazi kwa uweza wake. Sisi binadamu tunategemea nguvu kutoka kwake” alisema.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Search This Blog