Home » »



Meli STAR GET ya Kampuni ya SEAGULL iliyokuwa na abiria 248 imezama jana eneo la Chumbe

 Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imesema meli ya STAR GET mali ya kampuni ya SEAGULL Transport Company imezama leo, katika kisiwa cha Chumbe, Zanzibar ilikuwa na abiria 248 wakiwemo watoto 31 na watalii 10.

Taarifa ya mamlaka hiyo hiyo imesema, meli hiyo, MV SKY GET iliondoka katika Bandari ya Dar es Salaam leo saa sita mchana, ikiwa na mabaharia tisa.

Taarifa nyingine (si za SUMATRA) zinasema sababu ya kupinduka kwa meli hiyo inadhaniwa kuwa ni kutokana na upepo mkali uliosababisha mawimbi kuipiga nakupindukia upande mmoja.

Inaelezwa kuwa abiria wengi wameokolewa kutokana na jitihada mbali mbali kupitia msaada wa boti za Mv Kilimanjaro, Tug ya Bandari na vyombo vingine. Waliojeruhiwa wanatibiwa katika Hospitali ya Mnazimmoja.

Kwa mujibu wa SUMATRA meli hiyo imesajiliwa na Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) na kwamba, Cheti cha Ubora kimeanza tarehe 24 Agosti, 2011 na kinamalizika 23 Agosti, 2012. Imesema, meli hiyo ilikuwa imeruhusiwa kubeba abiria wanaoruhusiwa 300 na tani 26 za mizigo.

“SUMATRA kupitia Kituo cha Utafutaji na Uokoaji (MRCC) ilipata taarifa kuwa meli ya MV SKY GET iliyokuwa safarini kutoka Dar es Salaam kuelekea Zanzibar ilikuwa inazama katika eneo la karibu na kisiwa cha Chumbe, Zanzibar, eneo ambalo lipo umbali wa Kilomita za Bahari 13.8 kutoka Bandari ya Zanzibar” imesema taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa Sumatra, baada ya kupata taarifa hizo, kituo cha MRCC kilitoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na vyombo vya usafiri wa majini vilivyokuwa karibu na eneo la tukio.

“ Zoezi la uokoaji linaendelea katika eneo la tukio kwa msaada wa vyombo vifuatavyo: Mv Flying Horse, Mv Kilimanjaro III, Tug Bandari ya Zanzibar, KMKM, Mv Zanzibar I, Police Patrol Boat, Navy” imesema taarifa hiyo.

Inaripotiwa kuwa hadi sasa, watu zaidi ya 145 wameokolewa na miili ya maiti 16 imeopolewa.

Waziri wa Ulinzi Dkt. Emmanuel Nchimbi alisitisha kusoma hotuba ya Wizara yake kwa kutumia kanuni ya 58 kifungu cha 5 kuomba kutoa hoja iliyokuwa inaendelea, ili kujadili jambo jingine muhimu.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog