Home » »

KWA TAARIFA YAKO - LICHA YA KUPATA MCHUMBA MALOPE HATAKI NDOA, PIA AFADHILIWA KWA KUPIGWA MAKOFI NA WAIMBAJI WAKE

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu
Rebecca akiwa na mchumba wake bwana Tshabalala walipokuwa kwenye mahojiano WAPO Radio FM.
Leo katika kipengele cha KWA TAARIFA YAKO tunaelekea huko nchini Afrika ya kusini ambako tunakutana na mwanamama malikia wa muziki wa gospel barani Afrika bibie Rebecca Malope mama huyu ambaye ana umri wa miaka 44 sasa ni kwamba kama tulivyowahi kuandika alipotembelea nchini mapema mwaka huu wakati wa pasaka kwamba baada ya kukaa mpweke kwa miaka mingi mwanamama huyu kwasasa amepata mchumba aitwaye Themba Tshabalala.

Mchumba ambaye pia alikuja naye nchini, lakini linapokuja suala la kufunga ndoa mwanamama huyu anasema bado mapema saaana kwani anataka kwanza wafahamiane vyema na mchumba wake huyo ambaye pia ni mmoja wa mameneja wake. Amesema mpaka sasa amewakataa wanaume watatu waliokuwa tayari kumuoa kwasababu hakuwa tayari, ila anadhani mwanaume huyu ndio mwafaka ingawa anasema bado yupo yupo kwanza kwenye suala la kufunga ndoa.

VITUKO VYA WAIMBAJI ALIOWATOA KIMUZIKI

Mwanamama huyu ambaye anamafanikio sana kwenye medani ya muziki barani Afrika, amewatoa waimbaji wengi sana akiwemo Lundi Tyamara mwanakaka ambaye ukisikiliza sauti yake inafanana na Rebecca, pia ni mwimbaji aliyekuwa mwitikiaji katika band ya Malope, lakini cha ajabu ni kwamba kati ya waimbaji wawili waliokuwa wanataka uadui na Rebecca ni mwanakaka huyu na dada mwingine ambaye alidiriki hata kumpiga makofi Rebecca kutokana na kile kwamba mwimbaji huyu anakubalika sana, kufuatia tukio hilo Rebecca alikaa kimya ingawa vyombo vya habari nchini humo viliandika tukio hilo.

Pamoja na hayo Rebecca ameendelea kusimama katika huduma pamoja na mashambulizi na maneno mengi yaliyowahi kusemwa juu yake na waimbaji hao likiwemo suala la mwanamama huyo kuhusishwa na ulevi wa pombe, kilichofanyika kwa sasa waimbaji hao wamejirudi na kumuomba msamaha mwanamama huyo huku Lundi akiwa tayari amejishusha kabisa katika suala la Gospel kutokana na shutuma nyingi juu yake kutoka katika vyombo vya habari.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog