Home » »

BREAKING NEWS....WALI WA SHEREHE WAUA MMOJA 40 HOI IRINGA

Wahanga wa tukio hilo wakiwa hoi kituo cha afya Ipogolo Iringa
Mganga mfawidhi wa kituo cha afya Ipogolo Dkt mary Makundi
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Ibofye wilaya ya Kilolo Godfrey Mtete (kushoto) akiwa na mgonjwa mwingine ktk kituo cha afya Ipogolo walikolazwa kwa kula chakula chenye sumu

MTU mmoja mkazi wa kijiji cha Ibofye wilaya ya Kilolo mkoani Iringa amefariki dunia na wengine zaidi ya 40 wamelazwa katika Hospitali mbali mbali za mkoa wa Iringa kikiwemo kituo cha afya Ipogolo na Hospital ya rufaa ya mkoa wa Iringa baada ya kula wali na kunywa togwa zinazosadikika kuwa na sumu katika shehere ya kutoa mahali .

Wahanga wa tukio hilo ambao wamelazwa katika kituo cha afya cha Ipogolo mjini Iringa waliueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com leo kuwa tukio hilo lilitokea juzi jumamosi baada ya mkazi wa kijiji hicho Bw James Ngaile kuandaa chakula na kinywaji hicho aina ya togwa kwa kwa ajili ya sherehe ya kuoza binti yake.

Alisema Yamile Mhehe ambaye amelazwa katika kituo hicho cha afya kuwa utaratibu wa chakula katika sherehe hiyo ilikuwa ni sahani moja kwa watu watatu na kuwa chakula kilichoandaliwa ni wali na ugali huku mboga ikiwa ni maharage na kabichi na baada ya chakula wageni walikuwa wakitumia kinywaji aina ya togwa kwa ajili ya kushushia chakula hicho.

Hata hivyo alisema baada ya kula chakula hicho muda wa saa moja usiku wananchi waliofika katika sherehe hizo walitawanyika kurejea majumbani kwao na kuwaacha walengwa wa sherehe hiyo wakiendelea na mapumziko ya usiku.

Alisema baada ya kufika nyumbani muda wa saa 2 usiku tumbo la kuharisha damu lilianza kumsumbua yeye na mke wake na hivyo kulazimika kukimbia kwa majirani kuomba msaada zaidi na baada ya kufika huku walikuta majirani zao nao wakisumbuliwa kama wao hali iliyowalazimu kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kijiji ambaye pia alikuwa hajiwezi kutokana na kukumbwa na tatizo kama hilo.

Hivyo kutokana na hali hiyo kuonekana kuwakumba watu zaidi ya 20 katika kijiji hicho uongozi wa kijiji ulilazimika kukodisha daladala na kuwachukua wagonjwa wote na kuwapeleka kituo cha afya Ihimbo na baadhi yao ambao hali zao zilionekana kuwa mbaya walikimbizwa kituo cha afya Ipogolo na wengine Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Iringa.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Godfrey Mtete alisema kuwa tukio hilo ni la kwanza kutokea katika kijiji hicho na kuwa hadi sasa bado hawajabaini tatizo lilikuwa katika chakula ,mboga ama togwa hiyo kwani alisema mbali ya tatizo hilo kuwakumba watu waliofika katika sherehe hiyo baadhi ya watoto kama watatu wamelazwa patwa na mkasa huo japo hawakula chakula wala kunywa kinywaji katika sherehe hiyo.

Mtete alisema hadi sasa mtu mmoja ambaye yeye alikuwa akimwita mjombe wake aliyemtaja kwa jina la Wagila Nyaupumba amefariki dunia kabla ya kukimbizwa hospital kwa matibabu.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa idadi ya wananchi waliopatwa na tatizo hilo ni 40 na kuwa watu zaidi ya 38 ndio ambao walionekana kuwa mahututi zaidi na kukimbizwa kupatiwa matibabu huku baadhi ya wananchi wameendelea kufikishwa Hospitalin jana baada ya kuonekana kuathirika na chakula hicho.

Alisema hatua ambayo kijiji kimechukua kuhusu chakula hicho ni kuzuia chakula hicho kumwagwa wala kupewa nguruwe ili kiweze kuchunguzwa zaidi .

Aidha alisema mbali ya chakula hicho kuwakumba wageni waliofika katika shughuli hiyo ya kuona binti bado bibi harusi mtarajiwa na bwana harusi pamoja na wazazi wa pande zote mbili pia ni wahanga wa tukio hilo .

Mganga mfadhiwa wa kituo cha afya Ipogolo Dkt Mary Makundi alithibitisha kupokea wagonjwa 9 kati ya 40 katika kituo hicho na kuwataja wagonjwa waliolazwa katika kituo hicho kuwa ni Rafiki Kabogo, Beth Ngaile, Neema Ngaile, Emelia Mwalafi, Edina Mkemangwa, Costanzia Maliga, Ayubu Kaywanga Godfrey Mtete na Yamile Mhehe.

Huku akidai hali zao zinaendelea vizuri na kuwa wagonjwa wengine walifikishwa hospitali ya mkoa wa Iringa na kituo cha afya Ihimbo kwa matibabu zaidi .

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael kamhanda alipoulizwa na mtandao huu kwa njia ya simu jana kuhusu tukio hilo alisema bado halijafika ofisini kwake na kuwa pindi litakapomfikia atalitolea ufafanuzi.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog