Imani .....Party 2
Ndugu mpendwa nakukaribisha sana katika mfululizo huu wa
makala ya Imani;naamini unazidi kubarikiwa na somo hili.Ni mimi Docta Lightness
William Ng’unda karibu tuendelee.
Makala
yaliyopita tulizungumza juu ya imani inayoambatana na matendo, na leo
nitaendeleza hapohapo ili nisikuache.Imani ya matendo inaenda pia sambamba na
ukiri wetu na ni muhimu kuchunguza sana ukiri wetu sio kwa kinywa tu bali
katika matendo pia.Ukiri wa matendo huwa una nguvu hata kuliko ukiri wa
maneno.Namaanisha usiishie kusema tu bali weka hayo maneno kwa matendo pia.Ni
muhimu ukiri wa maneno uende sambamba na ukiri wa matendo.
Mfano mzuri ni huu watoto wengi wa Mungu
wamekuwa wanaishi maisha ya kutozingatia kazi,na wanapendelea maisha ya
mteremko kwa watu wengine huku wakidai wanaishi kwa IMANI.Mungu anashindwa kuwabariki kwa sababu hakuna
wanachokifanya,wanaishia kumlaumu Mungu na kumwona Mungu kama muongo na kumbe
sivyo ilivyo.Mungu ameweka wazi katika (2Wathesalonike3:10)
Asiyefanya kazi na asile.Lazima uweke mikakati yako kiroho,kinafsi,kiakili
na kimwili kupitia ahadi za Mungu ili afanikishe mipango yako. Ukiomba pesa
fanya kazi fulani ili Mungu atumie huo mlango kukubariki huku ukiamini.
IMANI NI MKONO WA
KUPOKEA MAJIBU
Watoto wengi wa
Mungu ni waombaji wazuri lakini sio wapokeaji wazuri.Namaanisha mtu anaweza
funga hata siku 21 akiomba tu lakini upande wa upokeaji hayupo wala
haelewi.Maombi ni mazuri sana ila usiwe unajitesa bure lazima ujue kupokea
pia.Inawezekana mambo unayopitia Mungu alishayajibu siku nyingi lakini hukujua
jinsi ya kupokea na ndio maana biblia inasema
(Hosea 4:6) watu wangu
wanaangamia kwa kukosa maarifa).Nguvu ile ile uliyoitumia kuomba itumie
nguvu hiyohiyo kupokea.Namaanisha ukijua umeomba jambo lolote sawasawa na
mapenzi ya Mungu hilo ni lako tayari, na kujua kwamba ni mapenzi ya Mungu
utaangalia neno lake linasema nini juu ya hilo jambo unaloliomba na hayo ndiyo
mapenzi ya Mungu.Na huu ndio ujasiri
tulio nao kwake,ya kuwa, tukiomba kitu
sawasawa na mapenzi yake, atatusikia.Na
kama tukijua kwamba atusikia,tuombacho chote,twajua kwamba TUNAZO zile haja
tulizomwomba.’(1 Yohana 5:14) Hapa inamaanisha nini? tunajua tunazo zile
haja, kwa hiyo ukiomba uwe na ujasiri kuwa tayari unazo haja unazoziomba kwa
njia ya imani.
USHUHUDA WANGU
Rafiki najua
shuhuda zinajenga sana na zinainua sana imani ya mtu,mimi nina shuhuda nyingi
sana ila ni kwa nia ya kukujenga ili ujenge shauku ndani yako na Mungu atafanya
zaidi.Nilikuwa natamani sana kuwa lecture/mwalimu wa chuo kikuu.Na nilipomaliza
elimu yangu ya udactari ya chuo kikuu niliomba nafasi ya kuwa mwalimu katika
chuo nilichosomea.Tulifanya interview na nilikosa ile nafasi, binafsi iliniuma
sana lakini kwa sababu sikuwahi kuwa na
uzoefu wa kufundisha,na katika interview wenye uzoefu walikuwepo hivyo
wakachukuwa wenye uzoefu mimi nikakosa.Nikamuuliza Mungu akaniambia umeomba
sana anza kuamini kuwa wewe ni lecture nikaanza kukiri ingawa ilikuwa ngumu
sababu Tanzania kuna chuo kimoja tu cha kazi niliyosomea ya walemavu,ikabidi
nitafute kazi nchi za ulaya na Asia kwa vile walitangaza ajira pia.Siku moja
baada ya kuendelea kuamini niliitwa chuo hichohicho nikaambiwa wiki inayofwata
nije kazini na nilikuwa napenda sana kuanza kufaya kazi Tanzania na Mungu
akanijibu haja ya moyo wangu, na sasa ni lectuere.Usiogope hata wewe mpendwa
Mungu aliyetenda kwangu namsii atende na kwako pia ili aufariji moyo
wako.Usiogope Mungu anajua kilichobora kwa ajili yako maadamu Bwana ni mchungaji wetu hatutapungukiwa na
kitu (ZABURI 23:1) halleluya.Mungu ametuumba tutawale dunia nchi na vyote vijazavyo ni mali ya bwana
dunia na wote wakaao ndani yake (Zaburi 24:1),inamaanisha kazi zote pia ni
mali yake na anajua wapi atakuweka na kwa wakati gani rafiki.
Nimesema tena
imani ni mikono ya kupokea mahitaji na haja zetu tunazoomba.Tunapokea kwa
kadiri ya nguvu itendayokazi ndani yetu yaani imani yetu.Inamaanisha imani yako
ikiwa na viwango fulani unapokea haraka zaidi kinachotofautisha majibu mengi ya
wana wa Mungu ni imani waliyonayo kwa Mungu juu ya hilo jambo.Kila mtu
alipookoka alipewa kiwango cha imani sawa na mwenzake lakini huwa imani inakuwa
kulingana na unavyoifanyiza mazoezi ya kuiweka kwa matendo, na hapo ndipo
tunapotofautiana sisi kwa sisi.Na imani yako ikikaa bila matendo kuna mda
itakufa kama bibilia inavyosema (Yakobo 2:18) lakini
mtu akisema, wewe unayo imani ,nami ninayo matendo.Nionyeshe imani yako pasipo
matendo,nami nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo.Mstari wa 26 maana
kama vile mwili pasipo roho umekufa,hivyohivyo na imani pasipo matendo imekufa.
Ni kwa kadiri ya uhakika wa neno la Mungu
uliondani yako yaani imani yako ndiyo utapokea na ndiyo maana huwa nasisitizia
sana watu wawe wasomaji wa neno ili waongeze uhakika wa mambo yao katika kuzijua
ahadi zao na shetani hatakuweza kwa jana la Yesu.Embu fikiria kuhusu hali unayopta ni kweli hauna uhakia wa
neno la Mungu juu ya hali hiyo? Kuna nini Mungu amesema juu ya hali hiyo kwenye
neno lake? Anasema (1Petro 5:7) Huku
mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana na mambo
yenu. Dai haki yako kwa baba yako maana wewe ni mwana wake na si mtumwa
tena.Mungu si mwnadamu hata aseme uwongo ahadi zae zinasimamaa hata nyota
zingezimika ahadi zake zadumu hata milele Haleluya.
Imani ni kuwa
na uhakika /ujasiri na udhibitisho moyoni ukisoma tafsiri mbalimbali za
kiyunani.Unapoomba ule uhakika wa haja zako kwamba Mungu atakujibu na ujasiri
ndio mikono ya kupokea.Ninamaanisha unapokuwa na imani mambo yatarajiwayo
yanakuwa wazi au halisi kwako na ndani yako kabla hayajathihirika, nikimaanisha
unaanza kuona majibu yako kwa macho ya
imani.
Hivyo imani kama mikono inaambatana na
ujasi ili upokee nitafafanua zaidi hapa na kwa mifano ili uelewe zaidi.Kuna
kipindi nilikutana na hali fulani nilipoanza kazi,Mungu aliambia nikianza kazi
nimpatie mshahara wangu wa kwanza kama malimbuko.Na hata wazazi wangu na
marafii walikuwa wananiambia kumbuka mshahara wa kwanza sio wako Lightness.Nilipokuwa
nawaza nitaishi vipi mwezi mzima Mungu akanipa wazo la kuanzisha biashara kwa
mtaji wa sh alfu 10 tu.Nilikuwaga muoga sana wa kufanya biashara nikawa
nikitoka kazini nauza hereni, mikufu na
bangili za wanawake kwa rafiki zangu maofisini na kanisani.Nikaanza kupata hela
nyingi sana hadi mtaji ukafika laki moja
na kuendelea, na mpaka sasa najisikia raha sana kufanya biashara na nimeweza
hadi kuajiri watu wasiokuwa na kazi nafanya nao na nawalipa.Nitumia ujasiri na
Mungu ananibariki sana na sijawahi kupungukiwa au kujuta naipenda kazi yangu na
mshahara sasa ni kama mtaji wangu
0 comments:
Post a Comment