Home » » KWELI DUNIA HAINA HURUMA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

KWELI DUNIA HAINA HURUMA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

JAMAA AMUUA MKE WAKE KWA KUMCHINJA NA KISHA KUMTOBOA KIFUANI WAKIWA GESTI HUKO DAR



Mwili wa marehemu


Mtuhumiwa wa mauaji


Mkazi wa Tabata Mawenzi, Remi Joseph (36) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe kwa kumkata kichwa kwenye nyumba ya wageni ya Friends Corner ya jijini Dar es Salaam. 


Aliyeuawa ni Josephena Moshi (35), ambaye alikatwa kichwa na kuchomwa na kitu chenye ncha kali kifuani wakiwa kwenye nyumba ya wageni ya Friends Corner. 


Akihojiwa kuhusiana na tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Augustine Senga, alikiri kutokea mauaji hayo.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Alhamisi saa 8:00 mchana na kwamba familia hiyo ilikuwa inaishi Tabata Mawenzi. 
Senga alisema mwanamke huyo alifariki papo hapo baada ya kushambuliwa na kwamba chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika na uchunguzi unaendelea.

Kamanda Senga alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili na mtuhumiwa anashikiliwa na polisi. 


Hata hivyo, gazeti hili lilijulishwa kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kufanya mauaji hayo, alifanya jaribio la kutaka kujiua lililoshindikana. 

Kamanda alipoulizwa kuhusiana na mtuhumiwa huyo kutaka kujiua, alisema kuwa uchunguzi unaendelea. 

“Bado ni mapema sana kueleza kila kitu hayo niliyokueleza ni taarifa za awali kwani na huyu mtuhumiwa amekutwa na majeraha shingoni, hivyo masuala ya kazi yake na sababu vinachunguzwa,” alisema Senga.
Na Beatrice Shayo-Dar es salaam
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog