MKUU WA KITUO CHA POLISI JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA MAHABUSU HUKO NJOMBE.
Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mkoa ya Njombe, imemhukumu aliyekuwa mkuu wa kituo cha
Polisi Ilembula kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kukutwa na hatia ya
kumbaka mtuhumiwa aliyekuwa ndani ya mahabusu.
Hukumu
hiyo ilitolewa na Hakimu Augustine Rwezile, baada ya mshtakiwa huyo
James Nyambenga kukiri kosa hilo mahakamani, ambapo mshakiwa huyo
anadaiwa kumtoa msichana huyo kwenye chumba cha mahabusu alikokuwa
anashikiliwa na kumbaka.
Mwanamke huyo ambae ni mhudumu wa bar alikuwa anashikiliwa kwenye mahabusu ya kituo hicho kwa tuhuma za uzururaji.
Akisoma
hukumu hiyo Hakimu Rwezile amesema ushahidi uliotolewa na upande wa
mlalamikaji na vielelezo vya daktari aliyempima msichana huyo viliweza
kuithibitishia Mahakama kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo.
0 comments:
Post a Comment