BINTI WA MIAKA 27 AUAWA KWA KUKATWA MAPANGA HUKO SHINYANGA VIJIJINI, WIVU WA KIMAPENZI WAHUSISHWA.
Mwanamke mmoja
aliyefahamika kwa jina la Huma Simon (27) mkazi wa kitongoji cha Solwa
Kata ya Solwa Wilayani Shinyanga Vijijini ameuawa kwa kukatwa mapanga na
watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana.
Kwa mujibu wa Majirani
Mwili wa marehemu Huma umekutwa asubuhi katika eneo la Shule ya msingi
Solwa ukiwa umekatwa mapanga sehemu mbalimbali na kutelekezwa.
Taarifa zimesema Huma
ambaye anaishi na Mama yake Mzazi, alitoka usiku katika chumba alichokua
amelala na kumuacha Mtoto wake wa kike anayekadiriwa kuwa na miaka
miwili, na kukutwa asubuhi akiwa ameuawa.
Wananchi wa Kata Solwa wakiutazama Mwili wa Marehemu eneo la Tukio
Aliyebebwa Mgongoni Ndio Mtoto wa Marehemu aliyeachwa na Mama yake akiwa amelala usiku.
Mama Mzazi wa Marehemu akiwa amekaa chini analia mara baada ya kukuta Mwanae akiwa ameuawa
Mwili wa Marehemu Huma ukiwa unachukuliwa na Maafisa wa Polisi
Wananchi wa Kata Solwa wakiutazama Mwili wa Marehemu eneo la Tukio
Aliyebebwa Mgongoni Ndio Mtoto wa Marehemu aliyeachwa na Mama yake akiwa amelala usiku.
Mama Mzazi wa Marehemu akiwa amekaa chini analia mara baada ya kukuta Mwanae akiwa ameuawa
Mwili wa Marehemu Huma ukiwa unachukuliwa na Maafisa wa Polisi
0 comments:
Post a Comment