Chama cha Kutetea Abiria Tanzania (CHAKUA) Kimemtaka Waziri Sitta Aibane SUMTRA Ipunguze Nauli
CHAMA cha Kutetea Abiria Tanzania (CHAKUA) kimewaomba Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sita kuingilia kati na kuagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), isikilize kilio cha wananchi kuhusu kupunguzwa kwa nauli.
Hayo yalisemwa jana na mwenyekiti wa chama hicho, Hassan Mchanjama wakati akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es Salaam.
Alisema
wamefikia uamuzi huo baada ya Ewura kushusha bei ya mafuta, hivyo ni
vyema na abiria nao wakanufaika kutokana na mafuta kushuka tangu mwaka
jana Desemba, kwani inaonekana wanaonufaika ni wamiliki wa vyombo vya
usafiri.
Aliongeza
kuwa imekua ikishuhudiwa mara kwa mara mafuta yakipanda kidogo, nauli
nazo zinapanda haraka, lakini mafuta yakishuka Sumatra hawataki kuitisha
mkutano na wadau ili kujadili kushusha nauli .
“Sisi
Chakua tumechukua hatua ya kwanza kuwaandikia barua, lakini Sumatra ipo
kimya tukaandika tena Februari 5, lakini bado wamekaa kimya,” alisema Mchanjama.
Alisema
Chakua inataka nauli zote zipungue kwa asilimia 25, kwa mfano nauli za
daladala chini ya kilometa 10 nauli ya sasa ni Sh 400 hivyo ipungue hadi
Sh 300 na mikoani nauli ipungue kwa asilimia 25.
Alisema
nauli ikipungua itasaidia kupunguza bei za bidhaa nyingine ikiwemo
vyakula, kwani mfumko wa bei unachangiwa na gharama za usafirishaji.
Katibu
wa Barabara wa chama hicho, Gervas Rutaguzinda aliitaka serikali
kujenga vibanda vya kupumzikia abiria katika Kituo Kikuu cha Mabasi
Ubungo, kwani kila abiria anayeingia katika kituo hicho analipa Sh 200.
0 comments:
Post a Comment