Home » »

MGANGA WA KIENYEJI AKAMATWA NA BUNDUKI ILIYOTUMIKA MAUAJI YA MWANAMKE MJINI KAHAMA NA UJAMBAZI.


Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga linamshikilia mganga wa kienyeji Zacharia Ngobeko Dogo(35),mkazi wa kijiji cha Mbulu kata ya Mhongolo wilayani Kahama kwa kosa la kukutwa na bunduki aina ya SMG yenye namba 8945 iliyotumika katika mauaji ya  Mary Kashindye aliyeuawa kwa kupigwa risasi hivi karibuni wilayani Kahama.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Justus Kamugisha(Pichani) amesema mganga huyo wa kienyeji alikamatwa akiwa na silaha hiyo ikiwa na risasi nane ndani ya magazine iliyokuwa imehifadhiwa nyumbani kwake tarehe 18,2015 saa saba mchana.
Kamanda Kamugisha amesema mganga huyo na wenzake wawili wanatuhumiwa kuhusika katika matukio ya mauaji yaliyotokea tarehe 8 mwezi huu saa tatu usiku kwa kumuua Mary Kashindye kwa kumpiga risasi kutokana na ugomvi wa kiwanja kati ya marehemu na Jumanne Maige.
Amesema kutokana na ugomvi huo aliwakodi Andrew Buteye Mtakatifu(38) mkazi wa Tabora na Daudi Luchemela Ngasa(40) mkazi wa Nzega Tabora kutekeleza mauaji hayo.
Ameongeza kuwa silaha hiyo pia ilitumika katika unyang’anyi wa kutumia silaha wa tarehe 13 mwezi huu saa mbili usiku wilayani Kahama ambapo walipora shilingi milioni moja na nusu dukani kwa Manyangu Mboje.
Kamanda Kamugisha ameeleza kuwa katika mahojiano na watuhumiwa,wamekiri kuhusika katika matukio yote mawili na kuhifadhi silaha kwa mganga huyo wa kienyeji.
Katika hatua nyingine amesema watuhumiwa wamekiri kutenda makosa ya unyang’anyi kwa kutumia silaha katika mkoa wa Mbeya,Mwanza na Tabora.
Na Kadama Malunde-Shinyanga
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog