MAUAJI TENA SHINYANGA..!! MWINGINE AUAWA KWA KUKATWA MAPANGA USIKU WA MANANE AKIWA AMELALA NYUMBANI KWAKE.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha
Mwanamke aliyetajwa kwa
jina la Winfrida Simon (35) ameuawa kwa kukatwa mapanga baada ya
kuvamiwa na watu wasiojulikana akiwa amelala nyumbani kwake katika
kijiji cha Manyada, wilayani Shinyanga.
Kwa mujibu wa kamanda wa
polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha tukio hilo limetokea majira
ya saa nane usiku katika kijiji hicho kilichopo kata ya Usanda.
Kamanda Kamugisha
amesema watu hao wamemkata Winfrida mapanga sehemu za kichwani na
shingoni hali iliyosababisha kifo chake papo hapo.
Amesema chanzo cha
mauaji hayo bado kinachunguzwa na kwamba tayari watu wanne wanashikiliwa
na jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa mahojiano zaidi kuhusiana na
tukio hilo.
Kamanda Kamugisha
amewataja wanaoshikiliwa na polisi kuwa ni Misana Juma(30), Joseph
Jahila(24) Emmanuel Joseph(39) na Msafiri Kulwa wote wakazi wa Manyada
kata ya Usanda wilayani Shinyanga.
Tukio hilo linatokea
ikiwa ni Siku tatu tu baada ya watu watatu kuuawa kwa kukatwa mapanga
kisha kufungiwa ndani ya nyumba zaidi ya siku 5 katika kijiji cha Bugogo
wilayani Shinyanga.
0 comments:
Post a Comment