Home » » TAARIFA YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NDUGU KAILIMA RAMADHANI KUHUSU UPIGAJI KURA KATIKA UCHAGUZI UTAKAOFANYIKA TAREHE 15 NOVEMBA, 2015 KATIKA JIMBO MOJA NA KATA 25

TAARIFA YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NDUGU KAILIMA RAMADHANI KUHUSU UPIGAJI KURA KATIKA UCHAGUZI UTAKAOFANYIKA TAREHE 15 NOVEMBA, 2015 KATIKA JIMBO MOJA NA KATA 25


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

nembo%20ya%20NEC



TAARIFA YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NDUGU KAILIMA RAMADHANI KUHUSU UPIGAJI KURA KATIKA UCHAGUZI UTAKAOFANYIKA TAREHE 15 NOVEMBA, 2015 KATIKA JIMBO MOJA NA KATA 25
Ndugu Wananchi
Kama mnavyofahamu Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitoa taarifa ya kuahirishwa kwa uchaguzi katika majibo  nane (8) na Kata thelathini na nne (34). Sababu ya kuahirishwa uchaguzi katika Majimbo na Kata hizo kulitokana na vifo kwa wagombea katika Majimbo sita na majimbo mengine mawili yaliahirishwa kutokana na hitilafu mbalimbali.
Kesho tarehe 15 Novemba, 2015 ni Siku ya Kupiga kura ya kuchagua Mbunge katika Jimbo moja na kuchagua Diwani katika Kata 25.
Jimbo na Kata hizo ni kama inavyoonekana katika Jedwali hapa chini:#
Jedwali Na.1: JIMBO LINALOFANYA UCHAGUZI WA MBUNGE TAREHE 15.11.2015
NA
MKOA
HALMASHAURI
JIMBO
1.
Lindi
Masasi DC
Lulindi






Jedwali Na.1: KATA ZINAZOFANYA UCHAGUZI WA DIWANI TAREHE 15.11.2015
NA
MKOA
HALMASHAURI
NA
KATA
1.
Geita
Geita DC
1
Ludete
Mbogwe DC
2.
Isebya
2.
Tabors
Urambo DC
3.
Kiloleni
Nzega DC
4.
Mizibaziba
5.
Tongi
3.
Arusha
Ngorongoro DC
6.
Malambo
7.
Ngaresero
4.
Mara
Rorya DC
8.
Bakula
5.
Mwanza
Kwimba DC
9.
Bupamwa
6.
Mbeya
Chunya DC
10.
Mwambani
11.
Itewe
12.
Mkola
13.
Mbuyuni
Mbarali DC
14.
Rujewa
7.
Simiyu
Bariadi DC
15.
Matongo
8.
Tanga
Korogwe TC
16.
Majengo
9.
Tanga
Kilindi DC
17.
Songwe
10.
Njombe
Ludewa DC
18.
Mkongobaki
11.
Ruvuma
Madaba DC
19.
Mahanje
Namtumbo
20.
Mkongo Gulioni
21.
Lisimonji
12.
Kigoma
Kigoma Ujiji
22.
Kagera
13.
Rukwa
Sumbawanga DC
23.
Milepa
14.
Katavi
Mpanda DC
24.
Magamba
15.
Dar es Salaam
Kinondoni MC
25.
Saranga

Aidha, kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, nawapongeza wananchi wote katika Jimbo na Kata zinazofanya Uchaguzi kesho kutokana na utulivu waliouonyesha katika kipindi chote cha kusubili siku ya kupiga Kura kuchagua Mbunge au Diwani wao.
Ndugu Wananchi
Natoa rai kwa wale wote mliojiandikisha kama Wapiga Kura katuka Jimbo na Kata zinazofanya Uchaguzi kesho tarehe 15 Novemba, 2015 kujitokeza kwenye vituo walikojiandikisha ili kuweza kupiga kura na kuwachagua viongozi wanaowataka bila hofu, woga, wasiwasi au ushawishi. Kura ni haki yako na ni kwa mustakabali wako na nchi yetu.
Ndugu Wananchi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwakumbusha Wapiga Kura
wote mambo yafuatayo:-
(i)     Vituo vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni. Iwapo wakati wa kufunga Kituo watakuwepo Wapiga Kura katika mstari ambao wamefika kabla ya wakati wa kufunga Kituo na hawajapiga Kura, hao wataruhusiwa Kupiga Kura. Mtu yeyote hataruhusiwa kujiunga katika mstari wa Wapiga Kura baada ya saa kumi (10:00) jioni.
(ii)  Mpiga Kura akumbuke kubeba Kadi yake ya Mpiga Kura.
Sheria inaelekeza kuwa ili Mpiga Kura aruhusiwe kupiga kura ni lazima awe na kadi ya kupigia Kura. Fomu Na. 17 sio mbadala wa Kadi ya Mpiga Kura. Fomu hii ni kwa ajili ya Mpiga Kura mwenye Kadi ya Mpiga Kura kutoa Tamko kuthibitisha ndiye mwenye jina linaloonekana kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kwamba bado hajapiga kura katika kituo hicho au mahali pengine.
(iii)    Kipaumbele kitatolewa kwa wagonjwa, wanaoishi na ulemavu wa aina mbalimbali, wanawake wajawazito au wenye watoto wachanga na wazee ambao hawatatakiwa kujipanga kwenye mstari.
(iv)    Wakati wote wa Kupiga Kura na Kuhesabu Kura, Mawakala wa Vyama vya Siasa wawepo kwenye Vituo. Wajibu wao ni kulinda maslahi ya Vyama vyao na Wagombea. Hata hivyo hawatakiwi kuingilia masuala ya utendaji ambayo yamekabidhiwa kwa Msimamizi wa Kituo.
(v)       Kura zitahesabiwa katika Kituo cha Kupigia Kura mara tu Upigaji Kura utakapokamilika. Baada ya Kura kuhesabiwa, Matokeo yatajazwa kwenye Fomu za Matokeo ya Uchaguzi, 21B kwa uchaguzi wa Mbunge na 21C kwa Kata zinazofanya Uchaguzi wa Diwani. Fomu hizo zitatiwa saini na Msimamizi wa Kituo na Mawakala. Kila Wakala atapewa nakala za Fomu za Matokeo ya Uchaguzi wa Mbunge na Madiwani na nakala nyingine zitabandikwa mahali pa wazi nje ya Kituo.
(vi)    Msimamizi wa Kituo/Msimamizi Msaidizi wa Kituo atapeleka Fomu za Matokeo ya Uchaguzi na vifaa vingine vilivyotumika kwenye zoezi la Upigaji Kura kwa Msimamizi wa Uchaguzi/Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi. Wakala wa kila Chama na mlinzi wa Kituo watakaokuwa popote msafara unapoanzia wataruhusiwa kusindikiza msafara wa kupeleka matokeo ya Uchaguzi kwenda kwa Msimamizi wa Uchaguzi/Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata.
(vii) Matokeo yote yakishapokelewa na Msimamizi wa Uchaguzi kwa upande wa Uchaguzi wa Wabunge na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi kwa upande wa Uchaguzi wa Udiwani, yatajumlishwa mbele ya Mawakala na wote wanaoruhusiwa kuingia kwenye vituo vya Kujumlishia Kura.
(viii)        Kama ilivyokuwa wakati wa kuhesabu Kura, baada ya ujumlishaji kukamilika, Fomu Na. 24B Kwa Ubunge na 24C kwa Udiwani  za Matokeo ya Uchaguzi zitatiwa saini na Msimamizi wa Uchaguzi na Mawakala watakaokuwepo. Mawakala watapewa Nakala za Fomu za Matokeo na Nakala moja moja itawekwa mahali pa wazi nje ya Kituo cha Kujumlisha Kura.
(ix)              Matokeo ya Uchaguzi wa Mbunge yatatangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo mara tu baada ya kazi ya kujumlisha Kura kukamilika.
(x)                 Matokeo ya Uchaguzi wa Diwani yatatangazwa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya mara tu baada ya kazi ya kujumlisha Kura kukamilika.
(xi)              Tume pekee ndiyo yenye mamlaka Kisheria ya kumtangaza Mshindi wa Kiti cha Ubunge na Kiti cha Diwani kupitia Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo au Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata.
Ndugu Wananchi
Tume inapenda kusisitiza mambo muhimu yafuatayo:-
(i)               Mawakala wa Vyama vya Siasa wanaruhusiwa kuwepo Vituoni
kwa mujibu wa Sheria na kanuni, Wakala asiyekuwa na barua ya utambulisho kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi hataruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia, kuhesabia na kujumlishia Kura.
(ii)  Vyama vyote vya Siasa vinavyoshiriki katika Uchaguzi vinatakiwa kuhakikisha kwamba vinaweka Mawakala wake katika vituo vyote vya Kupigia Kura na Kujumlisha Kura. Mawakala hao watatakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa.
(iii)                        Mara baada ya Kupiga Kura na kwa kuzingatia Maadili ya Uchaguzi ya 2015 yaliyokubaliwa na Vyama vyote vya Siasa na kuridhiwa na Mahakama, Wapiga Kura wanatakiwa kuondoka Vituoni na kuendelea na shughuli zao. Vituoni Vyama vya Siasa vimeweka Mawakala wake ambao watalinda maslahi ya Vyama husika na Wagombea wao.
(iv)                        Mpiga Kura atapiga Kura kwenye Kituo alichojiandikisha au alichopangiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
(v)   Watu waliotajwa kwenye Sheria ndiyo pekee wanaoruhusiwa kuingia kwenye Vituo vya Kupigia, kuhesabia na kujumlishia Kura.
(vi)                        Mpiga Kura anayeishi na ulemavu wa kutoona ataruhusiwa kuja kituoni na mtu anayemchagua mwenyewe. Aidha, kwa Wapiga Kura wa aina hii ambao watataka Kupiga Kura zao wao wenyewe watapatiwa kifaa maalum cha Nukta Nundu (Tactile Ballot Folder). Vifaa hivyo vitakuwepo katika vituo vyote vya kupigia Kura.
(vii)            Ni kosa la jinai Mpiga Kura Kupiga Kura zaidi ya mara moja.
(viii)        Mpiga Kura ambaye atakuwa na kadi ya Mpiga Kura ila namba ya Kadi yake ni tofauti na namba iliyo kwenye Daftari la Kituo ataruhusiwa kupiga Kura.
(ix)     Wapiga Kura ambao picha zao hazionekani vizuri au hazionekani kabisa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wataruhusiwa kupiga Kura.
(x)        Wapiga Kura walioandikishwa na Tume na wanaishi katika maeneo mapya ya kiutawala yaliyogawanywa wakati au baada ya zoezi la uandikishaji kukamilika, hivyo, majina ya maeneo hayo kutofautiana na majina yaliyopo kwenye kadi zao wataruhusiwa Kupiga Kura.
(xi)     Wapiga Kura ambao wana Kadi za Kupigia Kura na majina yao hayapo katika Daftari la Kituo walichojiandikishia lakini yapo katika Orodha ya majina ambayo haina picha iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi wataruhusiwa Kupiga Kura.
(xii)  Kwa mujibu wa Sheria, Mpiga Kura ni lazima awe na kadi ya kupigia Kura ndiyo aruhusiwe kupiga kura. Hivyo, Mpiga kura asiye na Kadi ya Kupigia Kura hataruhusiwa kupiga Kura.
(xiii)                        Wapiga Kura ambao wana kadi ya kupigia kura, lakini hawamo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kituoni Hawataruhusiwa kupiga Kura.
(xiv)                        Ni marufuku, na ni kosa la jinai kumkataza mtu kwenda Kupiga Kura.
(xv)   Katika Uchaguzi wa Mbunge mwenye mamlaka ya kumtangaza Mshindi ni Msimamizi wa Uchaguzi. Kwa Uchaguzi wa Madiwani mwenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi.

Ndugu Wananchi,
Kwa kumalizia, Tume inawasihi tena Wapiga Kura wote kwenye maeneo yanayopiga kura kesho tarehe 15 Novemba, 2015 kujitokeza kwa wingi Kupiga Kura ili kuwachagua Viongozi mnaowataka wawaongoze kwa miaka mitano ijayo.
Tume inapenda kuwahakikishia Wananchi wote kwamba kutakuwa
na ulinzi wa kutosha katika Vituo vya Kupigia Kura.
Ni matumaini ya Tume kuwa hali ya Amani na Utulivu ambayo imekuwepo wakwati wa uchaguzi tarehe 25 Oktoba, itaendelea kudumishwa ili kuhakikisha kwamba Uchaguzi unafanyika kwa Utulivu na Amani kwa Ustawi wa Taifa letu. Kila Mwananchi, Viongozi wa Dini na Vyama vya Siasa tushirikiane wote ili kuhakikisha kuwa viashiria vya uvunjifu wa Amani na Utulivu vinaepukwa katika hali ya Amani na Utulivu, Uchaguzi utakaofanyika utakuwa Huru, Wazi na wa Haki.

KUMBUKA KUPIGA KURA NI HAKI YAKO YA MSINGI NA
MUSTAKABALI WA NCHI NENDA KAPIGE KURA.
MUNGU IBARIKI AFRIKA MUNGU IBARIKI TANZANIA


Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog