Jana November 27 2015 Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa
aliendelea na majukumu yake kwa kufanya ziara ya ghafla bandarini Dar
na kukutana na mambo ambayo yalimkwaza ikiwemo upotevu wa makontena
zaidi ya 340 pamoja na ubadhirifu… akaamrisha watu watano wasimamishwe
kazi na uchunguzi uendelee juu yao.
Muda mfupi baadaye jana hiyohiyo ikatoka taarifa Ikulu kwamba na Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade nae amesimamishwa kazi… leo nina taarifa nyingine kuhusu wengine watatu kusimamishwa kutoka hapohapo Mamlaka ya Mapato TRA.
Majina ya waliosimamishwa leo Anangisye Mtafya, Nsajigwa Mwandengele na Robert Nyoni… agizo la kusimamishwa kwao limetoka kwa Waziri Mkuu ambae amenukuliwa na blog ya Issa Michuzi kuhusu uamuzi huo >>> “Kazi
ya kuwachunguza ilianza jana ileile na sasa tumeona hawa watu wanapaswa
kuwa nje ya utumishi ili kupisha uchunguzi ufanyike kwa uhuru zaidi” >>> Waziri Mkuu Majaliwa.
Hii taarifa nimeitoa kwenye Blog ya Issa Michuzi.
Mpaka sasa jumla ya watumishi tisa
wamesimamishwa na agizo la Serikali ni kwamba hawatoruhusiwa kusafiri
nje ya nchi mpaka uchunguzi juu yao utakapokamilika.
0 comments:
Post a Comment