Home » » Ni kazi mpaka Jumamosi !! Waziri Mkuu Majaliwa kawasimamisha kazi wengine watatu TRA

Ni kazi mpaka Jumamosi !! Waziri Mkuu Majaliwa kawasimamisha kazi wengine watatu TRA




Jana November 27 2015 Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa aliendelea na majukumu yake kwa kufanya ziara ya ghafla bandarini Dar na kukutana na mambo ambayo yalimkwaza ikiwemo upotevu wa makontena zaidi ya 340 pamoja na ubadhirifu… akaamrisha watu watano wasimamishwe kazi na uchunguzi uendelee juu yao.
Hii ilikuwa jana, Kikao cha waziri Mkuu Majaliwa pamoja na Maafisa wa TRA na TPA
Hii ilikuwa jana, Kikao cha Waziri Mkuu Majaliwa pamoja na Maafisa wa TRA na TPA
Muda mfupi baadaye jana hiyohiyo ikatoka taarifa Ikulu kwamba na Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade nae amesimamishwa kazi… leo nina taarifa nyingine kuhusu wengine watatu kusimamishwa kutoka hapohapo Mamlaka ya Mapato TRA.
Majina ya waliosimamishwa leo Anangisye Mtafya, Nsajigwa Mwandengele na Robert Nyoni… agizo la kusimamishwa kwao limetoka kwa Waziri Mkuu ambae amenukuliwa na blog ya Issa Michuzi kuhusu uamuzi huo >>> “Kazi ya kuwachunguza ilianza jana ileile na sasa tumeona hawa watu wanapaswa kuwa nje ya utumishi ili kupisha uchunguzi ufanyike kwa uhuru zaidi” >>> Waziri Mkuu Majaliwa.
Hii taarifa nimeitoa kwenye Blog ya Issa Michuzi.
MAJALIWA BOY
Mpaka sasa jumla ya watumishi tisa wamesimamishwa na agizo la Serikali ni kwamba hawatoruhusiwa kusafiri nje ya nchi mpaka uchunguzi juu yao utakapokamilika.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog