Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,mchana wa Alhamisi hii Limempitisha Kassim Majaliwa kuwa Waziri mkuu mpya.
Kuthibitishwa kwa uteuzi wake kumetokana na kura za ndio na hapana zilizopigwa na wabunge.
Mh.
Majaliwa amethibitishwa na wabunge kuwa Waziri Mkuu mteule kwa kupata
kura za ndio 258 sawa na asilimia 73.5% ya kura zote 351 zilizopigwa.
Kura za hapana ni kura 91 sawa na asimilia 25 ya kura zote, na kura zilizoharibika ni 2.
Majaliwa amemshukuru Rais Magufuli kwa kumwamini na ameahidi kuwatumikia watanzania wote bila kujali itikadi zao za vyama.
0 comments:
Post a Comment