Jeshi la polisi mkoani iringa limewatahadharisha wananchi kuwa
makini ili kuepukana na matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha.
Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa polisi mkoa wa iringa RPC RAMADHANI
ATHUMANI MUNGI alipokuwa akizingumza na nuru fm juu ya kuzuia unyang’anyi wa
kutumia silaha kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka.
Aidha kamanda MUNGI ameyataja na kuyatahadharisha baadhi ya maeneo
kuwa makini na vitendo vya unyang’anyi wa kutumia silaha ni pamoja na kwenye
mabenki, na maduka ya kubadilisha fedha.
Akizungumzia namna ya kuepukana na matukio hayo kamanda mungi amesema
kuwa ni pamoja na wafanyabiashara kupeleke benki na kuacha kukaa nazo majumbani
mwao.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment