Home » » CHUO KIKUU CHA IRINGA CHAFANYA MAHAFALI YA 18 CHAJIVUNIA KUPAA KITAALUMA.

CHUO KIKUU CHA IRINGA CHAFANYA MAHAFALI YA 18 CHAJIVUNIA KUPAA KITAALUMA.





Hivyo  aliwataka  wahitimu  wa  chuo  hicho  kuendelea  kutoa  ushirikiano kwa chuo  hicho na  pale  michango yao  inapohitajika kwa ajili ya  kuendeleza  ujenzi  wa majengo  ya  chuo  hicho  kutoa ushirikiano  wao.
Huku makamu  mkuu  wa  chuo hicho  Prof Joshua Mwadumulla alisema  wakati  chuo  hicho  kinasherekea  mahafali haya ya 18  toka  kuanzishwa  kwake  bado wanatambue kuwa kumekua na ushindani mkubwa katika uga wa elimu ya juu kutokana na kuweko kwa ongezeko kubwa la vyuo vikuu katika Tanzania
“….Mwanzoni mwa miaka ya 70,kulikua na chuo kikuu cha Dar es salaam peke yake kikiwa na matawi mawili ambayo ni muhimbili na sokoine….leo hii baada ya miaka 40 tunazungumzia idadi inayokaribia 60 ya vyuo vikuu katika Tanzania….lakini idadi ya wanafunzi inayotakiwa kudahiliwa na vyup hivyo haijaongezekea sana….ndiyo maana kumekua na uhaba wa udahili wa wanafunzi….Uhaba huo umesababisha ushindani kubwa wa mahitaji ya wanafunzi…ndiyo maana kuna haja ya chuo kikuu cha Iringa kuwa  na mikakati mizuri ya kuongeza udahili kwa wanafunzi”
Akizungumzia mikakati hiyo  Prof Mwadumulla alisema kuwa wanajitahidi kuanzisha program  ambazo zina upekee Fulani ili kuweza kuanza kuachana na mfumo wa kijadi ya kuigana katika biashara Fulani ambazo mtu humuona mtu mwingine akifanikiwa kupitia biashara hiyo kutokana na biashara ya namna hiyo kuwa na faida kwa mazoea na kufahamiana na si kwa upekee na ubora.
Program nyingine zilizoanzishwa na chuo hiko ili kupambana na tatizo la ajira nchini Prof.Mwadumulla alisema kuwa wana program inayoitwa Team Academy yaani academia shirikishi inayomtaka mwanafunzi asome kwa vitendo zaidi tena kwa ubunifu kupitia nadharia ya darasani kuliko kuwa kasuku wa uradidi wa nadharia.
Aidha Prof.Mwadumulla aliwataka wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu waliohitimu hii leo kuwa na nyongeza ya elimu yenye tija na mafanikio waendapo makazini lakini pia akawataka kuwa na upendo,uvumilivu,subira,umakini na weledi huku wakikumbuka kuwa kauli mbiu ya serikali ya tano inayooongozwa na Dr John Pombe Magufuli kuwa ni “HAPA KAZI TU”.               



Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog