Home » » Obama amevuta sana sigara, ndani ya White House je? Jibu hili hapa..

Obama amevuta sana sigara, ndani ya White House je? Jibu hili hapa..

Rais Barack Obama anakaribia kumaliza muhula wake wa pili kuiongoza Marekani tangu mwaka 2008, lakini kuna tabia yake aliyokuwa nayo muda mrefu ya kuvuta sigara… alipoingia White House aliendelea kuvuta?
Obama alihojiwa na kwenye sentensi za kwanza kajibu hivi >>> “Sijavuta sigara hata moja ndani ya miaka mitano tangu nimeingia Ikulu… Niliahidi kwamba Muswada wa Sheria mpya ya Afya ukipita (2010) sivuti tena sigara, na kweli imetimia“.
Obama anasema alijaribu mara kadhaa kuachana na sigara mwaka 2008 wakati wa Kampeni  za Urais lakini ilishindikana, kuna wakati alijikuta akijibana zake kona na kuvuta tena na tena !!
Unajua kingine alichojibu Rais Obama kuhusu kuacha kuvuta sigara >>> ‘Namuogopa mke wangu’… Michelle kumbe nae hakuipenda tabia ya uvutaji sigara ya Obama iendelee !!
Barack-and-Michelle-barack-obama-2739161-690-458
Achana na hayo, swali jingine la kizushi kwa Obama… akiwa zake ‘out’ na Michelle wake wanakula raha, simu ya nani anaweza kupokea ikiita? >>> “Mmmmh… labda ya Malia, Sasha (watoto wake) na mama mkwe.. nyingine ya mshauri wangu wa usalama Susan Rice, na Katibu Mkuu Kiongozi,  Denis McDonough” >>> Barack Obama.
Basi hayo ndio majibu ya Rais Obama, kuna kitu hukutegemea kwamba angekijibu kwenye hayo?
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog