Home »
» WAISLAMU WAMTAKA JPM KUZINGATIA UTAWALA BORA NA USAWA
Kiongozi Mwandamizi wa dhehebu la
Kiislamu la Shia Ithnashery nchini Tanzania Imamu Swadiq Sheikh Hemed
Jalala ameitaka Serikali ya awamu ya tano kuzingatia utawala bora na
kuweka usawa baina ya wananchi bila ya kuangalia tofauti zao ili kwa
pamoja waeze kujiletea maendeleo.Sheikh
Jalala ameitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya
kuzaliwa kwa Mrithi wa Mtume Muhamad Imam Ali ambae alikufa miaka elfu
moja na 30 iliyopita lakini anakumbukwa kwa utawala wake wa kuzingatia
usawa kwa binaadamu.
Aidha Sheik Jalala amesema kuwa Utawala
bora hauwezi kupatikana kama hakutakuwa na utulivu na amani katika nchi
hivyo serikali ya awamu ya tano isimamie kikamilifu suala la amani na
utulivu ili wananchi waweze kufanya kazi kwa bidii.
0 comments:
Post a Comment