Home » » KUTOKA BUNGENI: SERIKALI YAPANDISHA PENSHENI KWA 100%

KUTOKA BUNGENI: SERIKALI YAPANDISHA PENSHENI KWA 100%

KIWANGO cha pensheni kwa wastaafu walio kwenye mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii waliokuwa wakilipwa kima cha chini Sh 50,115 kinatarajiwa kuongezwa kwa asilimia 100 hadi Sh 100,125.

Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji alisema jana bungeni kwamba, wastaafu hao wataanza kulipwa kiwango hicho kipya pamoja na malimbikizo yao baada ya utaratibu unaoandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Mifuko hiyo (SSRA) kukamilika.MISHAHARA

Kijaji alisema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Conchester Rwamlaza (Chadema), aliyetaka kufahamu ni lini wastaafu wataanza kulipwa fedha hizo. Mbunge huyo alisema tangu bajeti inayoisha ya mwaka 2015/16, serikali kupitia wizara ya fedha iliahidi kupandisha pensheni kwa wastaafu wanaolipwa Sh 50,000 ili walipwe 100,000.

Alisema ahadi sasa, haijatekelezwa kwa wastaafu hao, jambo linaloleta usumbufu na wao kushindwa kufahamu ni lini wataanza kulipwa fedha hizo. Naibu Waziri Fedha na Mipango, Kijaji, alikiri kwamba wastaafu wote kwenye mifuko wanaolipwa kima cha chini cha pensheni cha Sh 50,000 kuanzia Julai ,2015 walipaswa kulipwa kima kipya.

“Ni kweli serikali ilitekeleza ahadi ya kuongeza kima cha chini cha pensheni kufikia 100,125.85 kutoka Sh 50,114.43, tangu agizo hilo lilipotolewa Julai mwaka jana ni Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) pekee ndio ulioanza kutekeleza agizo hilo kuanzia Julai mwaka jana,” alisema.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog