Home »
» GARI LAZAMA BAHARINI “KIVUKONI”
Alfajiri ya leo gari aina ya Coaster
lililokuwa katika foleni ya kuingia katika kivuko upande wa Posta
kuelekea Kigamboni lilizama katika Bahari eneo la Kivukoni.
Mashuhuda wa ajali hiyo wanaeleza chanzo
cha gari hiyo kuingia na kuzama baharini kimetokana na kile
kinachodaiwa kufeli kwa breki wakati dereva wa gari hiyo akikata kona
kuelekea upande wa mbele ambapo gari zenye uharaka zinapewa nafasi kukaa
mbele pindi kivuko kitakapofika ziwe za kwanza kuingia katika kivuko
hicho.
Mashuhuda wanasema gari hilo lilipewa
kipaumbele kwani inasemekana lilikuwa limebeba waombolezaji waliokuwa
wakienda msibani upande wa Kigamboni.
Taarifa zaidi zinasema wakati dereva wa
gari hilo akitafuta namna ya kuegesha (kupaki) gari hilo ndipo gari hiyo
ilipofeli breki na kuzama Baharini.
Hadi kufikia hivi sasa juhudi za uokoaji zinaendelea huku baadhi yao wakiwa wameshapoteza maisha.
0 comments:
Post a Comment