Bodi
ya Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF) iliyokaa Ijumaa Aprili 22, 2016
jijini Dar es Salaam pamoja na mambo mengine ilijadili hali ya mwenendo
wa tasnia ya habari nchini hasa juu ya haki ya wananchi kupata habari.
Katika
kujadili hali hiyo, TEF imeguswa kwa namba ya kipekee kabisa na
mwenendo mzima wa urushaji wa bahari za Bunge kwa njia ya redio na
luninga, hususan katika mkutano wa tatu wa Bunge la 11 unaoendelea mjini
Dodoma kwa sasa.
Itakumbukwa
kwamba Muhimili wa Bunge kupitia Kitengo chake cha Habari, Elimu na
Mawasiliano, Aprili 15 2016 ulitoa taarifa kwa umma ikieleza utaratibu
mpya ambao sasa umeanza kutumika katika kurusha matangazo ya redio na
luninga kutoka Bungeni.
Katika
taarifa hiyo, Ofisi ya Bunge ilisema kuwa imeamua kuboresha mfumo wa
urushaji wa Matangazo ya Bunge kwa Bunge lenyewe kurusha Matangazo ya
Vikao vyake pamoja na Vipindi mbalimbali vyenye Maudhui kuhusu Shughuli
za Bunge ambazo hazijapata fursa ya kufahamika vyema kwa umma kuanzia
katika Mkutano wa Bunge la Bajeti unaoendelea sasa.
Ofisi
hiyo ilisema kuwa mfumo huo mpya ni Utamaduni wa kawaida kwa kila Bunge
hususani Mabunge ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola kuwa na Studio
zake kwa lengo la kurusha Matangazo ili yawafikie wadau kwa lengo la
kurusha kupitia vituo vyao. Kwa maana hiyo, Bunge lilisisitiza kuwa
chini ya utaratibu huo mpya, jukumu la kurusha Matangzo ya Vikao vya
Bunge litafanywa na Bunge lenyewe kupitia FEED MAALUM ili kurahisisha
kila Kituo cha Radio na Televisheni kupata Matangazo hayo kwa sehemu
walipo bila kufunga Mitambo yao Bungeni Dodoma.
Katika
kutekeleza uamuzi huo na mfumo huo mpya, kila kituo cha Televisheni na
Redio sasa watatumia Masafa ya Matangazo ya Bunge (Frequencies) bure
kupitia FEED MAALUM itakayorushwa na Satellite ya INTELSAT 17 ambayo iko
nyuzi 66 Mashariki kwa masafa maalum ambayo pia yaliwekwa wazi.
Kwa
mantiki hiyo, Bunge sasa limezuia vituo vyote vya televisheni nchini
kupeleka kamera zake ndani ya Bunge kwa kuwa habari hizo zitapatikana
kwenye feed maalum ambayo ni ya Bunge ambayo inasimamiwa na waandishi wa
Bunge ambao pia ndio wanaamua nini kionyeshwe kwa utashi wao.
Baada ya kutafakari hatua hizi mpya za Bunge na baada ya kufuatilia kile kinachorushwa, mambo kadhaa yamethibitika:-
0 comments:
Post a Comment