Home » » Sababu za bandari ya Tanga kuteuliwa kutumiwa na Bomba la mafuta kutoka Uganda

Sababu za bandari ya Tanga kuteuliwa kutumiwa na Bomba la mafuta kutoka Uganda


Serikali ya Uganda imetangaza rasmi uamuzi wa kutumia bandari ya Tanga baada ya kuwepo na ushindani na bandari za Lamu na Mombasa za nchini Kenya. Bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima katika Ziwa Albert nchini Uganda litapita katika ardhi ya Tanzania kwenda Bandari ya Tanga ambako ndiko meli kubwa za mafuta, zitakapotia nanga kubeba mafuta hayo kwenda sehemu mbalimbali duniani.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo April 24 2016 amewasili Tanzania akitokea Uganda alipokwenda kwenye mkutano wa majadiliano ya bomba hilo la mafuta lipite wapi kati ya Tanzania au Kenya. Akizungumza baada ya kuwasili Prof. Muhongo ameeleza sababu zilizofanya Bandari ya Tanga kuchaguliwa ambapo ushindani ulikuwa ni wa ubora wa bandari na ubora wa njia ambako bomba litapita……….
>>>’Tanga ni bora kwa sababu ina kina kirefu kulinganisha na bandari za mombasa na Lamu, Bandari ya Tanga ina kina cha zaidi ya mita 23 ambayo kimataifa inatakiwa ili meli kubwa inayokuja kuchukua shehena ya mafuta iweze kutia nanga na kupakia mafuta nakuondoka, tumewapiku wenzetu kwa kina, na pili bandari yetu inaweza kufanya kazi kwa siku zote za mwaka yaani siku 365′:-Profesa Sospeter Muhongo
Bomba hilo litaingilia Mkoa wa Kagera kutoka nchini Uganda na kupita katika mikoa ya Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma hadi Bandari ya Tanga. Bomba hilo linatarajiwa kukamilika mwaka 2020 katikati.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog