
Katibu mkuu wa itikadi na uenezi CCM, Nape Nnauye akizungumza na wana habari.
Walioteuliwa kugombea nafasi hiyo na kamati kuu iliyofanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni pamoja na naibu spika aliyemaliza muda wake Job Ndugai, Dkt. Tuliana Ackson na Abdullah Mwinyi.
Wana-CCM hao watatu watapigiwa kura wakati wa kikao cha kamati ya wabunge wote wa CCM kitakachofanyika kesho Novemba 16, 2015 saa nne asubuhi katika ofisi za makao makuu ya CCM Dodoma ili kuchagua jina moja kugombea nafasi hiyo katika bunge la jamhuri ya muungano.
Katibu mkuu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM), Nape Nnauye ameyazungumza haya>>
“Ibara ya 57, Kanuni za kamati ya wabunge wote wa CCM toleo la 2010 toleo la nne 2011, mbunge yeyote anayetaka kugombea nafasi ya naibu spika atatakiwa kuchukua fomu kupitia kamati hiyo na atairudisha kisha kamati itakaa kupata jina moja,”
”Kwa mujibu wa maelezo hayo mbunge wa chama hicho anayetaka kugombea unaibu spika, atatakiwa kuchukua fomu leo Novemba 15, kwa ada ya Sh 100,000 kisha atairudisha kesho Novemba 16, ndipo kamati itakaa kuchambua na kupitisha jina moja” ,- Nape Nnauye
0 comments:
Post a Comment