Tukio la kikatili na la kinyama limetokea katika kijiji cha kinyika pawaga wilaya ya iringa ambapo mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la melina kisogonze amemtupa chooni mwanae wa kumzaa wa siku moja baada ya kujifungua.
Akizungumza bibi afya wa kijiji hicho bi. tamasha amesemakuwa walipokea taarifa kutoka kwa wanainchi waliokwenda chooni kuhusu kelele za mtoto zilizotoka chooni kisha kumwita mwenyekiti na kufanikia kumtoa mtoto huyo ambaye kwa sasa anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa iringa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho bwana sulemani mbwawa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tukio hilo ni la kwanza kutokea kijijini kwake na ametoa wito kwa wanainchi kuwa makini na watu wanakuwa wajawazito kwa kuwa karibu nao.
0 comments:
Post a Comment