Home » » Kesi ya shekhe Ponda yaanza kusikilizwa chini ya Ulinzi mkali

Kesi ya shekhe Ponda yaanza kusikilizwa chini ya Ulinzi mkali


Kesi inayomkabili kiongozi wa jumuiya na taasisi ya kiislamu nchini Sheikh Ponda Issa Ponda imeanza kusikilizwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro huku jeshi la polisi likilazimika kuwadhibiti wafuasi wa shekhe Ponda nje ya uzio wa mahakama.
 
Shahidi wa kwanza katika kesi hiyo ni aliyekuwa mkuu wa polisi wilaya ya Morogoro (OCD) Sadick Tindwa ambaye kwa sasa ni OCD wilaya ya Handeni mkoani Tanga ametoa ushahidi wake kwa zaidi ya saa mbili ambapo ameieleza mahakama kuwa julai 31 mwaka 2013 akiwa OCD wilaya ya Morogoro alipokea barua kutoka kwa umoja wa wahadhiri wa dini ya kiislamu wakiomba kufanya kongamano la siku kuu ya Eid pili walilotaka kufanya katika uwanja wa shule ya msingi kiwanja cha ndege manispaa ya Morogoro Agosti 9 mwaka 2013 ambapo alitoa kibali kwa masharti ya kufanya kongamano hilo kwa kutokutoa  maneno ya kashfa dhidi ya dini nyingine.
  
Aidha amesema katika kongamaono hilo wahadhiri mbalimbali walitoa mada  ambapo msemaji wa mwisho alikuwa ni mshtakiwa Ponda Issa Ponda na wakati akiendelea kuzungumza alitoa maneno yenye mitazamo ya uchochezi, kashfa na kuumiza imani za dini nyingine ambapo amesema serikali ilipeleka majeshi kwa wananchi wa Mtwara wakati walikuwa wakidai haki yao kwenye gesi lakini kwa kuwa asilimia kubwa ya wananchi wa Mtwara ni wasilaaam lakini  serikali ilishindwa kupeleka majeshi kwenye mgogoro wa loliondo kwa sababu  asilimia kubwa ya wananchi wa lolindo ni wakaristu.
  
Uchochezi mwingine umedaiwa kuwa shekhe Ponda aliwaambia waumini wa kiisalaam wasiunge mkono kamati za ulinzi na usalama za dini kwani zimeundwa na Bakwata pamoja na serikali kwa manufaa yao binafsi, hivyo kamati hizo zikifika katika misikiti na kujitambulisha wafunge milango na madirisha kisha wawapige. 
 
Upande wa utetezi wenye mawakili watatu akiwemo wakili Juma Nasoro, Batheromeo Tarimo na Abubakar Salimu wameuliza maswali ya msingi ambayo ni: Je nafasi gani aliyokuwa nayo sheikh Ponda katika kongamano hilo?, kuna uhusiano gani kati ya mashtaka aliyofunguliwa sheikh Ponda na maneno aliyotoa kwenye kongamano?, kongamano lilikuwa halali ama sio halali?, mbali na jamhuri  je ni  dini gani iliwahi kulalamikia kuumizwa na maneno aliyotoa sheikh Ponda siku ya kongamanona ?
 
Kesi hiyo imeahiriswa na itaendelea kusikilizwa tena jan 27 mwaka huu katika mahakama ya hakim mkazi mkoani Morogoro.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog