Home » »

Waziri Mkuu kufungua majadiliano ya Serikali za Mitaa za Tanzania na China

 

Baadhi ya ujumbe wa watu wapatao zaidi ya 70 kutoka Serikali za Mitaa wakiaangalia mchoro wa ramani ya Tanzania ili kuelewa maeneo mbalimbali leo katika Makumbusho ya Taifa jiji Dares Salaam.

Naibu Gavana wa Jimbo la  Shandong , Xia  Geng akiangalia picha ya  mbalimbali za baba wa taifa hayati Mwalimu Julius  K. Nyerere katika Makumbusho ya Taifa  ikiwemo ya kuwekwa wakfu  kuwa  Rais wa Kwanza  wa Tanzania  mwaka 1962 leo jijini Dares Salaam.

Baadhi ya ujumbe  wa ya ujumbe wa watu wapatao zaidi ya 70 kutoka Serikali za Mitaa  China  wakiaangalia moja ya behewa la  Reli ya Tanzania na Zambia  leo  mara baada ya kuetembelea ofisi ya makao makuu ya reli hiyo jijini Dares Salaam.


Baadhi ya ujumbe   wa watu wapatao zaidi ya 70 kutoka Serikali za Mitaa  China  wakiaangalia picha za viongozi mbalimbali wa nchi hizo kwenye  makao makuu ya ofisi ya  Reli ya Tanzania na Zambia jijini Dares Salaam.
Naibu Gavana wa Jimbo la  Shandong , Xia  Geng( kulia) akimkabidhileo  zawadi ya kuonesha upendo  Afisa Masoko ya  Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia(TAZARA), Michael Myange (katikati) na kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Polisi cha TAZARA, Bakari Makuka mara ya kutembelea  ofisi ya makao makuu ya reli hiyo jijini Dares Salaam.
Naibu Gavana wa Jimbo la  Shandong , Xia  Geng( kushoto)akionesha moja ya tisheti zinazotengenezwa nchini kutipia mwekezaji kutoka nchi hiyo kwenye Mamlaka ya Ukanda Maalum waUwekezaji Tanzania (EPZA)  leo  mara baada ya  kutembelea eneo hilo jijini  Dares Salaam.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda kesho anatarajiwa kuwa mgenio rasmi katika  mkutano wa majadiliano wa ushirikiano wa Serikali za Mitaa za China  na Tanzania utakaofanyia katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa  Mwalimu  J.K. Nyerere jijini Dares Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari ilitotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI imeeleza kwamba  mkutno huo ni miongoni mwa mambo yatakayofanywa katika ziara ya wajumbe wa watu wapatao 70 kutoka   Serikali za Mitaa kutoka China, wakiwemo magavana,mameya na wafanyabiashara ambao wamewasilini nchini tangu jana ikiwa ni mikakati ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali za  Mitaa za Tanzania na China.
“ Ujio wa wageni hawa unafungua ukurasa mpya wa urafiki na kusaidia kuleta maendeleo na utoaji wa huduma nzuri kwa jamii  na kiuchumi,” ilisema taarifa hiyo.
Ujumbe huo pia utakutana na baadhi ya Mawaziri wa Sekta mbalimbali, Wakuu wa Mikoa,  Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa.
Wengine watakaokutana nao ni baadhi ya Mameya/Wenyeviti wa Halmashauri za Jiji, Manispaa, Miji na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri,Taasisi za Serikali na Binafsi  pamoja na Wafanyabiashara.
Wakati huohuo Serikali ya China imesema iko tayari kushirikiana na Tanzania kuboresha miundombinu ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) ili kuweza kukuza shughuli za kiuchumi na kijamii.
Kauli hiyo  imetolewa leo na  Makamu wa Rais wa Umoja wa  Wachina  wenye Urafiki na nchi za Nje, Feng  Zuoku mara baada ya ujumbe huo kutembelea ,  reli hiyo , Makumbusho ya  Taifa na Mamlaka ya Ukanda Maalum waUwekezaji Tanzania (EPZA) jijini Dares Salaam.
Tumejifunza mengi katika ziara hii.Tutaendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya miundombinu, biashara na uchumi,” alisema  Rais huyo.
Aliongeza kuwa  waomeona miundombinu ya EPZ  ni mizuri hivyo wawakezaji kutoka nchi hiyo  wako tayari kuja kuwekeza.
Akizungumzia kuhusu Makubusho ya Taifa alisema wamejinza mambo mengi ya historia ya Tanzania  ambayo inafanana na China.
Rais huyo aliwapongeza Watazania kwa ukarimu wanaouonesha kwao , hivyo wanategemea baada ya ziara hivyo ushirikino huo utaingia katika sura mpya.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog