Home » »

CHRISTINA SHUSHO ALIVYOWEKA MAMBO SAWA CCC JUMAPILI

Siku ya jumapili tarehe 24 November, 2013 katika Ukumbi wa Kanisa la CCC Upanga Mwanamuziki wa injili aliyejijengea jina katika ukanda wa Afrika Mashariki na Mwanamuziki anayeongoza kwa kutwaa tuzo nyingi kuliko wanamuziki wengine wa injili inchini Tanzania Christina Shusho amefanya Live Recording ya aina yake katika Ukumbi huo.

Live Recording hiyo ilianza majira ya saa 12 ilikuwa nikiwango cha kimataifa na Iliandaliwa kwa ustadi Mkubwa kulinganisha na matamasha mengine ya Injili hapa Tanzania. Christina Shusho katika Nyimbo zake hizo pia alifanya Collabe na wanamuziki wengine wa injili hapa Tanzania kama Upendo Kilahiro pamoja na Joshua Mlelwa. Mgeni rasmi katika Tamasha hili alikuwa Mhe. Bernad Membe waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Waziri hiyo akizungumza katika tamasha hilo alisema ipo haja ya vijana wa kitanzania kumcha Mungu ili kuweza kuja kuwa viongozi wa nyanja mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa hapa Tanzania.

Christina Shusho akiwa sawa stejini.
Christina na Upendo Kilahiro wakiimba pamoja Thamani ya wokovu wangu.
Waitikiaji wa Christina Shusho wakienda sawa.
Mgeni wa heshima mheshimiwa Benard Membe akizungumza na waumini waliofika tamashani.
Christina Shusho akienda sawa na kundi la The Voice.
MC no 2 watukio, unclejimmy temu akienda sawa.
Mpiga Saxaphone nambari One Nchini Uganda Isaiah akihudumu.
Shetani aliipata, maana thamani ya wokovu ilikuwa level nyingine.

Vijana wakisebeneka wakati wa tamasha.
Samuel Yona, aliyeandaa na kuongoza muziki wa mwanamama Christina Shusho.
Upendo Kilahiro na Christina Shusho.
Kamati iliyoandaa tamasha hilo.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog