Home » »

HAYAWI HAYAWI HATIMAYE YANAKUA, NI JUMAPILI HII

Hatimaye kundi la Glorious Worship Team (GWT) linatarajia kuachia DVD yao mpya siku ya jumapili hii katika kanisa la CCC Upanga jijini Dar es salaam. DVD hiyo ambayo ilirekodiwa live mwishoni mwa mwaka juzi katika kanisa hilo, tayari audio yake ilishatoka ikifahamika kwa jina la "Umenifanya Ibada" ambayo imekuwa ikipendwa na wengi kutokana na nyimbo zilizomo, sauti pamoja na mpangilio wa muziki kiujumla.

Uzinduzi huo unaotarajia kusindikizwa na waimbaji kama Miriam Lukindo, The next level team, Upendo Nkone, Florence Mureith kutoka Kenya, Rivers of Joy, Zion band pamoja na kundi la Acapela The Voice, kiingilio katika uzinduzi huo ni shilingi 10,000. Kundi la GWT ambalo limesheheni vijana wenye vipaji mbalimbali katika tasnia ya kumtukuza Mungu hadi kufikia bendi zinazopiga miziki ya kidunia kuwashawishi baadhi ya waimbaji na wapigaji wa kundi hilo kujiunga nao wamekuwa wakigonga mwamba kutokana na msimamo thabiti wa vijana hao katika kumtumikia Mungu.

Kwasasa kundi hilo limekamilika kila idara, uimbaji, upigaji, maombi pamoja na uongozi wake madhubuti kutoka kwa kijana Emanuel Mabisa ambaye alianza kuliongoza jahazi la kundi hilo tangu hawajatoka katika kundi la Glorious Celebration ambako ndiko walitoa album ya kwanza iitwayo Niguse.
Wapigaji wa GWT wakijifua tayari kwa kumtukuza Mungu jumapili.

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog