Home » »

MAVETERANI KENYA NA BARA KUKUMBUSHIA CHALLENGE YA ENZI HIZO, HUO MUZIKI WA HARAMBEE USIUPIMIE, KUNA MAHMOUD ABBAS, PETER DAWO, J J MASIGA, JUA CALI NA KADENGE, STARS…

Na Mahmoud Zubeiry, Nairobi
WACHEZAJI wa zamani wa Kenya ‘Wazee wa Kazi’ wametaja kiksi cha nguvu ambacho kinamenyana na wakongwe wenzao wa Bara kutia nakshi michuano ya mwaka huu ya Challenge.
Kikosi hicho chini ya kocha George Sunguti kina wachezaji 30 ambao waliwika Harambee Stars enzi zao.
Wazee wa Kazi; Wachezaji wa zamani wa Harambee Stars

Kikosi hicho ni; Mohammed Abbas (kipa), John Busolo (kipa), Josphat Murila (beki), George Sunguti (mshambuliaji), Austin Oduor (mshambuliaji), Elly Adero, Sammy Pamzo Omollo (mabeki), Allan Thigo (kiungo), Joe Kadenge (mshambuliaji), Tobias Jua Kali Ochola (beki), Ben Oloo, George Onyango, Wycliffe Anyangu (mabeki), Paul Ochieng’ (beki), Peter Dawo (mshambuliaji), Ben Musuku, Aggrey Lukoye, J.J Masiga (washambuliaji), Paul Onyiera (kiungo), Mike Amwayi, Douglas Matual, Joe Birgen, James Siang’a (makipa), Abdul Baraza, Ricky Solomon, John Bobby Ogola, James Nandwa (washambuliaji), Ambrose Golden Boy Ayoyi, John Nyawaya na David Ochieng’.
Tanzania Bara bado haijataja kikosi chake kitakachokuja Nairobi na hadi jana hakukuwa na taarifa za hata kuanza mazoezi.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog