Home » »

KAMPUNI ya Simba Logistic Equipment Supply yazindua kifaa cha kuzimia moto kwa kurusha kiitwacho B

kifaaa-1 _DSC0036 - Copy-1 _DSC0041 _DSC0054 - CopyKAMPUNI ya Simba Logistic Equipment Supply hivi karibuni ilizindua kifaa cha kuzimia moto kwa kurusha kiitwacho Bonex ambacho vinatumia kuzimia moto katika majumba, magari na sehemu nyinginezo.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya uzinduzi wa vifaa hivyo Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Simba Logistic Equipment Supply Co Limited, Fareed Nahdi alisema kuwa vifaa hivyo ni rahisi kutumika katika matukio mbalimbali ya kuzimia moto.
Alisema kuwa havihitaji matengezo ya mara kwa mara kwa kuwa vikinunuliwa vinatumika kwa mara moja kwa tukio moja.
Alisema kuwa ni vifaa ambavyo ni rahisi kubebeka na kutumika katika mazingira yoyote kutokana na udogo wake ambao unaumuhimu mkubwa katika kuzima moto.
“Hii ni aina mpya ya uzimaji  moto kwa kutumia vifaa hivi muhimu ambapo ukitofautisha na vifaa vingine ambapo kunakuwa kuna maelekezo mengi ya kufuata lakini hiki unarusha tu hivyo hata watoto wanaweza kutumia”alisema Nahdi.
Alisema kuwa hakina madhara kama vile moshi wala aina nyingineyo ya madhara na kinasaidia harakati za uokozi wa wat.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mohamed Mpinga aliyekuwepo kushuhudia uzinduzi huo alisema kuwa kifaa hicho kinaweza kusaidia zaidi hata katika kuzima motoo wa magari.
Alisema kuwa wenye magari wanapaswa kwua na kifa hicho kwa kuwa ni rahisi kutumika pia.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog