UKATILI..!! ALIPULIWA KWA MAFUTA YA MOTO BAADA YA KUKOPA CHIPSI
Nusu kifo! Kijana
aliyefahamika kwa jina la Hanafi Daudi (31), mkazi wa Salasala
Kilimahewa jijini Dar, yupo katika hali tete kufuatia kumwagiwa mafuta
ya moto yaliyokuwa yanakaangia chipsi.Hanafi ambaye amelazwa katika
Hospitali ya Taifa Muhimbili Wodi ya Sewa Haji amesema aliyemchoma moto
ni muuza chipsi ambaye alikwenda kumkopa chipsi.
Hanafi Daudi akiwa na majeraha usoni baada ya kuchomwa na mafuta ya moto.
Alisema tukio hilo
lilijiri Machi 2, mwaka huu, Goba jijini Dar es Salaam ambapo yeye na
wenzake wawili walikuwa wakilinda nyumba ambayo haijakamilika.
MSIKIE MWENYEWE
“Ilikuwa usiku wa saa
3:30 hivi, muda ambao watu walikuwa wanaangalia mpira. Ndipo nilipoamua
kwenda pale kwa lengo la kuomba kukopeshwa chipsi kwa kuwa sikuwa na
pesa muda huo. Niliamini ningemlipa kesho yake.
Akiwa hospitali.
“Nilipofika, yule jamaa
nilimuona kama yuko tofauti hivi lakini nikaamua nimuombe anisaidie kwa
muda ule. Nikashangaa tu akanyanyua karai la mafuta ya chipsi na
kunimwagia usoni.
“Nilihisi
kuchanganyikiwa, nikakimbia mpaka kwa wenzangu. Wakati huo macho yote
yalikuwa yameziba, sioni kitu chochote. Ndipo wenzangu wakanibeba na
kunileta hapa Muhimbili kwa msaada wa usafiri njiani,” alisema Hanafi.
Akionyesha jeraha la mkononi
WENZAKE WAMKIMBIA
Akaendelea kusema: “Wale
wenzangu baada ya kunifikisha hapa na kuondoka sijawaona tena mpaka
leo. Sina msaada wowote, sina ndugu wa kunisaidia, sina mawasiliano na
watu wa nyumbani Tanga.
“Najisikia vibaya sana
kwa sababu mtuhumiwa alikimbia muda uleule aliponifanyia ukatili huu.
Kikubwa ninamwomba Mungu anisaidie kwani yeye ndiye anayejua cha
kunifanyia.”
Moja ya jeraha alolipata mguuni.
ANAHITAJI MSAADA
Hanafi anaomba msaada
kwa Watanzania waweze kumsaidia chochote kwa sababu mpaka sasa mwezi
mmoja na zaidi umepita akiwa hospitalini hapo kwa kusaidiwa na manesi
kwa kuwa hana mtu wa kumuuguza.
0 comments:
Post a Comment