Home » » Mbeya: Binti Akamatwa kwa Alichokiandika Facebook .

Mbeya: Binti Akamatwa kwa Alichokiandika Facebook .

Mtu mmoja anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Mbeya kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mtandao wa Face book.

Mtuhumiwa huyo aliyefahamika kwa jina la Carolne Kajela, alikamatwa jioni ya desemba 12, mwaka huu eneo la Uyole Jijini hapa, baada ya kuandika katika ukurasa wake wa Facebook kupitia kundi la Kwinyara Let’s talk kuwa, mmiliki wa mabasi ya Rungwe Express anaingiza mabasi hayo kupitia taasisi ya dini.

“Mtumbua majipu atumbue na hili.. mmiliki wa mabasi ya RUNGWE EXPRESS anapitisha mabasi kupitia taasisi moja ya kidin imbombo... jilipo,” unasomeka ujumbe huo, ambao mpaka anakamatwa ulikuwa umependwa na watu 35 na kuchangiwa maoni na watu 120

Taarifa kutoka ndani ya jeshi la polisi zinasema baada ya mtuhumiwa huyo kukamatwa na kuhojiwa, amekiri kosa na kuomba asamehewe kwani shetani alimzidi.

Mmiliki wa mabasi hayo Yohana Sonelo, alipohojiwa amekiri kampuni yake kupeleka mashitaka polisi na kwamba wanahitaji athibitishe alichokiandika mtandaoni, lasivyo sheria ya makosa ya mtandao namba 14 ya mwaka 2015 ambayo ilianza kutumika Septemba Mosi mwaka huu ifuate mkondo wake.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kumkamata mtuhumiwa huyo na kwamba taratibu za upelelezi zinaendelea kisha watapeleka jalada kwa mwanasheria wa serikali ili mtuhumiwa afunguliwe mashitaka na afikishwe mahakamani.
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog