Mch
Edward mseve wa kanisa T.A.G ushirika wa
uyole amesikitishwa na kitendo
kilichofanywa na vijana ambao ni waendesha bodaboda baada ya kuvuruga utaratibu wa ibada maalum
ya mazishi katika kanisa hilo siku ya leo
Hayo
yametokea baada ya kijana mmoja ambaye ni mwendesha bodaboda alifahamika kwa
jina la Gabriel Ngalele kufariki dunia
na mch mseve kuanza ibada ya mazishi kanisani
Wakati ibada
inaendelea vijana ambao ni waendesha bodaboda wapatao 300 walivamia kanisani
hapo na kuchukua mwili wa marehemu huyo kwa nguvu na kuupeleka sehemu ya
makaburini kwa ajiri ya maziko
Aidha vijana
hao Wakiwa makaburini waliendesha
ibada na hatimaye kuuzika mwili huo
Mch mseve
ameeleza kuwa wengi wa vijana hao walikuwa walevi na wavuta bangi kwani baada ya kuwatuliza vijana hao waache
kupiga kelele wakiwa kanisani kwa ajiri ya maombi walianza kuhamaki na kitu ambacho amedai kuwa huenda ndo
kimechangia kuichukua maiti hiyo bila kufuata utaratibu
Mch huyo
ameongeza kuwa hawezi kuchukua hatua zozote kwani hawajamdhulu kwa lolote huku
akinabaisha kuwa hayo yote amemwachia mungu ashugulike na suala hilo
Hata hivyo
kwa upande wake wa jeshi la polisi mkoani mbeya lilijaribu kutuliza kitendo
hicho lakini lilishindwa kuwadhibiti vijana hao kutokana na wingi wa mabodaboda hao.
0 comments:
Post a Comment