Home » »

JAMANI MANABII NA MITUME KWELI HAYA NDIO MAOMBI KULA MANYASI? MWE WAPENDWA KUWENI MAKINI

Mdada akila majani ambayo huduma hiyo wanasema ni chakula kutoka mbinguni mwe!
Kuna mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa kuhusu huduma za watumishi mbalimbali, moja wapo ni hii huduma iitwayo Rabboni Centre ministries iliyopo Pretoria nchini Afrika ya kusini, huduma hii iliyochini ya mwanzilishi wake mwalimu ,mchungaji na nabii Daniel Lesego ilianza mwaka 2002. Ni huduma ambayo kwa watu wasioabudu hapo huitilia mashaka kutokana na mwenendo wake.

Kwasasa wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na hatimaye wanaishia kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo akisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.


Inaelezwa kwamba mara baada ya maombi waumini wengi huanza kutapika jambo ambalo kanisani hapo huashiria kwamba mtu amejazwa Roho Mtakatifu.


Lakini kama haitoshi nabii Lesego hufanya maombi huku amewakanyaga watu. Huduma hii imekuwa gumzo nchini humo na nchi jirani kwa jinsi mambo yao yanavyokwenda.


Mnasemaje watumishi kuhusu jambo hili? mwe kula manyasi kweli? mma!


Hapa nabii huyo akikanyaga watu kama njia ya mafundisho yake.
Haa!! angalia jamani, sasa ng'ombe watakula nini jamani???
Mungu tufunulie macho ya rohoni kuyajua mambo haya kama ni wewe au sisi kha!
Hajamaliza bado.
Baada ya manyasi ni mwendo wa kutapika sasa
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

NURU FM 93.5 IRINGA

.

.

.

Nyali

Pages

Pages

Powered by Blogger.

Blog Archive

Search This Blog